Ndugu yangu una point ya msingi sana, lakini wasio weza toa point wanakimbilia matusi tu. Mimi nampenda sana Magufuli pamoja na kuwa si mwana CCM wala UKAWA, lakini tulipo fika tunahitaji kiongozi kama yeye. Hata hivyo najiuliza maswali, ni kweli kosa kama la Mama Kilango lazima afukuzwe kazi outright namna hii? Pamoja na kweli kukosea kwake kumelitia taifa hasara ya hiyo mishahara.
Msingi wa swali langu ni hili. 1 Kila mwanadamu anakosea, na onyo ndio mwalimu bora na hata Rais Magufuli ana makosa yeke mengi tu lakini tunayakubali tunapo ona nia yake ya dhati 2. Siamini kama Mama Kilango kafanya makusudi, maana ni mwezi mmoja na sitegemei kama amesha tengeneza mtandao ili afaidikike na pesa hiyo, maana kaenda juzi tu. Pengine hakuwa smart na kawa misled. 3. Kama Rais katuma team yake iliyo pata ukweli, angeweza kabisa kuwachukulia hatua waliolipa, walio pokea na kumwonyesha Mama Kilango weakness yake na kumpa onyo kali ili aweze kuwa makini. 4. Mwisho, kama ni zero tolerance, yapo mengi yaliyo mazito na yamefanywa kwa maksudi kuliko hili na watanzania wanayajua wazi. Kwa mfano kwa nini uozo wote huu upo kana kwamba hapakuwapo na uongozi kabla ya serikali ya Magufuli? Anachukua hatua gani maana wote tunajua kwa nini tumefika hapa, sio mmoja tu katufikisha ni wengi na china ya kiongozi kama yeye akiwapo chini ya serikali hii hi ya CCM na kuona haya yote. Je Chama kifutwe?