Pressure za kuoa na umri

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,753
Wadau kama utamaduni wetu wa Kitanzania nimewekewa pressure ya juu sana ya kuoa!. Umri wa miaka 38 kwenda 39 sasa pressure imekuwa juu sana kama unavyojua utamaduni wetu.

Mimi nilivyokuja US kama vijana wengi ambao tulimaliza shule miaka ya kati ya 1990's tulikuwa hatujui vizuri tunakuja huku kwenye nchi nyingine na mazingira yatakuwaje. Hivyo vijana wengi tumeanza kuwa wenyewe bina watu wazima wa kutuangalia au kutupa mawazo kuanzia miaka 21.

Pamoja na kuwa na uhuru wa hali ya juu hasa hapa USA vilevile tumekuja kwenye utamaduni wa kujitegemea sana. Mapema sana kwenye safari yetu ya maisha ya hapa ilibidi tuchague maisha gani tunataka kuna waliochagua kujirusha, kupiga deals na kujichanganya na wengine tuliamua kujaribu kujisomesha na kutafuta kazi au biashara huko mbele. Kwa tuliochangua kwenda shule na kukimbia matamani ya hapa USA tulijaribu kupunguza au kuacha vitu Fulani vinavyo punguza mwelekeo wa maendeleo.

Pamoja na vitu ambavyo mimi binafsi niliamua kupungua ni wanawake/kukaa nawanawake na kuacha pombe. Hii ni baada ya kuona matatizo vijana wenzangu waliyokuwa wanapata. Nilisema nitaacha vishawishi mpaka nipate green card na kumaliza elimu ya degree.

Mungu akanibariki lakini tatizo ni moja tu elimu ya kujisomesha hapa USA sio rahisi na degree ya kwanza hapa ni ndefu sana hivyo nilisubiri green card yangu kwa miaka mitatu ili niweze kulipia shule kwa bei nafuu kwama wenyeji. Kupiga mahesabu na elimu ya kusua sua nilimaliza chuo nikiwa na miaka 31 kitu ambacho ni cha kawaida kwa watu wa kuja kama mimi. Nilifanikiwa kupata green card, kazi nzuri na kila kitu ambacho nilikuwa nataka.

Tatizo ni kwamba baada ya kuweka ule utaratibu wa kujiheshimu na kupunguza vishawishi sasa umekuwa kama utamaduni siwezi kurudi kama zamani. Pamoja na kwamba hii tabia imenisaida kimaisha kwenye kazi na pesa haijanisaidia kwenye maisha ya familia. Watu naokutana nao kwenye kazi si wabongo na hata si waafrica, sehemu nayoishi haina watanzania wengi au waafrica wengi sio mji lakini sihemu ya makazi/mtaa.

Umri wa kwenda madisko na kujirusha umepita na napenda kukaa nyumbani na kufanya mazoezi. Kwa ufupi maisha yangu naweza kuishi mwenyewe bila wasiwasi. Tatizo lingine ni kwamba unavyozidi kuwa mtu mzima vitu viwili vinajitokeza kuhusu mahusiano (1) Unakutana na wanawake wengi wenye matatizo sana kwenye background zao (2) Unakuwa na akili sana ya kiutu uzima na unajua weakness haraka sana za watu. Kuwa smart sana kwenye mapenzi wakati mwingine sio nzuri. Napenda kuwa na familia lakini sitaki kuwa tu na mtu yeyote kwa sababu ya kuwa na familia.

Sasa na pressure kubwa sana wazazi wangu hatuwezi kuongea kitu kingine ni kuoa tu! Cha ajabu nafanyiwa connection za watu ambao siwajui kabisa na marafiki wengine wananipa namba na picha wa wanawake tofauti ambao sijawahi kuwaona eti niwapigie simu.

Pamoja na nia njema za hawa ndugu na marafiki nafikiri tatizo langu kubwa ni mazingira. Naogopa kuongea hawa madada kwenye simu na wenyewe kufikiria wanaenda kuolea na jamaa marekani wakati hata hatujuani.

Pamoja na kwamba sijauliza waunganishi wengi wamekuwa wakinipa viwango vya elimu vya hao madada na picha za vishawishi na kuonyesha uzuri wao.

Kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu najihisi kama nilifanya makosa kwa kuwa kama nilitokomeza kabisa mahusiano yeyote ambayo yangeweza kunirudisha nyumba kwenye nia yangu ya elimu na kazi pamoja na mafanikio.

Sijajua bado nitafanya nini lakini nitafanya maamuzi yangu mwenyewe kwani mwishoni mimi ndiye nitakuwa na familia na sio mtu mwingine. Naotoa somo tu hasa kwa wale wadogo zangu.
 
Very interesting,hayo hata huku nyumbani yapo,wapo watu wanamaliza shule hata ku-socialize hawajui,kwa sababu maisha yao yalikua ni shule na kulala
 
Mkuu kwanza karibu kwenye chama la masenior bachelors...ni tatizo kweli..japo us kuchelewa kuoa ni kitu cha kawaida sana..sema watu(ndugu) nyumbani wanakuwa hawaelewi...lakini kuongezea uliyoongea pia kwa sisi kudate african american woman ni shida sana kwa sababu ya attitude zao... Unajua jinsi walivyo they are not humble and submissive to men(hata washkaji wao wanakimbilia kwa wazungu)... Kwa hiyo unajikuta unakula tu(maana ni warembo) lakini si kuoa...but inafika point inabidi tu uoe na kuwa na watoto...dah uzi wako umenigusa sana mkuu..karibu kwenye chama..
 
Your Born alone and you can die alone, so the choice is yours!!!. Fanya maamuzi bila kuamuliwa na mtu ili usije ukajutia baadaye, maana unatakiwa uishi kwa furaha na si karaha.
 
Wewe huna tofauti na Dr. Lwaitama yaani yeye kitabu mwanzo mwisho mambo ya nyuchi hana hata kwenda kusali anaona kama anapoteza muda zaidi hata kununua gari anajionea shida imefika wakati anahoji kwa nini watu tunavaa nguo na wakati mababu zetu walikuwa wanatembea uchi. Huko Marekani kwa jinsi ulivyo eleza stori yako nina wasi wasi utakuja kuolewa na wanaume wenzio maana ndo zenu
 
Wewe huna tofauti na Dr. Lwaitama yaani yeye kitabu mwanzo mwisho mambo ya nyuchi hana hata kwenda kusali anaona kama anapoteza muda zaidi hata kununua gari anajionea shida imefika wakati anahoji kwa nini watu tunavaa nguo na wakati mababu zetu walikuwa wanatembea uchi. Huko Marekani kwa jinsi ulivyo eleza stori yako nina wasi wasi utakuja kuolewa na wanaume wenzio maana ndo zenu

Critical Thinking and Argumentation~PL 111
 
Wadau kama utamaduni wetu wa Kitanzania nimewekewa pressure ya juu sana ya kuoa!. Umri wa miaka 38 kwenda 39 sasa pressure imekuwa juu sana kama unavyojua utamaduni wetu. Mimi nilivyokuja US kama vijana wengi ambao tulimaliza shule miaka ya kati ya 1990's tulikuwa hatujui vizuri tunakuja huku kwenye nchi nyingine na mazingira yatakuwaje. Hivyo vijana wengi tumeanza kuwa wenyewe bina watu wazima wa kutuangalia au kutupa mawazo kuanzia miaka 21!. Pamoja na kuwa na uhuru wa hali ya juu hasa hapa USA vilevile tumekuja kwenye utamaduni wa kujitegemea sana. Mapema sana kwenye safari yetu ya maisha ya hapa ilibidi tuchague maisha gani tunataka kuna waliochagua kujirusha, kupiga deals na kujichanganya na wengine tuliamua kujaribu kujisomesha na kutafuta kazi au biashara huko mbele.

This is deep and very relatable. Mimi nilienda kupiga boksi nikiwa bado teenager. Kwa hiyo kimsingi nimeanza kuishi peke yangu mbali na wazazi wangu nikiwa na umri mdogo sana.

Kwa watu ambao hawanijui, wanaweza kudhani labda nimekulia kwenye mazingira fulani ya kudekezwa hivi. La hasha! Maisha ya Marekani kama huna skills za maisha ni magumu sana hususan ukiwa bado mdogo.

Nisingekuwa na nidhamu, hekima, busara, na common sense basi leo hii ningekuwa nimeshafulia kabisa na huenda hata ningekuwa jela au marehemu.

Lakini nashukuru kubahatika kurithi sifa bainishi ya common sense kutoka kwa mmoja wa wazazi wangu (nadhani kama siyo mama mzazi basi atakuwa babu mzaa mama).

Peer pressure ni kitu kibaya sana. Nimeona jamaa wengi sana waliokuwa wanabeba boksi waliopotoshwa na hizo pressure na sasa maisha yao hayana mbele wala nyuma.

Tatizo lingine ni kwamba unavyozidi kuwa mtu mzima vitu viwili vinajitokeza kuhusu mahusiano (1) Unakutana na wanawake wengi wenye matatizo sana kwenye background zao (2) Unakuwa na akili sana ya kiutu uzima na unajua weakness haraka sana za watu. Kuwa smart sana kwenye mapenzi wakati mwingine sio nzuri. Napenda kuwa na familia lakini sitaki kuwa tu na mtu yeyote kwa sababu ya kuwa na familia.

Hii observation nayo iko on point sana hususan hiyo namba mbili. Kwa watu analytical na observant kama mimi, hii sifa ni baraka na laana.

Binafsi huwa nachanganua hadi cadence ya mtu. Na kwenye observation huwa naenda mbali mno hadi najistukia mwenyewe.

Hivi kwa mfano tu, ni nani humu huwa anajaribu kuangalia kama mwanamke ana nose hair zilizochomoza? Na kama anazo kwangu ni kama deal breaker flani hivi.

Kwa hiyo nakuelewa kabisa unaposema wakati mwingine ukitumia akili (na ukiwa na akili sana) kwenye mapenzi si vizuri kabisa. Kila utayekutana naye utamwona ana kasoro tu na labda hakidhi vigezo vyako na blahze blahze kama hizo.
 
Hilo la kuchagua sana mwenza ni jema. Tumia akili zako zote upate wa vigezo utakavyo. Afterall, ndoa ni nkataba. Huna haja kuingia ubia na ambae hujamchuja vema.
 
Ndg kisa chako kimenvutia,umejaribu ku-analyze u,re truth,a thing whch is right bt umri uliofkia huna reason ya kukwpa kuoa,huku nyumban kna wadada 35+,hawajafanikiwa kuolewa,this age iz right 2u coz wanajitambua,na anaweza kukushape in to a socialization.
 
Wewe huna tofauti na Dr. Lwaitama yaani yeye kitabu mwanzo mwisho mambo ya nyuchi hana hata kwenda kusali anaona kama anapoteza muda zaidi hata kununua gari anajionea shida imefika wakati anahoji kwa nini watu tunavaa nguo na wakati mababu zetu walikuwa wanatembea uchi. Huko Marekani kwa jinsi ulivyo eleza stori yako nina wasi wasi utakuja kuolewa na wanaume wenzio maana ndo zenu

Jina lako ni Educator mbona hau toi education sasa hayo matusi yanasaidia vipi vijana hapa, kukuza upeo wa watu na jamii yetu. Tumekuwa tulilalamikiwa watu wa diaspora kutukana lakini sisi ndiyo tunatukanwa kila siku bila sababu au ukweli. Hii sio fantacy ya vitabu na kujilinganisha na watu hii ni issue ya mtu mmoja tu na wengine walio kwenye issue kama yangu. Kama una utoto na huelewi unaweza kwenda kwenye topic ya mtu mwingine matusi hayasaidii jamii yetu. Matusi kwa mtu ambaye hata humjui ni inaonyesha weakness na utoto na sio Strength
 
Wadada wenye Staha au wadada Leftover???
Ndg kisa chako kimenvutia,umejaribu ku-analyze u,re truth,a thing whch is right bt umri uliofkia huna reason ya kukwpa kuoa,huku nyumban kna wadada 35+,hawajafanikiwa kuolewa,this age iz right 2u coz wanajitambua,na anaweza kukushape in to a socialization.
 
Back
Top Bottom