Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,865
- 6,362
Uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro unapenda kuufahamisha umma kuwa haumtambui ndugu Lembruce Mchome kama Mwenyekiti wa Jimbo la Mwanga, kinyume na jinsi anavyojitambulisha katika shughuli mbalimbali.
Aidha, uongozi unapenda kuutaarifu Umma kuwa Mwenyekiti halali anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa ni Mhe. Kirua Hassani Msangi, ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutekeleza majukumu ya uongozi wa Jimbo la Mwanga kwa mujibu wa taratibu na maamuzi halali ya uongozi husika.
Soma Pia: Chadema yamlima barua Mchome, yamtaka ajieleze ndani ya siku 14
Hivyo, wananchi, wanachama na wadau wote wanashauriwa kupuuza taarifa, matamko au utambulisho wowote unaotolewa na ndugu Lembruce Mchome kwa kujinasibisha na nafasi hiyo, kwani hautambuliwi na uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro.
Aidha, uongozi unapenda kuutaarifu Umma kuwa Mwenyekiti halali anayekaimu nafasi hiyo kwa sasa ni Mhe. Kirua Hassani Msangi, ambaye ndiye mwenye mamlaka ya kutekeleza majukumu ya uongozi wa Jimbo la Mwanga kwa mujibu wa taratibu na maamuzi halali ya uongozi husika.
Soma Pia: Chadema yamlima barua Mchome, yamtaka ajieleze ndani ya siku 14
Hivyo, wananchi, wanachama na wadau wote wanashauriwa kupuuza taarifa, matamko au utambulisho wowote unaotolewa na ndugu Lembruce Mchome kwa kujinasibisha na nafasi hiyo, kwani hautambuliwi na uongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro.