tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 25,867
- 25,193
Wiki iliyopita Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, profesa Sifuni Mchome, aliweka hadharani muundo mpya wa upangaji wa madaraja ambapo alitangaza kufuta daraja la sifuri na kuanzisha daraja la tano.
Baadaye aliibuka Naibu Waziri wa Elimu,Philip Mulugo na kumkana Prof Mchome--kwamba ni muongo--hayo madaraja amejitungia mwenyewe akiwa na mkewe nyumbani kwake, kwa hiyo hakuna kitu kama hicho kilichotangazwa na Profesa!
Mh. William Lukuvi alimtetea vikali sana Mulugo (Serikali) kwamba yuko sahihi na kuonya kuwa Prof Mchome (Raia) ni muongo mkubwa! Lukuvi aliwataka wananchi wamuamini Mulugo kwa kuwa yeye ni Serikali tofauti na Prof Mchome ambaye ni raia wa kawaida. Hii inaleta picha kwamba madaraja mapya yaliyotangazwa na Prof Mchome ni mawazo yake binafsi na hayajawahi kujadiliwa na mtu yeyote ndani ya Wizara ya Elimu.
Kufuatia sintofahamu na kizungumkuti hiki, Profesa Mchome anapaswa kuachia ngazi kwa kulitangazia Taifa uongo kwa sababu anazozijua yeye. Yaani Profesa huyu aketi nyumbani na mkewe waamue kutunga madaraja mapya ya ufaulu na kuutangazia umma wa watanzania kinyume cha sheria halafu aachwe aendelee kuongoza wizara hii nyeti? Haiwezekani hata kidogo-- anapaswa kuachia ngazi mara moja.
Hatuwezi kukubali kuona Wizara ya Elimu ikiongozwa na profesa uchwara kama huyu Mchome.
Baadaye aliibuka Naibu Waziri wa Elimu,Philip Mulugo na kumkana Prof Mchome--kwamba ni muongo--hayo madaraja amejitungia mwenyewe akiwa na mkewe nyumbani kwake, kwa hiyo hakuna kitu kama hicho kilichotangazwa na Profesa!
Mh. William Lukuvi alimtetea vikali sana Mulugo (Serikali) kwamba yuko sahihi na kuonya kuwa Prof Mchome (Raia) ni muongo mkubwa! Lukuvi aliwataka wananchi wamuamini Mulugo kwa kuwa yeye ni Serikali tofauti na Prof Mchome ambaye ni raia wa kawaida. Hii inaleta picha kwamba madaraja mapya yaliyotangazwa na Prof Mchome ni mawazo yake binafsi na hayajawahi kujadiliwa na mtu yeyote ndani ya Wizara ya Elimu.
Kufuatia sintofahamu na kizungumkuti hiki, Profesa Mchome anapaswa kuachia ngazi kwa kulitangazia Taifa uongo kwa sababu anazozijua yeye. Yaani Profesa huyu aketi nyumbani na mkewe waamue kutunga madaraja mapya ya ufaulu na kuutangazia umma wa watanzania kinyume cha sheria halafu aachwe aendelee kuongoza wizara hii nyeti? Haiwezekani hata kidogo-- anapaswa kuachia ngazi mara moja.
Hatuwezi kukubali kuona Wizara ya Elimu ikiongozwa na profesa uchwara kama huyu Mchome.