Mh. Rais Magufuli, wengi wanakusifia kwa kauli na matendo yako. Pengine wanakuogopa kukushauri moja kwa moja wakihofia kutofautiana na wewe.
Lakini kumbuka akutakiae mazuri atakukosoa daima.
Kuna kauli tata umekuwa ukizitoa ambazo kwa kiongozi hapaswi kuzitoa kwa watu anaowaongoza, sina haja ya kuzirudia, bali unazifahamu mwenyewe.
Tafakari kwa makini na ufahamu kuwa mtumishi ni binadamu, na ubongo wa binadamu huwa na tabia na hulka ya kuganda na kufunga kwa kiingereza wanasema "Freezing and Shutting Down" pale unapokuwa umeelemewa na vitisho vyenye kukatisha tamaa.
Nafahamu, unayo nia njema ya kukomesha Ufisadi, Rushwa na uzembe, na ninakuunga mkono.
Lakini kaa chini utafakari kuwa Uongozi wa nchi ni zaidi ya kutoa Maneno makali mbele ya Luninga na Vyombo vya habari.
Ukiendelea hivyo, wasaidizi wako wote wataamua kutulia, wakikuacha wewe kama main player, wakihofia kutofautiana nawe, watakuwa wanafanya kitu kinaitwa, "go slow" yaani mgomo baridi.
Jifunze kufanya encouragement pia.
Nakushauri kama Mwananchi Mzalendo.