Prof. Mahalu kutuhumiwa kwa ubaguzi akiwa kwenye taasisi ya kanisa inaleta picha gani kwa mustakabali wa Tanzania?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
876
4,101
Zaman tuliaminishwa kwamba Prof ni mtu msomi na mwenye uwezo mkubwa wa kutambua mema na mabaya.

Leo hii profesa akiwa ndani ya taasisi ya dini ambapo tunaamini analelewa kiroho anapotuhumiwa kuwabagua binadamu na kuelekezwa wasipewe huduma hata ya chakula ni fedhea sana kwa kanisa na wasomi.

Unajiuliza profesa anawezaje akajihusisha na masuala ya kuuza chakula na vinywaji? Cafeteria inawezaje KUWA Sehemu ya profesa kusimamia utoaji huduma?

Mambo mengine jaribuni kuyatafakari na kuona namna ambavyo mtayavumilia hata kama msipoyapenda. Nchi si mali ya watu fulani wala familia fulani kama ambavyo sasa familia chache zenye fedha zimeamua kutuamulia namna ya kuishi .

Mtu wa aina hii taasisi za kidini zinamkumbatia wa kazi gani?
 
Sasa ninyi na bange zenu za kudanganywa na mavuta unga huko klabu hausi mlidhani kanisa kutoa waraka basi mnaweza kulichezea chezea na maujinga yenu? Mlikwenda ukumbi wa kanisa wakawatoa baru Sasa mkaona vyuo vyote Mwanza ni kwenda kuchafua chuo Cha kikatoliki? Hivi ninyi wakatoliki mnawajua?
 
Unajiuliza profesa anawezaje akajihusisha na masuala ya kuuza chakula na vinywaji? Cafeteria inawezaje KUWA Sehemu ya profesa kusimamia utoaji huduma?

Mambo mengine jaribuni kuyatafakari na kuona namna ambavyo mtayavumilia hata kama msipoyapenda. Nchi si mali ya watu fulani wala familia fulani kama ambavyo sasa familia chache zenye fedha zimeamua kutuamulia namna ya kuishi .

Mtu wa aina hii taasisi za kidini zinamkumbatia wa kazi gani?
Ulichokieleza ni wewe pekee unayekijua, sasa unategemeaje wachangiaji washiriki?

Uliyoandika katika hiyo aya ya katikati ni shahidi tosha kwamba wewe ni mtu wa hovyo, bila hata kujua tatizo unaloliwasilisha kuhusu huyo profesa.Naangalia tena jina 'Resillience', nishaona mada nyingi nyingi humu ulizoanzisha lakini sijazisoma.
Kama zote ni za aina hii, basi utakuwa una matatizo kichwani.
 
Back
Top Bottom