Profesa Kitila Mkumbo: Waziri Ndalichako hana mamlaka ya kupanga sifa za kujiunga na chuo kikuu

Lizaboni pia umeng'ara mwezi huu post5 per day kila post buku 7
5x30=150
7000x150=to 850'000pesa nzuri kwa kazi ya kukaa nyuma ya PC na kupst tu iwe points au pumba hongera
Hicho ni kiwqngo kidogo sana kustahili kulipwa Lizaboni. Mapato yangu ni zaidi ya kiasi hicho
 
ila mbele ya wanasiasa hafurukuti. unasema wameng'ara hao wengine, hivi wameng'ara au wametangazwa sana na vyombo vya habari? Nijuavyo mm kung'ara ni kufanya jambo lenye.manufaa kwa jamii inayokuzunguka na wala sio kutangazwa sana. Kuna wakati magaidi wanatangazwa sana baada ya kufanya mauaji, nayo ni kung'ara? Ama inatokea ajali mbaya sana inatangazwa sana.nato utasema ajali zimeng'ara sana? Ama mfano mrahisi kwako, Shigongo ameng'ara mwezi huu?
Ni heshima tu kwa kiongozi wako. Ila kwenye majukumu yake yupo vizuri sana
 
Dr. Bana ndio akamaliza kabisa. Amesema yeye anawajua Ma-Professor zaidi ya 20 ambao hawakupitia kidato cha 6. Pia akaongeza kuwa hata yeye(Dr. Bana) hakuwahi kufika kidato 6. Mwisho akamalizia kwa kusema, hata Prof. Mathew Luhanga, ambaye alishika nafasi ya Makamu Mkuu wa Chuo pale UDSM kwa miaka 14, hakuwahi kufika kidato cha 6. Hivyo hoja ya Prof. Ndalichako haina mashiko.

Hii inathibitisha ile methali ya Kiswahili isemayo "ujuaji mwingi mbele kiza".
 
  • Thanks
Reactions: mij
Nimemsikia Profesa Kitila Mkumbo na nimemuelewa vyema,

Profesa Ndalichako kama aliropoka hivyo alivyonukuliwa basi ndio walewale kama Profesa Lipumba.

Nitarudi......

Profesa Kitila Mkumbo uko sahihi kabisa. Suala la sifa za kujiunga chuo kikuu au chuo chochote ni suala la SERA YA ELIMU na si matamko ya viongozi wa kisiasa. Kiongozi wa Kisiasa anaweza kukazia utekelezaji wa sera- na si kutoa matamko ambayo hayapo kwenye sera
 
wanajiandaa kuto matamko ili wakishindwa kuleta viwanda wapate cha kusema, ila naona mkwamo ni mkubwa
 
Hata ww ukivua nguo zote ukazunguka kariakoo utang'ara tu.Swali ni je umeng'ara kwa lipi?
 
Nimemsikia Profesa Kitila Mkumbo na nimemuelewa vyema,

Profesa Ndalichako kama aliropoka hivyo alivyonukuliwa basi ndio walewale kama Profesa Lipumba.

Nitarudi......

Hiyo ni nadharia. Rejea Musoma Resolution.
 
Ndalichako kila wiki anatoa tamko. Apunguze kelele apige kazi zitaonekana tu kelele hazisaidii elimu ya tanzania bado duni kabisa.

Ndalichako nyamaza sasa maana kuna matamko hata huyakumbuki tena. Tumeshachoka kukusikia kila saa
 
Kwa aandiko lako hilo Lizbon, nimeanza kumuelewa Malisa G Malisa. "Kuwa Ccm inahitaji uwe mjinga kiwango cha lami"Kung'ara siyo tatitzo, TATIZO ni umeng'ara kwalipi? hata Scorpion aling'ara sana miezi kazaa iliyopita. Nirudi kwa Makonda na Ndalichako, Makonda siwezi mzungumzia sana kwani ni kujidharirisha kwa upande wangu, Kwa upande wa mamaangu Ndalichako huyo naye anathibitisha msemo wa wanasayansi kwamba " usafi wa kitu nipamoja na chombo kilichobeba kitu husika" maana yake huwezi kuwa na maji safi kwenye kikombe kichafu. Ndalichako alikuwa kiongozi mzuri sana Hapo awali ila kwa sasa ameanza kupoteza muelekeo, matamko yake yamekuwa mengi sana tena wasiyo na tafti ,kwa sasa anakotupeleka ndalichako kama hatoangaliwa kwa makini ni kubaya sana, kwahiyo Lizbon tumkemee badala ya kumsifu na kumpongeza.Matamko ya diploma na mengine kama hayo binafsi yananipa shida sana kuyaelewa tunahitaji kuyakemea kwani yanaturudisha kwenye centralized system of Education tukitoka kwenye Decentralized system. Athali kubwa ya mfumo ambao Ndalichako anataka kuweka ni kwa watoto wa maskini ambao wengi wao hawana mazingira rafiki pengine ya kuwafanya kwenda direct huko wanakokutaka.
 
Hapa karibuni waziri Ndalichako alinukuliwa akitoa tamko (ambalo kwa tafsiri nyepesi tuu ndilo tamko la serikali) la serikali kukusudia kufuta mfumo wa kudahili wanafunzi elimu ya juu wale waliopitia mfumo wa ngazi ya cheti na stashahada (Diploma). Uamuzi/tamko hili limepingwa na kukosolewa vikali na watu mbalimbali ikiwemo wanazuoni wa kuheshimika nchini.

Sauti hizi zimebeba ujumbe mmoja tuu, kwamba waziri anaongoza wizara kukabiliana na matatizo makuu ya mfumo wetu wa elimu pasipo kujua chanzo hasa ni nini. Yeye ameona vyanzo kuwa ni uvaaji majoho holela na udahili wa wanafunzi wasiopitia kidato cha sita kuwa ndiyo msingi na chimbuko la elimu kudorora nchini.

Kweli? Binafsi sikutegemea fikra kama hizi zitoke kwa mtu ambaye amekuwa sehemu nyeti ya sekta ya elimu kwa kipindi kirefu. Mimi binafsi namkumbuka alipokuwa katibu mkuu wa Baraza la Mitihani la Taifa ambapo amehudumu na nina uhakika ameshiriki au kupata taarifa mbalimbali za tafiti kutoka tume mbalimbali zilizoundwa kuchunguza madudu kwenye sekta ya elimu.

Pengine huyu dokta hakujua kuwa tatizo la elimu yetu sii kama anavyodhani, bali ni mfumo mzima ambao hauwekwa sawa. Mfumo wa elimu usio na mitaala mpaka sasa (curriculum), elimu ya vyuo inayowafundisha watu nadhalia zaidi kuliko vitendo ambapo mpaka leo hakuna msomi hata mmoja, kwa mfano, aliyeandika kitabu cha somo la uchumi. Ni mfumo wa nadhalia tuu umejaa vyuoni.

Kwa nini mimi kama Rais nisimfute kazi mtu huyu? Mtu anayejaribu kutuaminisha kuwa anafanya kazi kwa nguvu kumbe ni kinyume? Ina maana mtu mwenye diploma hana uwezo kiutendaji kuliko mwenye kidato cha sita? Ni nini kilimpata huyu mama mpaka akafikia maamuzi haya? HAPANA, kama ambavyo ningeweza kumtumbua mama Kilango kwa kutotoa taarifa ya mtumishi hewa hata mmoja, huyu basi nisingejiuliza usiku kucha! Ningemtumbua aisee, sitanii.

Tanzania leo inahitaji mabadiliko makubwa kwenye kila sekta; afya, elimu, mawasiliano, usafirishaji nk nk. Lakini mageuzi hayo hayawezi kufanywa bila kuwa na a well-designed master plan. Hatuwezi kufaya mageuzi bila upembuzi yakinifu hata siku moja. Sekta ya elimu ni sekta nyeti sana ambayo maamuzi yoyote ya hovyo yataathiri taifa kwa miaka mia ijayo

Ningekuwa Rais ningemfutilia mbali huyu waziri
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Siku zote mtu akijituma hakika matunda yake hupatikana kwa muda mfupi. Vivyo hivyo kwa upande wa wanasiasa na watendaji wa Serikali. Kadri wanavyojituma ndivyo wanavyokuwa na faida kubwa katika jamii wanayoitumikia.

Si siri, Profesa Joyce Ndalichako na Paul Makonda wameutendea haki yake Mwezi Novemba ambao kwa hakika ni lala salama katika kuelekea mwaka mpya wa 2017. Wametimiza wajibu wao na wananchi wamewakubali. Hii haina maana kuwa mawaziri na watendaji wengine hawajafanya kazi zao. Hapana. Wamewajibika kwa upande wao ila kama kawaida kila penye watu wengi lazima atapatikana mmoja wa kuwazidi wenzake.

Hongera sana Mama yetu Prof Ndalichako na ndugu yetu Paul Makonda kwa kazi nzuri mliyofanya kwa mwezi Novemba. Naamini kuwa mwezi Desemba mtafanya kazi mara mbili zaidi ya mlivyofanya sasa. Wananchi tunawaunga Mkono
Kwa makonda sio mbaya sana Ila maza kapoteza anakurupuka nalazima akane anachokiamini na ndo kupoteza kwenyewe..
 
Back
Top Bottom