Precision Air mmezidi

Precision Air mmezidi

huwa najiuliza kwanini kila siku wao tu ndio mabingwa wa kucancel flight zao?
Je tuamini kuwa ni shibe?

Ila hawa jamaa kama ni ndege wanazo nyingi sasa inakuwaje wana cancel flight kwa muda mrefu sana hivyo wakati kila siku twasikia wameagiza ndege mpya kutoka France

Je tuamini kuwa hizo ndege wanazouziwa huwa ni mbovu maana haiwezekani juzi wameintro ndgee mpya leo ndege wanacancel.

Pia watanzania mnajiunga kwa kumsupport Fastjet ili huyu mtu aweke heshima
 
Hiyo Mkuu ni Imprecision Airline na wala siyo Precision Airline!!

Juzi nako ndege iliyokuwa iondoke saa 5 ikasogezwa hadi saa 5:40. Sijui wa-TZ tuna matatizo gani jamani?
 
Precision ndio zao,nimeapa sitapanda ngala ngala lao..itakua walichwa kwa sababu ndege ilijaa maana wanatabia kuuza ticket mara mbili

Nakubaliana na wewe kabisa, nlishawahi kuachwa mwanza na watu kibao eti ndege imejaa! Nikajiuliza hawakujua hilo wakati wanauza ticket au ni tamaa ya hela!
 
Precision wamecancel kama kawaida ndege ya kwenda Mwanza saa tano leo hii tarehe 9.12.2012 mpaka saa tatu usiku.

Hawa jamaa wananikera sana sana sana. Kwa anayekwenda MWanza awe alerted.....

Labda abiria hawajatosha kurusha ndege hiyo kwa hiyo wanataka kuunganidha na safari hiyo kama walikuwa na safari mara mbili kwa leo. Hii inaweza kuwa imechangiwa na Fastjet.
 
Yaani hayo yalinikuta mie jana! Reporting time ilikuwa kumi jioni(from dar to mwz) tukacheck inn. Kufika kumi na mbili tukaboard! Bwana weeeee! Pilot akatutaliisha pale uwanjani kama dk 15. Halafu akasema ndege ina matatizo kidogo so tunarudi ili mafundi wakaangalie tatizo. Akatuahidi tutaondoka saa 2 na dk 20. Muda huo kufika! Kimya! Hakuna hata maelezo yeyote! Tukakaa mpaka saa 3, abiria wakaanza zogo! Ndo mara wanatuambia ndege iko tayari twende! Yaani tumefika mwanza saa tano kasoro! Kwa kweli inasikitisha mno! Mbaya zaidi wanawapa watu ile MISANDIWICHI yao isiyo na radha, imepooooaAaa!ati kiburudisho. Kiburudisho muda wa dinner?hakya nani nilikuwa staki kupanda fast jet ila nimeamua kuipanda! Bora nijuwe nalipia cheap so na service itakuwa cheap!kuliko haya manyokanyoka ya PW na ATL. Maskini Tz!
 
Hiyo ni dala dala za Kenya Airways, wanawasomba abiria aw Kwenda America Europe na destinasheni za mbali ili wakapandie ndege Kenya ili Kenya Airways ifanye biashara na abiria aw Tanzania.... Hawakuwa wajinga kuinunua, kila kitu ya precision inaamuliwa Kenya, ila hata Kenya wageni wanaambiwa msije panda ndege Hiyo, ni jalala
 
Mi nawachukia sana walishatutelekeza mwanza airport hawa,hawana maana.

Mimi nafikili wana angalia idadi ya abiria wanao kwenda destination fulani wakiwa ni wengi wanabadirisha ruti - yaani wanataka kuiga jamaa wa dala dala wanao katiza ruti. Naona FJ imekuwa HAIR Raising KWAO - Ghafla bin vuuuum - Its time they knew when 2walk away, knew when 2RUN!
 
Precision wamecancel kama kawaida ndege ya kwenda Mwanza saa tano leo hii tarehe 9.12.2012 mpaka saa tatu usiku.

Hawa jamaa wananikera sana sana sana. Kwa anayekwenda MWanza awe alerted.....

Mkuu hii sio ndege ya kupanda,tuanze kupanda fast jest ili awa precision wajifunze hile si ndege ni taka taka
 
Labda CEO wao aliyeachia ngazi aliona haya yanakuja akala kona mapema
 
Kweli usafiri wa anga Tanzania bado tuko nyuma sana. Ukilinganisha na Kenya unaona jinsi gani tulivyo mazuzu. Hebu angalia
- Kutoka London Kwenda Nairobi kuna ndege nne kila siku. Kutoka London kwenda Dar kuna ndege moja (BA ambayo ni mara tatu kwa week)
- Wastani wa nauli kutoka London kwenda Nairobi direct £450. Kutoka London kwenda Dar direct £680.
- Ukipanda BA kwenda Nairobi kutoka London unaruhusiwa mzigo kila 46, kutoka London kwenda Dar na BA mzigo kilo 30.

