Prof Kitila: Magufuli usiteue Wahadhiri

Kwani hivyo vyuo havina SUCCESSION PLAN? Haviandai watu wa kushika nafasi iwapo mmoja akiondoka aliye chini apande? Hivyo vyuo vina tabia ya one man show kwenye vitivo ?

Hiyo ndio tabia ya wasomi wa kitz tumejawa na roho mbaya hawataki wangine waonekane hata kama mtu anaonesha nia na uwezo!..."kweli wanapenda one man show"
U mimi mwingiiiii
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Njaa haina adabu, leo anayakana maneno yake
IMG_wois3s.jpg
 
Lengo la kuanza kwa swali hilo ninataka kujua kama wanataaluma wetu wanamisimamo na vitu wanavyovizungumza. Katika sehemu mbili zilimnukuu Prof. Kitila Mkumbo akisema "Huu utaratibu wa kuwateua wasomi tu ambao ni walimu na wanataaluma kutoka vyuo vikuu hasa Chuo kikuu cha Dar es Salaam si mzuri maana rais haoneshi kuwaandaa wengine kuchukua nafasi zao, tuachwe wasomi tufanye kazi za kitafiti na kitaaluma" hiyo ilikua ni 17/4/2016 chanzo ilikua ni ITV.

Pia Tanzania Daima liliandika hivi:
"Mhadhiri Muandamizi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Kitila Mkumbo amemshauri Mh. Rais Magufuli aache kuteua Wahadhiri katika nafasi za kisiasa ama majukumu mengine kwa kuwa vyuo vikuu vimeanza kukabiliwa na uhaba wa wahadhiri baada ya wengi wao kupewa teuzi mbalimbali.

Aidha Prof. Kitila amesema vyuo vikuu vilivyoathirika zaidi baada ya wengi wa wahadhiri wake kuteuliwa ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Chanzo: Tanzania Daima January 20,2017"


Sasa swali ni je yeye mbona hajakataa hiyo nafasi ya Ukatibu Mkuu?
 
Kuna tofauti gani waliomtangaza lowassa kwenye list of shame kwa miaka 8 mfulilizo na wakaja mkanusha na kumpigia kifua. Au kunya anye kuku akinya bata ttzo??
 
Hii nchi ina wasomi lakini hawana elimu, wanaongea sana wakiwa hawapo kwenye system lakini akikaribishwa anaanza kusifia, mchawi mpe mwanao amlee. Safi Mhe Rais tuone tena kama atakukosoa huyu mbuzi.
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
Hii nchi ni ya ajabu sana wataalamu na wanazuoni wanasema hili lakini wanatenda kinyume chake! Mwakyembe na katiba mpya? Shivji na katiba mpya? Kitila na teuzi za wahadhiri? Lipumba kujiuzulu na kurudi? Slaa kufanya jitahada za kumuingiza lowassa CHADEMA baadae yy kujitoa? Wanatanguliza tumbo kuliko kusimamia wanachoamini!?!
 
Kitila ni Mtumishi wa umma na hii ni post ya ndani ya utumishi wa umma angechukuliwa kwenda kuwa katibu mkuu wa CCM hapo sawa mngekuwa na haki ya kusema
 
Binafsi nimekosa imani na hawa wasomi wetu! wanachosema na kutenda ni vitu viwili tofauti!
Ukisikia wanavyotoa maoni DW unaweza hadaika,ila sasa sidanganyiki tena
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
lengo la kuanza kwa swali hilo ninataka kujua kama maneno ya wanataaluma wetu wanamisimamo na wanavyo vitu wanavyo vi-zungumz. katika sehemu mbili zilimnukuu Prof. Kitila Mkumbo akisema "Huu utaratibu wa kuwateua wasomi tu ambao ni walimu na wanataaluma kutoka vyuo vikuu hasa Chuo kikuu cha Dar es salaam si mzuri maana rais haoneshi kuwaandaa wengine kuchukua nafasi zao, tuachwe wasomi tufanye kazi za kitafiti na kitaaluma" hiyo ilikua ni 17/4/2016 source ilikua ni ITV

Pia Tanzania Daima liliandika hivi:
"Mhadhiri Muandamizi wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Kitila Mkumbo amemshauri Mh Rais Magufuli aache kuteua Wahadhiri katika nafasi za kisiasa ama majukumu mengine kwa kuwa vyuo vikuu vimeanza kukabiliwa na uhaba wa wahadhiri baada ya wengi wao kupewa teuzi mbalimbali.

Aidha Prof Kitila amesema vyuo vikuu vilivyoathirika zaidi baada ya wengi wa wahadhiri wake kuteuliwa ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Chanzo: Tanzania Daima January 20,2017"


sasa swali ni je yeye mbona hajakataa hiyo nafasi ya ukatibu ukuu
Kuna maswali mengine, majibu yote A & B ni sahihi,
Hili swali lako linaangukia kwenye majibu ya aina hiyo
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
Back
Top Bottom