Pressure za kuoa na umri

Pressure za kuoa na umri

This is deep and very relatable. Mimi nilienda kupiga boksi nikiwa bado teenager. Kwa hiyo kimsingi nimeanza kuishi peke yangu mbali na wazazi wangu nikiwa na umri mdogo sana.

Kwa watu ambao hawanijui, wanaweza kudhani labda nimekulia kwenye mazingira fulani ya kudekezwa hivi. La hasha! Maisha ya Marekani kama huna skills za maisha ni magumu sana hususan ukiwa bado mdogo.



Nisingekuwa na nidhamu, hekima, busara, na common sense basi leo hii ningekuwa nimeshafulia kabisa na huenda hata ningekuwa jela au marehemu.

Lakini nashukuru kubahatika kurithi sifa bainishi ya common sense kutoka kwa mmoja wa wazazi wangu (nadhani kama siyo mama mzazi basi atakuwa babu mzaa mama).

Peer pressure ni kitu kibaya sana. Nimeona jamaa wengi sana waliokuwa wanabeba boksi waliopotoshwa na hizo pressure na sasa maisha yao hayana mbele wala nyuma.



Hii observation nayo iko on point sana hususan hiyo namba mbili. Kwa watu analytical na observant kama mimi, hii sifa ni baraka na laana.

Binafsi huwa nachanganua hadi cadence ya mtu. Na kwenye observation huwa naenda mbali mno hadi najistukia mwenyewe.

Hivi kwa mfano tu, ni nani humu huwa anajaribu kuangalia kama mwanamke ana nose hair zilizochomoza? Na kama anazo kwangu ni kama deal breaker flani hivi.

Kwa hiyo nakuelewa kabisa unaposema wakati mwingine ukitumia akili (na ukiwa na akili sana) kwenye mapenzi si vizuri kabisa. Kila utayekutana naye utamwona ana kasoro tu na labda hakidhi vigezo vyako na blahze blahze kama hizo.

Kuna jamaa zangu wengi wanaishi Boston, sijui ndio nyie!
 
Usivute mke toka Tz ...utajutra...labda utafute waliokuja US kusoma...jichanganye utapata mke...lakini usitumie mtu nauli...narudia utajutra na hao ma opportunist....
Mama nyumba kubwa heshima kwako..na hii ndo dilema tunayopata maana..kusema ukweli african american woman hawaoleki-wachache sana wenye attitude nzuri..na kuvuta mtu kutoka bongo huwezijua anaweza kuja kukujimbia tumeona haya(hasa wale mademu mawenge wenge na walimbukeni).. Ni kazi sana..na usr bachelor ndo unazidi kukolea..dah
 
it seems wewe ni domo zege maana kwa maelezo yako unasuuzia ulikuwa unatafuta maisha as if ulihama dunia kwenda sayari ya MARS kutoishi na watu usiowajua si sababu ya kutokuwa na mtu kwa umri wako.. huwa huna socialization activities hapi ulipo kwenye nyumba za ibada, kutembelea marafiki etc. BADILIKA kiongozi maisha si kazi/pesa tu
 
Kuwa na staha basi mwenzako yuko real na anaomba ushauri,...You to accept other people attitude and behavior.....
 
Nakupongeza sana kwa maamuzi thabiti uliyoyaganya. Kila uamuzi unaochukua siku zote una faida na hasara zake. Sioni kama una kitu cha kujilaumu. Ulikuwa uamuzi sahihi kwa nchi kubwa kama Marekani. Nadhani ni muda sasa umtafute mwenzi wako ukizingatia tabia yake zaidi. Kwa kuwa una green card nadhan unaweza kuja Bongo kwq muda kama miezi 3 hivi ukimshirikisha MUNGU utampata mke kipenzi cha moyo wako. Amini ktk Yeye akutiaye nguvu. Amina.
 
Kuchelewa kumaliza chuo/elimu ya juu sio tatizo sana coz kwa wengi wetu finances zilikuwa magumashi kwa hiyo ilibidi tuchelewe kidogo. Tatizo kwa mleta mada ni kutojichanganya na wadada hasa alipokuwa late twenties and early thirties. Kujichanganya ni muhimu sana pia huwa akili ya mapenzi ni tofauti na akili ya kawaida. Ukitaka upime vitu in details kwa mdada huwezi kupata mtu wa kuoa...coz hayupo mtu perfect.
 
Kuna movie moja nilikuwa naangalia ...nimecheka mdada baada ya pressure za kuambiwa umri umeenda haolewi...

Amekuja na list ndeefu ya vigezo viiingi...handsome, urefu, sijui nini...alichoniacha hoi ni kumalizia na 'asiwe na mama'

Mwenzake anamshangaa ...how...amejizaa mwenyewe? eti anajibu ... si amekufa...
 
Wadau kama utamaduni wetu
wa Kitanzania nimewekewa pressure ya juu sana ya kuoa!. Umri wa miaka 38
kwenda 39 sasa pressure imekuwa juu sana kama unavyojua utamaduni wetu.
Mimi nilivyokuja US kama vijana wengi ambao tulimaliza shule miaka ya
kati ya 1990’s tulikuwa hatujui vizuri tunakuja huku kwenye nchi
nyingine na mazingira yatakuwaje. Hivyo vijana wengi tumeanza kuwa
wenyewe bina watu wazima wa kutuangalia au kutupa mawazo kuanzia miaka
21!. Pamoja na kuwa na uhuru wa hali ya juu hasa hapa USA vilevile
tumekuja kwenye utamaduni wa kujitegemea sana. Mapema sana kwenye safari
yetu ya maisha ya hapa ilibidi tuchague maisha gani tunataka kuna
waliochagua kujirusha, kupiga deals na kujichanganya na wengine tuliamua
kujaribu kujisomesha na kutafuta kazi au biashara huko mbele. Kwa
tuliochangua kwenda shule na kukimbia matamani ya hapa USA tulijaribu
kupunguza au kuacha vitu Fulani vinavyo punguza mwelekeo wa maendeleo.
Pamoja na vitu ambavyo mimi binafsi niliamua kupungua ni wanawake/kukaa
nawanawake na kuacha pombe. Hii ni baada ya kuona matatizo vijana
wenzangu waliyokuwa wanapata. Nilisema nitaacha vishawishi mpaka nipate
green card na kumaliza elimu ya degree. Mungu akanibariki lakini tatizo
ni moja tu elimu ya kujisomesha hapa USA sio rahisi na degree ya kwanza
hapa ni ndefu sana hivyo nilisubiri green card yangu kwa miaka mitatu
ili niweze kulipia shule kwa bei nafuu kwama wenyeji. Kupiga mahesabu na
elimu ya kusua sua nilimaliza chuo nikiwa na miaka 31 kitu ambacho ni
cha kawaida kwa watu wa kuja kama mimi. Nilifanikiwa kupata green card,
kazi nzuri na kila kitu ambacho nilikuwa nataka. Tatizo ni kwamba baada
ya kuweka ule utaratibu wa kujiheshimu na kupunguza vishawishi sasa
umekuwa kama utamaduni siwezi kurudi kama zamani. Pamoja na kwamba hii
tabia imenisaida kimaisha kwenye kazi na pesa haijanisaidia kwenye
maisha ya familia. Watu naokutana nao kwenye kazi si wabongo na hata si
waafrica, sehemu nayoishi haina watanzania wengi au waafrica wengi sio
mji lakini sihemu ya makazi/mtaa. Umri wa kwenda madisko na kujirusha
umepita na napenda kukaa nyumbani na kufanya mazoezi. Kwa ufupi maisha
yangu naweza kuishi mwenyewe bila wasiwasi. Tatizo lingine ni kwamba
unavyozidi kuwa mtu mzima vitu viwili vinajitokeza kuhusu mahusiano (1)
Unakutana na wanawake wengi wenye matatizo sana kwenye background zao
(2) Unakuwa na akili sana ya kiutu uzima na unajua weakness haraka sana
za watu. Kuwa smart sana kwenye mapenzi wakati mwingine sio nzuri.
Napenda kuwa na familia lakini sitaki kuwa tu na mtu yeyote kwa sababu
ya kuwa na familia.

Sasa na pressure kubwa sana wazazi wangu hatuwezi kuongea kitu kingine
ni kuoa tu! Cha ajabu nafanyiwa connection za watu ambao siwajui kabisa
na marafiki wengine wananipa namba na picha wa wanawake tofauti ambao
sijawahi kuwaona eti niwapigie simu. Pamoja na nia njema za hawa ndugu
na marafiki nafikiri tatizo langu kubwa ni mazingira. Naogopa kuongea
hawa madada kwenye simu na wenyewe kufikiria wanaenda kuolea na jamaa
marekani wakati hata hatujuani. Pamoja na kwamba sijauliza waunganishi
wengi wamekuwa wakinipa viwango vya elimu vya hao madada na picha za
vishawishi na kuonyesha uzuri wao. Kwa mara ya kwanza kwenye maisha
yangu najihisi kama nilifanya makosa kwa kuwa kama nilitokomeza kabisa
mahusiano yeyote ambayo yangeweza kunirudisha nyumba kwenye nia yangu ya
elimu na kazi pamoja na mafanikio. Sijajua bado nitafanya nini lakini
nitafanya maamuzi yangu mwenyewe kwani mwishoni mimi ndiye nitakuwa na
familia na sio mtu mwingine. Naotoa somo tu hasa kwa wale wadogo
zangu

eti wanakuchaguli kwan wew huna macho? fanya roho yako inapenda usiwasikilize ndugu tho mueleweshe mama yako ndo mtu muhimu. pole
 