Hawa jamaa awafanya Watanzania hamnazo
 
Ndege zote zinazonunuliwa na PW ni mpya- brand new!
Amini usiamini PW wana routes nyingi na hakuna ndege inayokuwa on ground kusubiria itakayopata hitilafu.
Kila ndege mpya inayokuja inapangiwa route yake, na si rahisi kuvunja route ya kwenye ratiba.
Hii ndiyo shida ya kuwa na ukame wa mashirika ya ndege nchini, lau yangekuwepo PW wangekodi ingine ikapiga route husika.
Nawasifu sana PW so far kwa kuwa National Carrier, na wanaiepusha nchi na aibu ya mwaka.
Labda niwaulize wote mnaolaumu na kubeza kazi iliyotukuka ya PW kuwa ni kipi bora, kurusha ndege yenye snag, au kuipeleka kwanza hangar ikarekebishwe hata kama matengenezo yatakula masaa 6? Naomba jibu.

Mnazifahamu vizuri ajali za ndege, na jinsi zisivyo na Mswalie Mtume katika kuchinja abiria, halafu leo mnambeza rubani anayetoa taarifa kuwa ndege ina snag! kwa watu waliostaarabika walitakiwa watoe compliment kwa PW kwa kuzingatia kanuni za Usalama wa ndege na wasafiri.

Nawapongeza sana PW kwa umakini wenu, ndiyo maana hadi leo hamjakumbwa na fatal au catastrophi accident. Huu ni uzingatiaji wa juu sana wa kanuni za usalama.

Ki-aviation inasemekana kuwa 85% ya ajali za ndege husababishwa kutozingatia kanuni za usalama. Masuala kama mchafuko wa hali ya hewa na mis-communication yanachangia percent ndogo iliyobakia.

Ndege katika hali ya kawaida ina uwezo wa juu sana wa kujiepushia ajali yenyewe inapokuwa angani. Ndege inaweza kudevelop tatizo kubwa ikiwa angani, lakini ikatumia spare-capacity yake kukata mawingu hadi mwisho wa route yake, then ikishatua haitatoa go-ahead kwa rubani kuiondoa tena hadi irekebishwe.

Sasa system za safety zenye akili namna hiyo tunazibeza, tunataka nini?

Ile kawaida yetu ya kushinda tunalaumu tusiiingize kwenye masuala ya technical, na hasa maeneo nyeti kama usafiri wa anga.

Angani hakuna parking au stendi meen.
 
Mkuu PakaJimmy, maelezo unayoyatoa ni understandable sawa(na si kwamba watu hawayajui), tunachoongelea ni delay za kila siku, kutotolewa kwa taarifa mapema, majibu mabaya n.k wanaovionyesha.. haiingii akili mmeshafanya checking then mnaambiwa ndege hakuna!Kweli??..Sometimes mizigo inapotea na luggage tag uko nayo, tena ukiwa wa kwanza katika sehemu ya kusubiria mizigo!!

Kuna siku tulikuwa tunaondoka hapa JKN Airport na PW ya jioni, check in ilikuwa saa kumi na moja(na mtu unawahi kwa ajili ya foleni ya jioni ile) lakini hatukuwa na usafiri hadi kesho yake asb.(Taarifa ilikuja kutolewa saa mbili na nusu usiku)..imagine, kuna Binti alikuwa anakaa Kimara na alikuwa yuko na mtoto wake, hawana mahali pa kwenda, na kuna mzee aliletwa tu pale na anasema mwanae anakaa huko Tegeta, sasa situations kama hizi ndizo zinazoudhi!


Unapokata ticket unaacha njia ya mawasiliano, what is the use of that?..na kama wakishindwa kutoa huduma ya usafiri kwa wakati kwanini wanashindwa kuwahudumia wateja wao(kuwajibika kwa usumbufu)? Hizo expenses nyingine alipe nani? Usalama wa wateja uko wapi?

Wakati fulani mikutanoni/kazini mtu unachelewa almost kila wakati kwa sababu tu ya delay!Na ukiwaambia

Haijalishi kama wana ndege mpya au lah! wala idadi kubwa ya ndege au wahudumu...Hata kama wakiwa na ndege kidogo(chache) lakini huduma nzuri hakuna atakayelalamika! Watu wanasema/tunasema haya kwa kuwa inaudhi na kuna expectation fulani unayoitarajia katika kupata huduma iwapo ni haki yako.

We understand kuna wakati wa services(maintanance services), lakini iwapo kuna Technical matter taarifa zitolewe mapema,
 
Last edited by a moderator:
Kwa hali iliyokuwepo Airport ilyosababishwa na Pw ku cancel ndege kubwa iliyokuwa inaenda Mwanza na kureplace na ndege ndogo atakubaliana na mimi kuwa sasa PW wamefikia mwisho wao wa kuwahudumia wateja bila bugudha.
Mimi nimefika pale ili ni check in maana ndege ilikuwa inaondoka saa 5 asubuhi kufika pale nikakuta kundi kubwa la watu, wote wanawalalamikia wahudumu. Waudumu wanadai ndege ni ndogo hivo wanahudumia wale wanaounganisha safari Dar- Mwanza-Bukoba na wale wa Dar-Mwanza -Kigoma.
Binafsi sikuelewa kwanini wamefanya hivyo, wakati nashangaashangaa nikamwona mzee mmoja kapiga koti la PW anatoa maelezo watu wanamzomea wanataka kumshughuliakia. Nilipomsikiliza nikagundua naye hana hoja, yeye anawaambia watu ambao wanlalamika wanatickets kuwa wakae pembeni ndege ya mwanza imeshajaa hivo watoe nafasi kwa counter ili wahudumia watu wengine. Watu wakawa wanahoji inamaana wo si wateja, je wao hawahitaji kusikilizwa? Inakuwaje unapomwambia mtu akae pembeni umuhudumie mwingine waakti muda wake wa kuondoka unakaribia na hujampa boarding pass? Watu wengine hawaunganishi ila wana watu wanawasubilia kuwapeleka Musoma, geita na sehemu zingine. Wao itakuwaje unaposema utawapeleka saa 3 usiku tena unaitamka kirahisi with no apology!
Basi watu wakapandwa na hasira pale wakaanza kumtukana, jamaa akawaita polisi, wakaenda na kundi kubwa polisi nikiwemo mimi. Kwa mara ya kwanza nimeona polisi akitumia busara maishani mwangu. Amemuuliza jamaa maswali ambayo hakuweza kuyajibu. Sawia na kama nilivyohoji hapo juu. Jamaa akarudi counter, system nazo zikawa chini akabaki na option moja ya kuhudumia wale wanaounganisha. Mama mmoja akaamua kumzua asifanye kazi hata hiyo ya kuhudumia wle wanaounganisha, akawa anamzuia asitumie key board yake. Duuh kasheshe liawa kubwa. Sikuamini baada ya kupata boarding pass yangu, nikazama ndani. Nimefika Mwanza na abiria wngine tukagundua mizigo yetu haikupakiwa na PW hivyo wanasema itakuaja na ndege ya usiku huu. Tulitakiwa kuondoka Dar saa tano asubuhi ila tumeondoka saa 6 mchana. Na bado mizigo ikabaki Dar. Kuna jamaa yangu alitakiwa kuondoka Mwanza kwenda Dar saa 2 usiku, wameambiwa wamecancel mpaka saa 7 usiku. Nimeambiwa hii ni kama week ya 3 mchezo huu nafanyika na hawa hawa PW, kwenye viwanja vya Dar, Kilimanjaro, Mwanza na Zanzibar. Kwa kweli sioni kitu cha kujivunia na hawa Precission Airline. Imagine nimefika ninapoendea ila vifaa vyangu vya kazi vimebaki na hivyo kunilazimu kupoteza siku nyingine kuvipata kama vitatumwa na kunifikia. Lakini nimewasikitikia walio baki maana usione mtu anaishia Mwanza ukadhani wote wanaishia Mwanza wengine wanaendlea na watu wanashida mbalimbali. Can you imagine usumbufu walioupata?
 
Poleni sana kwa usumbufu.
Bear in Mind that all those are unplanned events.
 
Mkuu Chona, what an experience?..Pole sana mkuu, hii si wiki ya tatu ni mwaka wa nne(no exaggeration whatsoever) haya yanatokea, watu hawasemi tu..siku hizi ukipanda PW lazima uwataarifu unapoenda kuwa unaweza kufika siku hiyo au siku tatu baadae.

What am wondering is, kwani haya hawayaoni? Tatizo hasa liko wapi? Kwa nini wao tu? Wamefanya nini so far kuondoa(si kupunguza) tatizo? Why are they doing that, anyway?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hippocratessocrates nikweli unachosema. Nimekuwa ikitumia Precission mara kwa mara. Hii hali imekuwa ya kupitiliza sasa. Nadhani wanafikiri kuwa hii kitu haina athari kibiashara. Lakini nakwambia watagundua roo late as the dont have a plan of rectifying the problem. Wanawachukulia abiria kama watu wasio na alternative. Waache tu maana malalamiko niliyoyasikia leo ikiwemo mimi mwenyewe plus usumbufu nitafanaya uamuzi. PW si mzazi bwana.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom