Prof. Mbele amtolea Uvivu Mwigulu Nchemba

Prof. Mbele amtolea Uvivu Mwigulu Nchemba

Kwani Dj alifika hata hiyo high school?
Mkuu, hivi kuwa DJ kwenye club unayoimiliki na kuwa mbeba mabox ambayo yana mali usiyoimiliki, ipi kazi yenye heshima? Hapa chini ni picha yako halisi ukiwa unabeba mabox

attachment.php
avatar100127_10.gif
 
Akili yake ndogo. Anadhani kuwa na vyeti ndio uwezo. Yeye mwenyewe anaringia eti mchumi daraja la kwanza lakini ni hasara tupu. Labda atwambie yele kiongozi mwenye shahada ya uchumi alipoulizwa kwanini Tanzania ni masikini akaruka mita mia moja kuwa naye hajui na anashangaa tumeweke katika kundi la akili gani pamoja na shahada yake? Nasikia siku hizi anaitwa Dr. lakini ni bonge la kilaza!
 
kwa ccm kuelimika maana yake ni kuwa na makarasi yanayoitwa vyeti, hata kama umeyanunua, hata kama hukusoma, hata kama watu walikufanyia mitihani na thesis, so long as una mavyeti basi wewe ni msomi. haijalisha delivery yako na kilichopo kichwani. ndo maana tunaona phd holder anaanzisha division ziro na 5. ni elimu za vyeti hizo.
 
Kelele tu wote hao!!!!!

Angetuwekea machapisho ya njia za kuinua vijana wa Kitanzania kutokana na shughuli za kiuchumi za hapa!!!!!!

Prof ana machapisho mengi sana, hujaamua kumfatilia tu
 
Hii imetokea baada ya
Mwigulu kuanza kupinga mabadiliko yaliyofanywa na CDM kwenye blog yake
akisema" KUVULIWA VYEO ZITTO NI AKILI NDOGO INATAWALA AKILI KUBWA
Soma aliyoandika Mwigulu ambacho kinaonyesha kumkere sana Prof.
MWIGULU
NCHEMBA BLOG: KUVULIWA VYEO ZITTO KABWE"NDANI YA CHADEMA AKILI NDOGO
INATWALA AKILI KUBWA"



Joseph
Mbele
Mwigulu NchembaKwanza
kabisa, zingatia kuwa maamuzi hayo yamefanywa kidemokrasia. Hakuna mtu
katika chama makini ambaye yupo juu ya utaratibu huu

Chama kina wanachama maelfu, hao ndio CHADEMA; sio mtu fulani au mtu
fulani. Ungekuwa na akili kubwa ungetambua hilo.

Yawezekana umesoma shule, lakini hujaelimika. Uwezo wako wa kuchambua
mambo ni mdogo. Unadhani kuwa na vyet na digirii ndio sifa sana.

Ngoja nikueleze. Mimi ninayeandika hapa ni profesa Mtanzania hapa
Marekani. Nilihitimu B.A (First Class, UDSM, 1973), M.A. 1978, UDSM)
nikiwa nimepata "A" katika masomo yote, Nikahitimu M.A. (1982) na PhD
(1986) katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, Marekani, tena niliibuka
na tuzo ya mwanafunzi bora.

Nasikitika kueleza yote haya, na sijawahi, isipokuwa kwa sababaau ya
maringo unayoleta hapa, kuwadharau watu waliomaliza high school, imebidi
nikupe vidonge.

Pamoja na shahada zangu zote, nawaheshimu watu wote, wakiwemo wazee kule
kijini, ambao walinilea na wanaendelea kunilea kwa busara zao. Mtu
aliyemaliza hiyo high school anaweza akawa kiongozi mzuri na mwenye
busara kuliko yule mwenya Masters au PhD.

Kama kweli unaheshimu shahada za vyuoni anza utafiti huko huko CCM uone
wenzako ambao wanaringia shahada ambazo zina utata. Kwa mfano Mary Nagu
hakusoma chuo na kupata shahada yake katika chuo kinachotambuliwa na
taasisi yoyote ya kitaaluma inayotathmini na kuidhinishaa shughuli za
vyuo. Hapa Marekani tunaita "accreditation agencies."

Anza kwanza kuisafisha CCM, ambayo ina watu wanaodai wana PhD kumbe
hazijatoka kwenye vyuo vyenye sifa.

Unacholeta hapa ni kile kinachoitwa "intellectual arrogance," ambayo kwa
mtazamo wangu ni dalili ya kutoelimika.

Mtu aliyeelimika anapaswa kufahamu kuwa elimu haiko vitabuni au shuleni
tu. Inapatikana pia kwa wazee vijijini.

Halafu nashangaa mambo ya CHADEMA yanakuhusu nini. Mimi sio mwachama wa
chama chochote cha siasa, ila nimeona nirekebishe dosari katika kauli
yako.

Hon.Dr.Marry Nagu Teh teh teh teh teh teh teh
 
Prof ana machapisho mengi sana, hujaamua kumfatilia tu

Hao wamezoea kusoma magazeti ya global publishers. Machapisho ya kitaalamu wana muda gani wa kuyatafuta wakati wameharibiwa akili na umbea wa shigongo.
 
Tulikwisha waambia kuwa hilo jamaa nchemba ni kubwa jinga.
Mnachosha vichwa kujadili hili puuuzi.
 
mtu mwenyewe anaitwa mbele halafu ashindane na mwigulu kwa kipi huyo ni miongoni mwa maprofesa wachovu ambao hawajitambui.

nahisi ww ni nyumbandogo ya punguani huyo!
 
Kama kweli CCM wanawaona zito na kitila ni wazuri kihivyo kwan nini wameumia kufukuzwa kwao chadema, kwa nini wasifurahie kufukuzwa kwao chadema ili wawachukue huko ccm? CCM wanafikiri hizi ni enzi za NCCR kuwa wanaweza kuivuruga chadema kwa propaganda za kitoto. Chadema inajitayarisha kuchukua nchi, watendaji wote wa CCM waliopo chadema lazima wang'olewe kabla ya 2014.

support!
 
hapo anachokifanya Mwigulu, ukiunganisha na yale mawasiliano kwente email, unaona Mwigulu hawaokoi hao kundi la M, bali anaonyesha dhahili kuwa badala ya Zito na Kitila kuchanganyikiwa , ccm ndo wamechanganyikiwa kabisaaaa! mwaka huu tutaona mengi sana.
 
Hawa CCM wameshikwa pabaya. inabidi wajipange upya na mbinu mpya kwa ajili ya uchaguzi.... walidhan kazi kwisho 2015 Chadema kitakuwa kimesambaratika na mbinu zote watakuwa wanapewa na hawa wasaliti
 
Prof wa nini na unafanya nini huko na je umeifanyia nini nchi yako acha hizo mbeba mabox tu wewe. Tuna ma-profesor wengi hawana hata thamani wanashinda jf ili waonekane wana fikra kumbe fikra zenyewe ni kuwazungumziawatu, ongea issues Prof fake
 
ccm wako tayari kutumia kitu chochote kwa namna yoyote mahali popote as long as it will make their enemies unhappy bila kujali busara, hekima wala sheria za nchi zinasemaje, hata kama wao wenyewe ndo wenye tatizo watali kana.

The funny thing is that, these guys are doing it in such an ignorant way. Hivi unawezaje kumlazimisha mtu kwamba paka ni chui, eti kwa sababu unarudiarudia kusema paka ni chui basi you expect watu wengine wakukubalie tu!!

Majanga!!!!
 
ukirusha jiwe kwenye giza ukasikia mayowe ujue limenasa mipango yao na wasaliti wa ndani ya chama imenasa kwa chadema oksjeni ya mtanzania inawauma waliowatuma hawatawaelewa kwani plan imefeli huku imekula muda na fedha na imenasa kirahisi sasa inawauma

chadema yatosha

chadema tumaini jipya

imekula kwao na masalia wao

daah!mkuu umenena kweli.inatosha
 
Hili swali hakuna mwanccm anayeweza kulijibu
Kwanini mnataka Zitto awe mwenyekiti wa cdm na sio awe mwenyekiti wenu wa ccm kwasababu ana akili kubwa kama mnavyotaka kutuaminisha?
DAH! You are a great thinker bro! CCM wamchukue huyo zzk awe m/kiti wao, HUO NI UPUUZI WAO TU.
 
Back
Top Bottom