Prof Mchembe: Wanaoruhusiwa kutoa taarifa za Afya ni Waganga wa Mikoa na Wilaya siyo Wanasiasa

Kumbe fukuto la Waziri wa Afya kumtimua Daktari wa Wliaya Chunya limechukua sura nyingine...
Na Chalamila nae amekuwa msemaji wa wizara kule Mbeya.

Bado naona majaribio ya uongozi kwenye hii awamu ya tano tena.

Juzi Dmo huko Mbeya katoa taarifa ya mlipuko waziri kapaa nae.

Leo Katibu mkuu anasema Dmo ana mamlaka ya kutoa taarifa za wilaya yake.

JPM alifanya makosa makubwa sana kuweka safu isiyo na uzoefu. Wachumia tumbo.

Hebu ona Lukuvi na Mkuchika wanavyo toa maamuzi yao kwa busara..
 
Kadhalika Prof Mchembe amesema Corona ni ugonjwa wa mlipuko wa maambukizi kwa njia ya hewa kama ilivyo chorela kwa mfumo wa chakula.

Source ITV habari
Sasa kwanini huwa tunakuwa serious kwenye response ya Cholera (emergency operation centers, vituo vya karantini, daily data updates kutoka kila wilaya etc) ila kwenye corona tunasema haipo ipo haipo?

Prof. Mchembe kuna kitu anatamani kusema/kufanya ila uongozi wa Nchi bila shaka haupo tayari
 
Sasa kwanini huwa tunakuwa serious kwenye response ya Cholera (emergency operation centers, vituo vya karantini, daily data updats kutoka kila wilaya etc) ila kwenye corona tunasema haipo ipo haipo?

Prof. Mchembe kuna kitu anatamani kusema/kufanya ila uongozi wa Nchi labda haupo tayari
Labda!
 
Kumbe fukuto la Waziri wa Afya kumtimua Daktari wa Wliaya Chunya limechukua sura nyingine.

Profesa Mchembe, Katibu Mkuu Wizara ya Afya amesema rasmi kuwa ni jukumu la madaktari wa Wilaya na Mkoa kutoa taarifa za magonjwa ya milipuko ndani ya maeneo yao na si wanasiasa, akimaanisha Waziri.

Tamko hilo la Serikali ni kama kumweka katika nafasi yake Dr Dorothy Gwajima kuwa alivurunda kwa kumtimua Daktari wa Wilaya ya Chunya.
Sasa hao RMO au DMO wathubutu kutoa taarifa ya corona; hapo ndipo utakapoona vurugu 'match'.

Hivi huyo Katibu Mkuu wa Afya ni Profesa wa vitu gani?
Naona anajichanganya sana. Naye kaokotwa "Jalalani"?
 
serikali inapenda kusifiwa tu, huku ikificha aibu zake. Angalia walivyoumbuka Angola, wanapeleka Corona huko, wanazuiwa airport kwamba rudisheni ujinga wenu kwenu.
 
Prof.
Heshima kuu kwako!! Nina maswali machache ambayo naomba kama una wasaa utusaidie na ikiwezekana nawe unisikilize labda naweza kukufaa kwa leo.

Kwanza binafsi na kwa uelewa wangu na elimu kidogo niliyo nayo kuliza swali kuwa corona ipo au haipo kwa Tanzania ni kama kuuliza "mama mkwe kavaa nguo ya ndani ya rangi gani",hivyo sitauliza swali hilo.
  1. WHO wasema kuwa hamjatoa takwimu za corona tangu May 2020.Kama ni kweli ni sababu zipi ambazo zimefanya tusitoe takwimu hizo"
  2. Corona ni ugonjwa wa mlipuko lakini mpaka sasa tuna terminology mbili zimezuka,Pneumonia kali na changamoto za upumuaji.Magonjwa haya mawili yana uhusiano wowote na corona?
  3. Tuchukulie kwa mfano wewe kama Prof unaita waandishi wa habari na unasema haya yafuatayo,je utapata hasara gani?Maneno yenyewe ni haya,"Tanzania hatuna corona lakini corona ipo nchi jirani.Kwa kuwa tuna muingiliano na mataifa haya naagiza yafuatayo,abiria ndani ya vyombo vya usafiri vya watu wengi wavae barakoa,kila nyumba iwe na maji tiririka na sabuni....................."
'MIGNON', huwa nakusoma, lakini sijawahi kukusoma hivi! GT.
 
Prof.
Heshima kuu kwako!! Nina maswali machache ambayo naomba kama una wasaa utusaidie na ikiwezekana nawe unisikilize labda naweza kukufaa kwa leo.

Kwanza binafsi na kwa uelewa wangu na elimu kidogo niliyo nayo kuliza swali kuwa corona ipo au haipo kwa Tanzania ni kama kuuliza "mama mkwe kavaa nguo ya ndani ya rangi gani",hivyo sitauliza swali hilo.
  1. WHO wasema kuwa hamjatoa takwimu za corona tangu May 2020.Kama ni kweli ni sababu zipi ambazo zimefanya tusitoe takwimu hizo"
  2. Corona ni ugonjwa wa mlipuko lakini mpaka sasa tuna terminology mbili zimezuka,Pneumonia kali na changamoto za upumuaji.Magonjwa haya mawili yana uhusiano wowote na corona?
  3. Tuchukulie kwa mfano wewe kama Prof unaita waandishi wa habari na unasema haya yafuatayo,je utapata hasara gani?Maneno yenyewe ni haya,"Tanzania hatuna corona lakini corona ipo nchi jirani.Kwa kuwa tuna muingiliano na mataifa haya naagiza yafuatayo,abiria ndani ya vyombo vya usafiri vya watu wengi wavae barakoa,kila nyumba iwe na maji tiririka na sabuni....................."
Profesa hana muda wa kujibu maswali kama haya
 
Back
Top Bottom