Pres. Magufuli: Don't Put Your Sub-ordinates on Short-Leashes (ala Kilango)

Pres. Magufuli: Don't Put Your Sub-ordinates on Short-Leashes (ala Kilango)

Kuna watu wengi sana wenye utaalamu na wenye weredi wa kufanyanya kaz kwa moyo!asitishike!mbele kwa mbele
 
Serikali ya Magufuli ni ya kwenda mbio speed ya kilomita 1000 kwa saa ukiwa ni GO SLOW au una mgomo baridi jiandae kufunga virago utafute shughuli ingine ya kufanya lakini sio kubaki kuwa mfanyakazi wa serikali.Wako watanzania kibao tena vijana wasomi wa uhakika wenye uwezo wa kuchukua nafasi yako.

Kwa ufupi usijifanye hata uko frustrated na kazi ya serikali ikakufanya ufanye kazi chini ya kiwango kwa ajili ya frustration ni kujipa tiketi ya kuondolewa kazini.Kama unaona ajira ya serikali haikufai kwa vile ulivyozoea jiondoe mwenyewe upesi tena haraka.Magufuli keshasema waliozoea kufanya kazi kwa mazoea kimbunga kitawakuta.
Umeongea vizuri sana kaka
Nahisi amekuelewa
 
Nyie mnaolalamika mmewashwa na vidonda vya majipu mliyotumbuliwa? rudini mkakamuliwe vzr!
 
You will stifle creativity & innovations in governance.

So, probably Hon. Kilango deserved it. However, such summary dismissals will scare your subordinates (ministers and below) to a point of being Zombies instead being your linchpins in perfecting your governance.

Kama kuanzia mawaziri hadi vigogo wilayani watakuwa na mtera wakiogopa kisu chako cha majipu basi utawala utakuwia mgumu sana. Wasaidizi wako wataogopa kutoa maamuzi magumu (na pengine yenye hitlafu hapa na pale - i.e., not to your liking) wakichelea kuumbuliwa na bosi.

Mkuu wa ngazi ya juu akiteleza muite (au waziri wako amuite) chemba na kumpa karipio la kirafiki (faragha) halafu mtie moyo (encourage) aendelee kuthubutu makubwa zaidi.

Hii fukuza-fukuza hii utakuja jikuta uko peke yako kifikra katika awamu hii ya tano. Watanzania wengi wangependa urudi tena 2020 na nina uhakika utarudi lakini tumia diplomasia sasa katika utawala wako.

Kila mtu sasa anajua kasi yako na nidhamu yako. Najua Rais you are not diplomatic in nature but you need diplomacy (in your rule) now more than ever. Unaweza kubaki na kasi hiyohiyo ulionayo bila kudhalilisha wasaidizi wako.

Ushauri kwako kama rafiki.
Kikwete aliwachekea wakamuingia mpk kwenye koti!! awakimbize tu kwa maana hakuna namna
 
Mh. Rais Magufuli, wengi wanakusifia kwa kauli na matendo yako. Pengine wanakuogopa kukushauri moja kwa moja wakihofia kutofautiana na wewe.
Lakini kumbuka akutakiae mazuri atakukosoa daima.

Kuna kauli tata umekuwa ukizitoa ambazo kwa kiongozi hapaswi kuzitoa kwa watu anaowaongoza, sina haja ya kuzirudia, bali unazifahamu mwenyewe.

Tafakari kwa makini na ufahamu kuwa mtumishi ni binadamu, na ubongo wa binadamu huwa na tabia na hulka ya kuganda na kufunga kwa kiingereza wanasema "Freezing and Shutting Down" pale unapokuwa umeelemewa na vitisho vyenye kukatisha tamaa.

Nafahamu, unayo nia njema ya kukomesha Ufisadi, Rushwa na uzembe, na ninakuunga mkono.

Lakini kaa chini utafakari kuwa Uongozi wa nchi ni zaidi ya kutoa Maneno makali mbele ya Luninga na Vyombo vya habari.

Ukiendelea hivyo, wasaidizi wako wote wataamua kutulia, wakikuacha wewe kama main player, wakihofia kutofautiana nawe, watakuwa wanafanya kitu kinaitwa, "go slow" yaani mgomo baridi.

Jifunze kufanya encouragement pia.

Nakushauri kama Mwananchi Mzalendo.
Kwahiyo kwa akili yako ya kwaida ulitaka awe anabembelezabembeleza anapoona kitu ambacho anatakiwa akemee, tena kwa maneno makali? Wewe unataka turudi tulikotoka.Hayo mawazo yako subiri ukiwa Rais ndiyo uyatekeleze sasa mwache JPM afanye kazi.
 
Nashangaa watu hamjuhi kinachoendelea ile kitu ilitegeshwa tu ili waone kagusa ngazi hiyo. Chezea wewe! Hii movie mpaka muisome lazima mpate phd feki!
 
I do bèlieve that there is time for diplomacy, politics, and administration/governance. Let's allow our president do his duties because it's not time for politics nor diplomacy. Mahiga will do diplomacy.
Mmh
 
Sioni kama diplomacy inahitajika kipindi hiki. The President knows what he is doing. Siamini kama kweli wewe uko Tanzania au unategemea media kupata taarifa ya yanayojiri nchini. Hii diplomacy ndiyo imetufikisha hapa tulipo mkuu. Watanzania tumechoka, kuleana huku na kuoneana aibu ndo kumetufikisha hapa. Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na hata Wakuu wa Taasisi za serikali wao waligeuka kuwa wapigaji tu na Miungu watu. Walikuwa wakifanya madudu wanajua hawaguswi. Baadhi ya makatibu wakuu walikuwa wanadiriki kutoa maagizo kwa taasisi zilizo chini ya wizara yao ili budgets zao zipitishwe na Wizara lazima wafanye maarifa ya kumpa kitu kidogo Katibu Mkuu. Makati wakuu wengine wakawa wanakata OC za taasisi zao na pesa hizo wanachukuwa wao.
Ili kukomesha hali kama hiyo Mh.Rais lazima afanye hivyo ili hawa wasaidizi wake wawe na discipline. Mambo ya kubembelezana hayapo kwa kipindi hiki. Mbona Tanzania ina wasomi wengi tu na wazalendo!! siamini kuwa Mh. Rais atakosa watu wa kufanya naye kazi kama akiwatimua hawa waliozoea kufanyakazi kwa mazoea.
Kuchoka kwetu hakuondoi ukweli aliosema jamaa! Watanzania tuna shida moja nayo ni kutokusoma kwa makini! Tu wepesi sana wa kujibu hoja bila kujipa muda wa kutafakari
 
Sijui taratibu za serikari mtu akishateuliwa na raisi anaandaliwa mkataba gani wa kazi huko mbeleni kwenye kulinda haki zake.

Regardless kama tunataka kulipa hili swala zima moral justification moja ya matakwa ya raisi yalikuwa wakuu wa mikoa watufue wafanyakazi hewa na hilo limetamkwa mbele ya dunia; in other words hilo tamko ni kama ni terms za ajira ya kazi (kisheria mkataba unaweza kuwa oral agreement sio lazima maandishi) not that the president needs to prepare any before he hires or fires people. The mere fact his selection is based on presidential long customs since independence no court in the world would rule against unfair dismal even if the interpretation of the law was forced anywhere on 'god's earth' given the facts of the matter.

Kushindwa kubaini wafanyakazi hewa halafu wenzako waje wawakute sehemu ambazo wewe ndio unamlaka that is enough of a breach even if the RC had a contract; those findings alone offers a good reason to justify 'fair dismissal' based on the capacity to perform.

Raisi anahitaji bado kuweka nidhamu na aina ya uongozi wake na moja wapo people need to take accountability kwa nafasi zao. Wewe umepewa task umesema hakuna kitu, yeye katoa maagizo ya uchunguzi independent kakuta wafanyakazi hewa ina mwacha na option ipi tena? yaani kumuacha Ana Kilango ingekuwa ni kama kusema yeye mwenyewe raisi hayuko serious this was a necessary dismissal ili wengine waelewe kama viongozi wana 'strict liability' ni jukumu lao kuhakikisha maagizo yanafanyiwa kazi kitaalamu sio kimazoea.
Wewe nae huna tofauti na mama Kilango! Kwanini usitumie lugha moja ili kujenga hoja yenye mtiririko? Wasomi wa Tanzania makanjanja sana!
 
Hii inaitwa "TONE AT THE TOP" Mkuu anabadilisha tone toka awamu iliyopita na sasa anatengeneza ya kwake. Itabidi subordinates wote wa Mheshimiwa Rais wamwelewe tu ama kwa hiyari au kwa nguvu.
 
You will stifle creativity & innovations in governance.

So, probably Hon. Kilango deserved it. However, such summary dismissals will scare your subordinates (ministers and below) to a point of being Zombies instead being your linchpins in perfecting your governance.

Kama kuanzia mawaziri hadi vigogo wilayani watakuwa na mtera wakiogopa kisu chako cha majipu basi utawala utakuwia mgumu sana. Wasaidizi wako wataogopa kutoa maamuzi magumu (na pengine yenye hitlafu hapa na pale - i.e., not to your liking) wakichelea kuumbuliwa na bosi.

Mkuu wa ngazi ya juu akiteleza muite (au waziri wako amuite) chemba na kumpa karipio la kirafiki (faragha) halafu mtie moyo (encourage) aendelee kuthubutu makubwa zaidi.

Hii fukuza-fukuza hii utakuja jikuta uko peke yako kifikra katika awamu hii ya tano. Watanzania wengi wangependa urudi tena 2020 na nina uhakika utarudi lakini tumia diplomasia sasa katika utawala wako.

Kila mtu sasa anajua kasi yako na nidhamu yako. Najua Rais you are not diplomatic in nature but you need diplomacy (in your rule) now more than ever. Unaweza kubaki na kasi hiyohiyo ulionayo bila kudhalilisha wasaidizi wako.

Ushauri kwako kama rafiki.
Diplomacy, you mean hypocrisy? Massaging the known wrongs! no! No! then NO!
Unamshauri kuwaita faragha, yawezekana kisha waita kwenye faragha je? Hebu tuwe wakweli kwamba ukishafanya uongozi kama urafiki wa kuitana na kupeana maonyo darkroom, ujue hakuna atakaye regret! Hakuna haya ya ku-encourage ubunifu kwa watendaji wa karibu wa rais. Hawa ni watu ambao taratibu zao za kazi zinafahamika, zimepangwa. Ubunifu hauwezi kuendesha serikali, ila taratibu tu.

Take this living example of Hon. Kilango. Tangu siku anateuliwa hilo lilikuwa jukumu lake kati ya matano tu! In less than significant time she concluded! No thinking, no hesitation. What next! Remember we can learn to be wise but difficult to learn how to think. Alikuwa naibu waziri kabla! Waonee huruma wa TZ mambo ya kuteleza, kupitiwa, kujisahau, nk. huku bilions zikiliwa na shamba boys walioko kwenye payrolls hayana maana tena!
 
Inaelekea hata kiSwahili kinakupiga. Huyu "Waziri husika" hasa ni nani unaemzungumzia? Nimeshindwa kukuelewa mkuu ingawaje mimi ni mzaliwa na mkulia uswahilini.

Sasa kumbe unapayuka tu baada ya viroba? Sishangai kabisa sio rahisi kuelewa na ndiyo tatizo lenu kurukia rukia mambo na kujiona eti mna level ya sijui ulaya, Kenya au USA.

Kuna waziri husika alifanya press conference a week or so ago specifically on that matter sababu ipo chini yake. Tena kama umemsikia rais, kasema wazi hata yeye haelewi shetani gani alimkumba huyu...kuwa hata makosa yalipogunduliwa akaelezwa huyu RC alishindwa kuchukua hatua kwa waliomdanganya !! You go against directives, tena za Rais halafu mijitu eti ohh angeitwa na kupewa warning..ohh kujitetea !!

Sijui kama unaelewa " to read between the lines" jaza kama huelewi basi endelea kulalama !!
 
Tanzania imepata rais wa K weli awamu hiii mwenye nia yakuipaisha kiuchumi n.a. kuiheshimisha dhidi ya mabepari, kaza konde magufuri uko sawa
 
Back
Top Bottom