Bwana Yesu asifiwe..Asalaam alyekum wana JF..!
Leo nimeona nikitazame Chama cha Wananchi (CUF)..,ambacho kilikuwa kama nguzo kuu ya Upinzani nchini na Tishio kwa chama Tawala CCM na kuweza kuaminiwa ipo siku itachukua Dola! Lakini hali imekuwa tofauti baada ya kuanza kuibuka migogoro pamoja na kukosa imani mbele ya wananchi na inaonekana dhahiri nafasi yao imechukuliwa na CHADEMA..,huku CUF imeanza kufananishwa na SAU au UPDP..na siku hadi siku chama kimekuwa kikipoteza Mvuto pamoja na Kukikimbiwa na Wanachama wake, Huku kikifananishwa na CCM B...!
Napenda nihoji yuko wapi PROFESA IBRAHIM HARUNA LIPUMBA...? Ambaye ndiye Mwenyekiti wa Chama! kumezuka kila aina ya migogoro,na chama kupoteza mvuto na hata kuchemsha vibaya kwenye chaguzi ndogo kama kule Igunga na Uzini...! Naamini kama Prof.Lipumba angelikuwepo angeweza kutuliza Mgogoro kati ya HAMAD RASHID na SEIF SHARIFF, na pia angekipa chama Nguvu kwenye kampeni ndogo kama kule igunga! na vile vile angekuwa anakiweka chama kwenye mwelekeo...!
Lakini sasa hivi ni dhahiri Pengo lake kubwa linaonekana na sasa hivi Chama kinamuhitaji kwenye muda huu CRITICAL ambako CUF kinaonekana kupoteza mwelekeo huku Majukumu makubwa akiachiwa Julius Mtatiro mtu ambaye experience yake ni Ndogo kisiasa kuweza kufanya maamuzi makubwa na kukiendesha Chama...! na tumekuwa tukishuhudia madudu yake kama kashfa ya magari na kuchemsha Igunga...! na hivi majuzi amedai CUF inajipanga Arumeru..,hii ni dhahiri CUF wanazidi kujipigia msumari kwenye Jeneza kabla ya kuingizwa kaburini...!
Ningependa Nishauri kokote kule Prof.Lipumba achukue maamuzi mawili mazito...,Kurudi na Kukifufua chama ama Kujivua Gamba La Uenyekiti na Kumwachia Mtu ambaye ataweza kukiendesha Chama katika Mstari..! kuliko kuwa kimya nchi za nnje...,Na sijuy siku Chama kitakaposarambatika Sura yake Ataiweka wapi ..?
ndipo anapoanza kupiga porojo uchwara..Prof.Lipumba huwa anakumbuka siasa wakati wa uchaguzi mkuu tu.
Acha udini wewe