Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
Prof. Tibaijuka ahamishia kibao kwenye 'beacons’
Monday, 17 January 2011 19:30 newsroom
NA NJUMAI NGOTA
BAADA ya moto kuwashwa kwa wavamizi wa viwanja vya umma (wazi) na waliojitwalia maeneo ya hifadhi ya mikoko, kibao sasa kimehamia kwa watu waliojenga juu ya mawe ya alama za mipaka ya viwanja (beacons).
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameagiza waliojenga juu ya mawe hayo kubomoa kilichojengwa, kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.
Alitoa agizo hilo jana, akieleza kukerwa na baadhi ya watu waliojenga kuta juu ya mawe ya alama na wengine kuziweka ndani ya uzio wa nyumba zao.
Profesa Anna akizungumza kwa njia ya simu, alisema hivi karibuni alitembelea maeneo ya Mbezi, Dar es Salaam, ambako alikuta sheria za ujenzi zimekiukwa.
Nilipita maeneo ya Mbezi, niliona watu wamejenga uzio na mawe ya alama yakiwa ndani. Maeneo hayo yamepimwa kama ilivyo Sinza, mawe yanatakiwa yawe nje ya ukuta,Ó alisema.
Alisema atatuma watendaji kufanya ukaguzi katika maeneo hayo, akionya kuwa, wasiofuata taratibu za ujenzi watavunjiwa.
Profesa Anna alisema sheria inatoa adhabu kwa kosa la aina hiyo, ambayo ni kifungo cha miaka sita jela. Alisema kila mtu akitaka eneo lake liwe kubwa, wataziba hata njia za watu kupita.
Kwa mujibu wa Profesa Anna, anachofanya hivi sasa ni kutoa elimu kwa wananchi ili watambue umuhimu wa makazi na kufahamu sheria na kwamba, serikali haimkomoi mtu.
Desemba 14, mwaka jana, Profesa Anna aliamuru kuvunjwa kuta na jengo lililokuwa jirani na hoteli ya Palm Beach na lingine lililokuwa eneo la Ocean Road, kutokana na kujengwa kinyume cha sheria.
Kuta hizo na majengo yaliyokuwa ndani yalivunjwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Profesa Anna Desemba 30, mwaka jana, aliagiza wananchi waliojitwalia na kujimilikisha maeneo ya hifadhi ya mikoko, kubomoa nyumba zao la sivyo bomoabomoa itawakumba.
Wizara hiyo hivi karibuni ilifuta viwanja batili 44 viliyopo kwenye hifadhi ya mikoko, eneo la Jangwani Beach na kuwaagiza waliojimilikisha kubomoa majengo yao.
Monday, 17 January 2011 19:30 newsroom
NA NJUMAI NGOTA
BAADA ya moto kuwashwa kwa wavamizi wa viwanja vya umma (wazi) na waliojitwalia maeneo ya hifadhi ya mikoko, kibao sasa kimehamia kwa watu waliojenga juu ya mawe ya alama za mipaka ya viwanja (beacons).
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, ameagiza waliojenga juu ya mawe hayo kubomoa kilichojengwa, kabla ya hatua za kisheria kuchukuliwa dhidi yao.
Alitoa agizo hilo jana, akieleza kukerwa na baadhi ya watu waliojenga kuta juu ya mawe ya alama na wengine kuziweka ndani ya uzio wa nyumba zao.
Profesa Anna akizungumza kwa njia ya simu, alisema hivi karibuni alitembelea maeneo ya Mbezi, Dar es Salaam, ambako alikuta sheria za ujenzi zimekiukwa.
Nilipita maeneo ya Mbezi, niliona watu wamejenga uzio na mawe ya alama yakiwa ndani. Maeneo hayo yamepimwa kama ilivyo Sinza, mawe yanatakiwa yawe nje ya ukuta,Ó alisema.
Alisema atatuma watendaji kufanya ukaguzi katika maeneo hayo, akionya kuwa, wasiofuata taratibu za ujenzi watavunjiwa.
Profesa Anna alisema sheria inatoa adhabu kwa kosa la aina hiyo, ambayo ni kifungo cha miaka sita jela. Alisema kila mtu akitaka eneo lake liwe kubwa, wataziba hata njia za watu kupita.
Kwa mujibu wa Profesa Anna, anachofanya hivi sasa ni kutoa elimu kwa wananchi ili watambue umuhimu wa makazi na kufahamu sheria na kwamba, serikali haimkomoi mtu.
Desemba 14, mwaka jana, Profesa Anna aliamuru kuvunjwa kuta na jengo lililokuwa jirani na hoteli ya Palm Beach na lingine lililokuwa eneo la Ocean Road, kutokana na kujengwa kinyume cha sheria.
Kuta hizo na majengo yaliyokuwa ndani yalivunjwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.
Profesa Anna Desemba 30, mwaka jana, aliagiza wananchi waliojitwalia na kujimilikisha maeneo ya hifadhi ya mikoko, kubomoa nyumba zao la sivyo bomoabomoa itawakumba.
Wizara hiyo hivi karibuni ilifuta viwanja batili 44 viliyopo kwenye hifadhi ya mikoko, eneo la Jangwani Beach na kuwaagiza waliojimilikisha kubomoa majengo yao.