The Humble Dreamer
JF-Expert Member
- Oct 12, 2015
- 8,011
- 11,429
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema kuwa licha ya hali ya uchumi duniani kuendelea kuyumba, Tanzania imeonyesha uimara kwa kuendelea kukuza uchumi wake kwa kasi na ustahimilivu wa hali ya juu.
Akitoa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa mwaka 2024 na Mpango wa Maendeleo kwa mwaka wa Fedha 2025/2026 bungeni jijini Dodoma leo, Alhamisi Juni 12, 2025, Profesa Mkumbo alisema mafanikio hayo yanatokana na usimamizi makini wa sera pamoja na mshikamano wa Watanzania katika kujenga uchumi wa Taifa.
“Nihitimishe kwa kulihakikishia Bunge lako tukufu kuwa hali ya uchumi wa nchi yetu kwa sasa ni himilivu, ukiwa na mwelekeo chanya na ukuaji endelevu. Kuimarika kwa uchumi kunatokana na usimamizi makini wa sera za uchumi jumla, pamoja na ushiriki wa wananchi wote katika ujenzi wa Taifa. Ninawashukuru na kuwapongeza Watanzania wote kwa mshikamano huu wa kizalendo,” amesema Profesa Mkumbo.
Profesa Mkumbo amebainisha kuwa licha ya changamoto za kiuchumi duniani, Tanzania imeendelea kuvutia wawekezaji na kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati katika sekta mbalimbali zikiwemo miundombinu, nishati, kilimo na afya -hatua ambazo zimechangia ustawi wa uchumi wa Taifa.
