Prof. Mbele amtolea Uvivu Mwigulu Nchemba

Prof. Mbele amtolea Uvivu Mwigulu Nchemba

Huwa nikimwona anaongea au kwa bahati mbaya kusoma alichosema Mwigulu- Namlinganisha na mtoto wa darasa la saba aliyefeli. Sidhani kama ni arrogance- ila ni uwezo wake wa kufikiri na kupambanua mambo ndiyo umefikia hapo. Kwa mtizamo wangu- hafai hata kuwa karani wa chama.
 
.....Kama DJ hakufikia hata high school na akafanikiwa kunasa huo mtandao wa MM's, basi ni dhahiri kuwa hizo akili kubwa zina walakini!
 
Weka wazi, mafuriko yaliyotokea wapi? Tangu lini bongo tukatoa misaada ya mafuriko kwenda Illinois au Phillipines? Hiyo ndo kazi inakuweka mjini na kuweza kupiga picha mbele ya Vogue la weñyenazo. Kama hiyo syo kazi yako tuambie sasa kazi yako ni ipi na ofisi ziko wapi?
Yaani mimi nianze kujieleza kwako?

Umewahi kuona daktari anajieleza kwa mgonjwa?
 
KAMA HUU NDo UPROFESA BASI NA WEWE NI PROFESA VYETI TU,HUNA LOLOTE,HAUNA TOFAUTI NA HAO WENYE PHD FEKI
 
Jibu lake ni JOHN MNYIKA ataonekana ana PhD na Mwigulu kaishia dara la mazoezi Ngumbalu.

Profesa kasema kweli. Hivi ukimchukua Mwigulu mwenye Masters first class ukamuweka na JJ Mnyika form 6 halafu ukawaambia watu waangalie jinsi wanavyojenga hoja zao mbalimbali au jinsi wanavyo behave nani ataonekana msomi zaidi?
 
Yaani mimi nianze kujieleza kwako?

Umewahi kuona daktari anajieleza kwa mgonjwa?
Jamani huyu jamaa ni Mnyalu. Hachelewi kujinyonga? Tuachane nae manake anatuharibia topic yetu. anajaribu kupindisha habari kuu
 
Jamaa siasa naona haziwezi, propaganda ndo kabisaa anapaisha mipira na kipa hapati taabu hata ya kuruka
 
Mwigulu ni mchumi daraja la I sio kwamba alipata first class hili lifahamike hivyo. Hajafikia level ya Senior Economist kuelekea Principal Economist hadi Chief Economist (Kama kina Prof. LIPUMBA). So anawachanganya watu wafikiri alipata first class. Katika level ya wachuni huyu ni mtu mdogo sana hawezi pewa kazi ya kuandika mradi ama kusimamia kwenye mashirika ya kimataifa coz hajafikia level zinazotakiwa .
WELL SAID Mwakalinga
 
Prof.Umenena,
wako watako kubeza usijali, ndio wanaishi kwa kazi hiyo.Ila Watanzania wengi wenye hitaji la mabadiliko bado hawaja yumba na wanaendelea kuimarika kidemokrasia,maana hakuna aliye juu ya sheria.CCM gamba limekwamia kiunoni,inawauma wakiona CDM wanajivua kiulaini bila shari.
Ninge washauri nao waige mfano huu wa CDM.Magamba mengi yamen`gang`ania,na wengine wameanza kuwania mbio za Urais bila hata aibu.2015 watafahamu ukweli wa watanzania
 
Kuna mipango ya CCM haijaka.ilika ndani ya CDM. So kuwaondoa hawa kumemchanganya mwigulu, kijana wa fitina. Mwigulu anafikiri wote tumesahau alivyomtungia kitila kesi. Leo hii uchungu anautoa wapi?
 
Hii imetokea baada ya Mwigulu kuanza kupinga mabadiliko yaliyofanywa na CDM kwenye blog yake akisema" KUVULIWA VYEO ZITTO NI AKILI NDOGO INATAWALA AKILI KUBWA
Soma aliyoandika Mwigulu ambacho kinaonyesha kumkere sana Prof.
MWIGULU NCHEMBA BLOG: KUVULIWA VYEO ZITTO KABWE"NDANI YA CHADEMA AKILI NDOGO INATWALA AKILI KUBWA"


Joseph MbeleMwigulu NchembaKwanza kabisa, zingatia kuwa maamuzi hayo yamefanywa kidemokrasia. Hakuna mtu katika chama makini ambaye yupo juu ya utaratibu huu

Chama kina wanachama maelfu, hao ndio CHADEMA; sio mtu fulani au mtu fulani. Ungekuwa na akili kubwa ungetambua hilo.

Yawezekana umesoma shule, lakini hujaelimika. Uwezo wako wa kuchambua mambo ni mdogo. Unadhani kuwa na vyet na digirii ndio sifa sana.

Ngoja nikueleze. Mimi ninayeandika hapa ni profesa Mtanzania hapa Marekani. Nilihitimu B.A (First Class, UDSM, 1973), M.A. 1978, UDSM) nikiwa nimepata "A" katika masomo yote, Nikahitimu M.A. (1982) na PhD (1986) katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, Marekani, tena niliibuka na tuzo ya mwanafunzi bora.

Nasikitika kueleza yote haya, na sijawahi, isipokuwa kwa sababaau ya maringo unayoleta hapa, kuwadharau watu waliomaliza high school, imebidi nikupe vidonge.

Pamoja na shahada zangu zote, nawaheshimu watu wote, wakiwemo wazee kule kijini, ambao walinilea na wanaendelea kunilea kwa busara zao. Mtu aliyemaliza hiyo high school anaweza akawa kiongozi mzuri na mwenye busara kuliko yule mwenya Masters au PhD.

Kama kweli unaheshimu shahada za vyuoni anza utafiti huko huko CCM uone wenzako ambao wanaringia shahada ambazo zina utata. Kwa mfano Mary Nagu hakusoma chuo na kupata shahada yake katika chuo kinachotambuliwa na taasisi yoyote ya kitaaluma inayotathmini na kuidhinishaa shughuli za vyuo. Hapa Marekani tunaita "accreditation agencies."

Anza kwanza kuisafisha CCM, ambayo ina watu wanaodai wana PhD kumbe hazijatoka kwenye vyuo vyenye sifa.

Unacholeta hapa ni kile kinachoitwa "intellectual arrogance," ambayo kwa mtazamo wangu ni dalili ya kutoelimika.

Mtu aliyeelimika anapaswa kufahamu kuwa elimu haiko vitabuni au shuleni tu. Inapatikana pia kwa wazee vijijini.

Halafu nashangaa mambo ya CHADEMA yanakuhusu nini. Mimi sio mwachama wa chama chochote cha siasa, ila nimeona nirekebishe dosari katika kauli yako.

Kwa kumuongezea Profesa Mbele na wanajamii wajue wana CCM wenye elimu za walakini

1. Emmanuel Nchimbi na Phd feki toka chuo sio accredited
2. Milton Mahanga mbunge wa kulazimisha wa Ukonga phd feki haiko accredited
3. Mary Nagu phd feki
4. Richard Ndassa mbunge wa Sumve vyeti feki
5. Phillipo Mulugo Naibu Waziri wa Elimu vyeti feki
6. William Lukuvi waziri vyeti feki
7. Steven Wassira masters ya kufanyiwa Marekani alitoa pesa afanyiwe home work na paper
apunguze majigambo tuna data zake
8. Anthony Diallo mwenyekiti wa CCM Mwanza na mbunge wa zamani vyeti feki
9. Sophia Simba masters ya kufanyiwa ndio maana uwezo mdogo
MWENYE MAJINA MENGINE ONGEZA ORODHA

Ndio maana viongozi wa CCM uwezo mdogo maana wengi ni vyeti feki hata walio na vyeti walipata darasani elimu zao hazireflects uwezo wao utafikiria walikomea darasa la saba wakapewa wadhifa mkubwa kuliko elimu zao mfano
Mwigulu Mchemba, William Ngeleja, Celina Kombani, Magessa Mulongo mkuu wa mkoa wa Arusha na wengine wengi
 
Haya ndiyo wanayoyataka viongozi wetu...Kuwakera watu hadi kuwafanya bubu waongee....

Bahati mbaya viongozi wetu wengi ni sikio la kufa....Mwigulu ni kielelezo tu cha jinsi walivyo!
 
Ni ushabiki tu hana lolote, akiambiwa aeleze anafanya nn kuimarisha upinzani na mfumo wa vyama vingi, utaona kuwa ni mmoja anayefurahi akiona vyama vya upinzani vinasamabaratika. Kuna wakati nilisema chama changu mpaka sasa hakielewi maana ya mfumo wa vyama vingi na hatupotayari kuelewa, hujuma dhidi ya vyama vya upinzani ni tofauti na kushindanisha sera, nashukuru kwasasa Katibiu Mkuu na Mwenezi wameamua kuonyesha kwa vitendo jambo hili badala ya kukaa tu na kupiga porojo. Mapinduzi ya kifikra yanahitajika kujiingiza katika mfumo wa vyama vingi na kuelewa kitu gani kifanyike kukuza demokrasia ya vyama vingi.

Wana CCM wengi bado hawajaelewa faida ya vyama vingi hata kwa chama chao. Bila vyama vingi viongozi wasiopenda demokrasia watawatesa sana members wao wanaoamini katika excellence na siyo technical know who!

Vyama vingi ni faida kwa kila raia ya watanzania aliye chamani ama asiyepo chamani. Bila uthabiti wa vyama vingi demokrasia itakuwa ndoto ya mchana!

Hivi sasa hatuwezi kuiita hii ni demokrasia maana CCM wameamua kwa makusudi kutumia dola kulazimisha matakwa ya kundi dogo badala ya kuachilia matakwa ya watanzania kujiamulia wanachotaka ndiyo maana kuna kuiba kura, kupiga watu mabomu kurubuni vijana katika vyama vya upinzani etc... Kama ni demokrasia wote ambao wangeonekana kusababisha vurugu katika vyama wangeshugulikiwa na dola maana ni makubaliano ya kila mtanzania kuingia katika vyama vingi hivyo kuhujumu vyama ni kuenda kinyume na matakwa ya watanzania.
 
Back
Top Bottom