Prof. Muhongo -> SYMBION -> Kikwete ->

Prof. Muhongo -> SYMBION -> Kikwete ->

Status
Not open for further replies.
Wakuu,

Kuna sekeseke linaendelea chini kwa chini ambalo likifumuka linaweza kupelekea Prof. Muhongo kuhamishwa Wizara au kupoteza nafasi yake.

Kifupi ni kuwa jamaa kaingilia maslahi ya wakubwa na kwa sasa mambo si mambo. Tutayasikia ya kusikika muda si mrefu.

Nimeandika ili wajue tayari tumejua, tuna taarifa za ndani zaidi na tunafahamu kinachoendelea kati yetu na wamarekani.


Nadhani mheshimiwa alikuwa hamfahamu vizuri mh Muhongo. Ni unadulterated product ya Mwalimu Nyerere.
Hawa jamaa wa ukanda wa ziwa pasenti kubwa hawana tamaa ya pesa na ni waadilifu. Enzi za Mwalimu walijaa Ikulu na kwenye system nzima ya security ndiyo maana hata rushwa ilikuwa ngumu kupokea.
Hawa hupenda kuacha MARK katika utendaji wao.
Big up Mh. Muhongo!
Wakikuhamisha wizara kataa, rudi ulikotoka wasije wakakubenea!
 
Njia mojawapo inayotumiwa na CIA kujipenyeza katika nchi ni kupitia miundombinu. Hawa wenzetu wana ujanja kutuzidi.
Wakishashika nguzo za umeme watatafuta kingine tena lakini lengo lao ni kuiweka nchi kiganjani. Itafika mahali wanasiasa wetu wanajikuta hawawezi kufanya maamuzi independently. Ndio maana kuna mahali nimesema haya madhara aliyotuletea Kikwete yatatuandamana hata miaka 30 baada yake kutoka mamlakani. It is a shame.

Slaa akizungumza mnamwona punguani mwenye tamaa ya madaraka.
 
Dawa ya kusavive kwenye
Chama Kigumu ni kusimamia hoja yako na sio matakwa ya mtu hata kama mtu
huyu ni JK mwenyewe. Kitakacho mfanya Prof. aendelee kuongoza wizara
hiyo ni hicho tu. Awatumie wataalam wake vizuri na apime hoja zao then
atoe maamuzi ambayo roho yake imeridhika nayo.

ku 'survive' siyo savive!
 
Njia mojawapo inayotumiwa na CIA kujipenyeza katika nchi ni kupitia miundombinu. Hawa wenzetu wana ujanja kutuzidi.
Wakishashika nguzo za umeme watatafuta kingine tena lakini lengo lao ni kuiweka nchi kiganjani. Itafika mahali wanasiasa wetu wanajikuta hawawezi kufanya maamuzi independently. Ndio maana kuna mahali nimesema haya madhara aliyotuletea Kikwete yatatuandamana hata miaka 30 baada yake kutoka mamlakani. It is a shame.

Jasusi,

Ummeacha hata hizi NGO, ukikuta inafadhiliwa na hawa mmekufa, hata hawa mlioshangilia wamekuja ni wale wale, I mean PEACE CORP.

Unacheza na hawa muziki kwa mwendo wa kasi
 
Jasusi,

Ummeacha hata hizi NGO, ukikuta inafadhiliwa na hawa mmekufa, hata hawa mlioshangilia wamekuja ni wale wale, I mean PEACE CORP.

Unacheza na hawa muziki kwa mwendo wa kasi

PEACE CORPS, PEACE CORPS!; Hawa wamekuja kujifunza kiswahili na kuichunguza nchi hata kwenye peripheral areas disguising as volunteers. Siyo siri lakini serikali imelala tu.
 
walioonyesha mapungufu ya wazi kama vile Jairo bado hawajachukuliwa hatua jambo ambalo linatia mashaka kama kweli serikali ya sasa ina nia kweli ya kukomeha ufisadi? au anayetaka kukomesha ufisadi ndo anakuwa adui.
 
Symbion is owned by a former CIA operative. We know that once you work for CIA you will always be CIA.
Sasa CIA wameshapata upenyo ndani ya Bongo kupitia urafiki wa Wilson na Kikwete. Mengine jazieni wenyewe.
Hakukosea sana Dr. Slaa aliposema kuwa Kikwete ni janga la taifa. Madhara yake kuwa mamlakani yatatuathiri kwa miaka mingine 30 ijayo.
Jamaa hatumii akili hata kidogo halafu ndo rahisi wa nchi,ye anadhani hawa watu ni kuwachekea.Very sad yani.