Kuchelewa kumaliza chuo/elimu ya juu sio tatizo sana coz kwa wengi wetu finances zilikuwa magumashi kwa hiyo ilibidi tuchelewe kidogo. Tatizo kwa mleta mada ni kutojichanganya na wadada hasa alipokuwa late twenties and early thirties. Kujichanganya ni muhimu sana pia huwa akili ya mapenzi ni tofauti na akili ya kawaida. Ukitaka upime vitu in details kwa mdada huwezi kupata mtu wa kuoa...coz hayupo mtu perfect.

Umri unapozidi kwenda choice inazidi kupungua ...si kwa wanawake wala wanaume...possibility ya kupata magumashi ni kubwa sana ...kwa sababu huna muda tena wa kuchunguza...mfano wengi tuliolewa na watu ambo hatukuanza kujuana kwa gia ya ndoa...ndoa ilikuwa matokeo ya kiridhika kuwa tunaendana na tunaweza ishi pamoja.. .

Lakini umri ukienda kila relationship inakuwa serious hata kama hai deserve...
kwa kuwa unakimbia na muda...
 
Umri unapozidi kwenda choice inazidi kupungua ...si kwa wanawake wala wanaume...possibility ya kupata magumashi ni kubwa sana ...kwa sababu huna muda tena wa kuchunguza...mfano wengi tuliolewa na watu ambo hatukuanza kujuana kwa gia ya ndoa...ndoa ilikuwa matokeo ya kiridhika kuwa tunaendana na tunaweza ishi pamoja.. .

Lakini umri ukienda kila relationship inakuwa serious hata kama hai deserve...
kwa kuwa unakimbia na muda...

Binafsi siamini katika courtship ya mda mrefu. Nilichelewa kumaliza chuo lakini bado haikuwa sababu ya kuathiri uwezo wangu kimahusiano. Nikikutana na mdada ndani ya mwaka inatodha kufanya maamuzi.

Alichokosea ni kutojichanganya na wanawake kwa hiyo hata approach yake kwao ni tatizo. Na kwa umri huo wa 37-40 ndio atapata shida sana.
 
it seems wewe ni domo zege maana kwa maelezo yako unasuuzia ulikuwa unatafuta maisha as if ulihama dunia kwenda sayari ya MARS kutoishi na watu usiowajua si sababu ya kutokuwa na mtu kwa umri wako.. huwa huna socialization activities hapi ulipo kwenye nyumba za ibada, kutembelea marafiki etc. BADILIKA kiongozi maisha si kazi/pesa tu

Nashukuru kwa mawazo lakini kwenye dongo la domo zito siko hivyo. Mimi sio mtu wa kutokea kila demu lakini nina bahati ya kupendwa na nina mwangalio mzuri hivyo sijawahi kupata shida ya kupata wanawake lakini kama nilivyosema huko nyuma nili avoid kwa muda mrefu kujenga uhusiano wa kudumu. Katika umri huu hakuna cha domo tena hata hivyo ni ule umri wa watu kuangalia una nini!. Ukiwa na kazi ya professional kama yangu na una vibali vimetulia huhitaji kuongea sana lakini unaweza kwa kirahisi kubambikizwa bila mapenzi. Kigumu zaidi ni ukweli kwamba kwa umri huu kila mwanamke anakuja kwa kuolewa tu hivyo inabidi uwe mwangalifu.
Kwa sisi miaka hiyo niliona rafiki zangu wakifungwa, wengine kujiingiza kwenye mambo ya dili na kufungwa, wengine ulevi na hata madawa ya kulevya. Wengi wa marafiki zetu tuliokuja nao miaka hiyo wamerudi au kurudishwa Tanzania bila elimu na wengine bila hata posho kidogo. Hivyo nilivyo acha pombe na kupunguza mambo ya wanawake nilikuwa na nia njema na niliona mengi kwa wakati ule. Kama mnakumbuka mlishasikia Watanzania wanafungwa miaka iliyopita mambo yalikuwa si mazuri kishawishi miaka hasa ya 2000-2005
 
This is some REAL topic. I feel y'all , na kuelewa hasa ni vipi mda unaweza pita kirahisi rahisi. Na because the cause of such situations is multifactorial.

Ila ningependa kuuliza kwa mfano NN, dont you think kuwa kuna some compromise inayotakiwa?
Sidhani kwamba ikija tokea ukawa na mwenza ni kwamba yeye hajaona fault yeyote kwako. Some things can be compromised fellas!
 
Kamundu naona endelea kuwa mvumilivu uoe mtu utakayeridhia wewe..kuwa mwangalifu ya hao unaochaguliwa possibility ni kubwa wakaficha makubwa for the sake ya ndoa kama unavyojua wadada na ndoa tena..mean while don't be desperate otherwise utapata bomu..all the best
 
Last edited by a moderator:
Hivi why do indian arranged marriages have a higher success rate then most other marriages hata kwa walioko western world?
 
Wewe huna tofauti na Dr. Lwaitama yaani yeye kitabu mwanzo mwisho mambo ya nyuchi hana hata kwenda kusali anaona kama anapoteza muda zaidi hata kununua gari anajionea shida imefika wakati anahoji kwa nini watu tunavaa nguo na wakati mababu zetu walikuwa wanatembea uchi. Huko Marekani kwa jinsi ulivyo eleza stori yako nina wasi wasi utakuja kuolewa na wanaume wenzio maana ndo zenu

Nimecheka lol
 
Kuna wazee wana miaka 45 na wanaoa mabinti wadogo!!!!!we jichanganye utapata mke wewe tu ndio unajichelewesha
 
Hivi why do indian arranged marriages have a higher success rate then most other marriages hata kwa walioko western world?

Mambo ya Wahindi si kama tunavyodhani...labda wahindi wa Tz...ila huko kwao ndoa ni majanga tu...hao wanaobaka watoto wadogo na kuwatundika mitini?

Ma feminist huko ndio mwake..nina marafiki zangu 3 wote hawana hata mpango na kitu kinaitwa ndoa...na umri umeshasonga....mmoja anakaribia 50...mwingine ana approach 40...hakuna cha arranged mchumba wala nini...upper class hao...
 
This is deep and very relatable. Mimi nilienda kupiga boksi nikiwa bado teenager. Kwa hiyo kimsingi nimeanza kuishi peke yangu mbali na wazazi wangu nikiwa na umri mdogo sana.

Kwa watu ambao hawanijui, wanaweza kudhani labda nimekulia kwenye mazingira fulani ya kudekezwa hivi. La hasha! Maisha ya Marekani kama huna skills za maisha ni magumu sana hususan ukiwa bado mdogo.

Nisingekuwa na nidhamu, hekima, busara, na common sense basi leo hii ningekuwa nimeshafulia kabisa na huenda hata ningekuwa jela au marehemu.

Lakini nashukuru kubahatika kurithi sifa bainishi ya common sense kutoka kwa mmoja wa wazazi wangu (nadhani kama siyo mama mzazi basi atakuwa babu mzaa mama).

Peer pressure ni kitu kibaya sana. Nimeona jamaa wengi sana waliokuwa wanabeba boksi waliopotoshwa na hizo pressure na sasa maisha yao hayana mbele wala nyuma.



Hii observation nayo iko on point sana hususan hiyo namba mbili. Kwa watu analytical na observant kama mimi, hii sifa ni baraka na laana.

Binafsi huwa nachanganua hadi cadence ya mtu. Na kwenye observation huwa naenda mbali mno hadi najistukia mwenyewe.

Hivi kwa mfano tu, ni nani humu huwa anajaribu kuangalia kama mwanamke ana nose hair zilizochomoza? Na kama anazo kwangu ni kama deal breaker flani hivi.

Kwa hiyo nakuelewa kabisa unaposema wakati mwingine ukitumia akili (na ukiwa na akili sana) kwenye mapenzi si vizuri kabisa. Kila utayekutana naye utamwona ana kasoro tu na labda hakidhi vigezo vyako na blahze blahze kama hizo.

Eti wanasema bata ukimchunguza sana humli,so mi nijichukulie tuuuu kisa baba au mama anaweza kudead bila kumuona mjukuu aaaarghhhhhhhhhh ila kuna uncle wangu mmoja wa kanisani aliniacha hooi one day,kuna cheo kimoja alikuwa ananishauri kugombea pale kanisani kutokana na elimu yangu ila tatizo criteria moja nilikuwa namiss (to have a wife) uncle mi nikamwambia sina mtu kwa sasa akanijibu kwa hiyo unasubiri wakufuate wakwambie uwaoe??:sleepy:
 
Back
Top Bottom