Sikubaliani na mleta post hata kidogo, kwamba kitendo hiki kitaenda kuua creativity and innovation za subordinates wa JPm..
Wewe ulitaka Mtu akionyesha creativity and innovation ktk kudanganya na kukwepa majukumu avumiliwe....!!???
Kwamba viongozi wetu watashindwa kufanya au kutoa maamuzi magumu na muhimu kwa kuogopa kutumbuliwa.....
Naomba nikukumbushe kiongozi mmoja tu aliyefanya maamuzi yenye kuonyesha creativity and innovation na akasapotiwa.
RC MAKONDA, kaagiza wenye silaha wote wahakikiwe, JPM alikuwa wa kwanza kuhakiki silaha yake kutii agizo la RC.Natafsiri kitendo kile kama Ku- promote creativity and innovation. Baadhi walitafsiri kama SHOW OFFS.
Wewe ulitaka avumilie kiongozi Muongo na asiyetimiza wajibu wake, amwite amsihi, ambembeleze, then what!!!???...
Hayo ndiyo aliyofanya Mkwere tukafika haha tulipo fika.
Kitendo hiki kinaujumbe mzito, ujumbe sahihi kama ule aliotuma kipindi alipotoka kukaguliwa Silaha.