Hawa watu watakuja kujibu oneday,huwezi kuongoza nchi kama huna kichwa.
 
yaan maliasili na NISHATI hata malaika hawez kuja kuiongoza:sleepy:

Sure!
Wizara hii pamoja na nyingine kadhaa ziko katika 'Memorandum of Understanding' katika ya serikali na mafisadi. Wizara "ZAO" nyingine ni Fedha, Nishati na madini na PMO-RALG. Jiulize kwa nini ufisadi ni mkubwa sana katika halmashauri za wilaya na miji na serikali haimfuti mtu kazi, pamoja na Mrema kupiga kelele sana bungeni kwamba wabadhirifu wafutwe kazi.
 
Kuna watu wana uchungu na nchi hii. Watu wenye kupenda maendeleo kwa wote.

Profesa Muhongo alisema anataka kuleta mabadiliko makubwa ndani ya wizara yake ya Nishati na Madini kwa kuahidi kuwa hakutakuwa na umeme wa mgao tena! Sasa hivi tatizo hilo limerudi tena kwa kasi kubwa, mara tu baada ya vikao vya Bunge kwisha!

Ni akina nani hawa wanaomwangusha Profesa? Sasa hivi yanatimia yale aliyoyasema Mheshimiwa Zito Kabwe baada ya kuona mbali na kutoa sababu za mgao wa umeme kuendelea kuwepo. Baba akifa na kuacha mali kwa watoto dhaifu, mali yote husambaratika.
 
Njia mojawapo inayotumiwa na CIA kujipenyeza katika nchi ni kupitia miundombinu. Hawa wenzetu wana ujanja kutuzidi.
Wakishashika nguzo za umeme watatafuta kingine tena lakini lengo lao ni kuiweka nchi kiganjani. Itafika mahali wanasiasa wetu wanajikuta hawawezi kufanya maamuzi independently. Ndio maana kuna mahali nimesema haya madhara aliyotuletea Kikwete yatatuandamana hata miaka 30 baada yake kutoka mamlakani. It is a shame.

Kupigana haiepukiki maana wanjua wakitolewa madarakani wataishia kama kina Ceusesccu, na wengineo wa aina hiyo.
 
Jamaa hatumii akili hata kidogo halafu ndo rahisi wa nchi,ye anadhani hawa watu ni kuwachekea.Very sad yani.

Hawa watu watakuja kujibu oneday,huwezi kuongoza nchi kama huna kichwa.
Mimi huwa naogopa zaidi nikiangaliaga zile filamu zao za Holywood ambazo zinahusu mambo ya CIA wanaact kwa umahiri wa hali ya juu mpaka feelings zako zinaamini kama ndio matukio halisi, sasa je wale CIA wenyewe halisi wenye kazi yao huwa wanafanya kazi kwenye viwango gani?
 
Waiting for Amerika to speak out about this very soon.........
 
Mimi huwa naogopa zaidi nikiangaliaga zile filamu zao za Holywood ambazo zinahusu mambo ya CIA wanaact kwa umahiri wa hali ya juu mpaka feelings zako zinaamini kama ndio matukio halisi, sasa je wale CIA wenyewe halisi wenye kazi yao huwa wanafanya kazi kwenye viwango gani?

Mkuu unachokiona kwenye movie ni almost the same wanavyofanya kwenye matukio halisi.Kama propaganda ni kidogo sana.Hao watu si mchezo mkuu.Viongozi wetu kazi yao wao kucheka cheka tu.
 
Jasusi,

Ummeacha hata hizi NGO, ukikuta inafadhiliwa na hawa mmekufa, hata hawa mlioshangilia wamekuja ni wale wale, I mean PEACE CORP.

Unacheza na hawa muziki kwa mwendo wa kasi

Hivi TISS wana kazi gani jamani. Yaani mpaka leo hawazijuwi mbinu za Wamarekani miaka yote kiasi kwamba watu tusio wa usalama wa taifa tunaelewa? Maana wanawaacha tu wanaingia tu na kuendelea kutunyonya tu. Wamarekani hawana huruma maana hii ni sawa na kumkamua panya (milking a rat while you are a rich person who own thousand of cows).
 
Hivi TISS wana kazi gani jamani. Yaani mpaka leo hawazijuwi mbinu za Wamarekani miaka yote kiasi kwamba watu tusio wa usalama wa taifa tunaelewa? Maana wanawaacha tu wanaingia tu na kuendelea kutunyonya tu. Wamarekani hawana huruma maana hii ni sawa na kumkamua panya (milking a rat while you are a rich person who own thousand of cows).
Matajiri wakubwa wa marekani hawawaonei huruma wananchi wao masikini ndo waje kutuonea sisi "makima wa msituni" huruma?

Upumbavu na ujinga utaendelea kutu cost milele kwa style hii.
 
NJOZI
Ni kweli Marekani na Asasi yake ya Kijasusi wana nguvu za kiuchumi, kijasusi na hata kiteknolojia na kwamba pamoja na kusudio la kuhakikisha kuwa Marekani inakuwa nchi yenye maendeleo kwa watu wake, bado agenda ya njozi ya kutaka nchi yao iendelee kuwa ‘kiongozi na askari wa dunia' inawasumbua baadhi ya Wamarekani. Hata inapokuja kwenye kumtafuta nani awe Rais wao, huwa wanapenda kuwauliza wagombea hilo swali la hiyo njozi ingawa kwa namna tofauti tofauti.

HALI HALISI
Pamoja na nguvu na njozi zao, ni imani yangu kuwa nchi nyingine kama za kwetu pamoja na kuonekana ‘wadogo' kwa mataifa hayo ‘makubwa', si kweli kuwa hatuna kabisa sauti juu ya mambo kama haya ya UBADHILIFU wa wazi, maana watu wamekuwa na ulewa mkubwa na haki za binadamu zinatetewa kila mahala hata ndani yanchi ‘zilizoendelea' ambako kuna wananchi wengi sana (nguvu ya umma) ambao hawataki kuona Mataifa yao yajulikane kwa uovu na kuchukiwa na mengine kutokana na uonevu au wizi. Sote tunakumbuka hata suala la RADA likivyoanza kupigiwa kelele Uingereza, kabla ya sisi wenyewe hatujafikia kiasi hicho!

Hata wao si wajinga; wakikumbana na msimamo mkali unatoka kwa mtu mmoja (hata awe Rais au Waziri) au kikundi cha wachache tu basi wanapata nguvu ya kuwashawishi wengine wengi wanaobaki na hakika mwisho wa siku misimamo kama hiyo lazima ishindwe (at least in that material time); lakini wanapogundua kuwa Rais au Waziri anamsimamo mkali na mihimili yote ya dola inamuunga mkono plus wananchi (walio wengi), amini kuwa hakuna cha shirika la kijasusi wala nini hata wao hurudisha siraha nyuma wakiomba dua kusubiria upepo ubadilike!


HATUA:
Kwa vile suala la uzalishaji wa umeme wa nyongeza wa haya majenereta ya Syimbion na mikataba ya huko nyuma toka Richmond haina tija na inatia hasara TANESCO & Taifa letu kwa ujumla waziwazi, nashauri Katibu na Waziri mwenye dhamana kuwapa kazi watathmini wazawa wenye ujuzi na maadili toka hata UDSM & IFM to undertake a in-depth technical & financial appraisal kisha Waziri awasilishe kauli yake kwenye Baraza la Mawaziri na kisha Bungeni juu ya matokeo ya hiyo tathmnini na mapendekezo ya maamuzi magumu ya kuiokoa TANESCO kutokana na makucha ya haya makampuni, mikataba mibovu pia kesi ile kesi isioisha inayosimamiwa na Mh. Mkono & Advocates; halafu wananchi tuone ni nani anayepinga ambaye yuko upande wa hayo makampuni! Kwa kufanya hivi itabidi waamuwe kutupa a fair deal au waondoke, tununue majereta yetu wenyewe! Muda wa kututisha- a sovereign state na kulia lia sasa umekwisha. Kuwekewa vikwazo vya kiuchumi si lazima itangazwe UN, inawezwa kutangazwa kupitia mikataba mibovu, na kampuni kutuwekea mikwara tena ndani ya mipaka ya nchi yetu kwa kutunyima umeme na au kutuuzia kwa bei mbaya na kwa kutafuta support toka kwa wachumia-tumbo wachache wanaofikiri kuwa wanaweza kuwashawishi Wabunge wote kukubaliana na upuuzi huu!

Chukueni hatua sasa!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom