PPF yamfukuza kinara wa kuomba rushwa

PPF yamfukuza kinara wa kuomba rushwa

Status
Not open for further replies.
Katika gazeti la Guardian ya leo, PPF wametoa tangazo la kumfukuza kazi Bi. Gisella Mhoro. Dada huyu alinin'gang'ania sana mwaka jana tumkatie mafao yetu ili aweze kutoa cheque zetu. Nawapongeza sana PPF kwa kumnasa dada huyu. Mafao ni jasho la mtu, haliliwi hovyo. Natoa mwito kwa PPF wasiishie hapo bali waendelee kuwachunguza wengine.

Hapo nimefurahia sana. Ingelikua gari ningesema irudi rivasi
 
Yule mama alikua mroho kweli...Nakumbuka jamaa yangu ambaye nae alikua akifuatilia mafao alisema yule danda angelikua mzuri halafu apende hela kihivyo angemumwambia wakutane Magomeni amtere kwanza halafu ammegee mafao....Lakini muonekano wa yule dada ulimtisha.....Nadhani waliobaki watakuwa na nidhamu. Kwa vile muda wa mafao yangu umekaribia tena, nitakuja nicheck kama kuna kimbelembele aliebaki..

wewe unachukua mafao mala ngapi, haubakizi za uzeeni? au umeathirika?
 
Wamesahau kwamba huyo Gisella ni sehemu ya mtandao mrefu wa wizi. Kwa kufanya hivyo haitakuwa mwisho. suala hapa ni kuukata mtandao mzima kuanzia chini kwenda juu. Ni sawa sawa na Rais wa nchi anayesema atapambana na mafisadi wakati yeye ni zao ama "product" ya mtandao wa mafisadi na yupo kwa ajili ya kuwatetea na kuwalinda.....Kwa hiyo suala hapo ni kusafisha tuu. Sio longo longo la kutuchezea cheusi chekundu wavuja jasho wa nchi hii..

PPF ni wezi kuanzia Mkrugenzi Mkuu bwana William Erio na wakurugenzi wake wote.

1. Erio ni bilionea kupitia 10% za kwenye miradi, ndio maana akina Gisella nao wameamua kukamua wanako weza. Miradi mibovu ya Bunge na UDOM ni juhudi za kifisadi za Erio
2. Erio ni mwizi wa fedha za umma, alilazimisha kulipwa milioni 540 eti mafao ya mwisho wa mkataba wakati bado anaendelea na kazi. Wadogo nao wamejifunzia kwake na kuanza kuwakamua wastaafu maana ndipo nao wanapoweza kupafikia.
3. Erio ni mwizi na analinda wezi papa hapa PPF kama mifano michache hapa chini

A. Meshaki Bandawe: Alikula hela za wastaafu wa mashamba ya Mtibwa sugar zaidi ya milioni 20. Alipoona soo Erio akamhamishia Mwanza, na kumbambikia Kamanga hela chache zilizobaki. Walipotaka kumfukuza Kamanga naye akamtaja mwizi mkuu kuwa ni Bandawe ambaye ni kipenzi cha Bw, Erio. Erio akalipotezea na Kamanga kufutiwa mashtaka. Sasa kwa nini na wengine nao wasijichotee panapowezekana?

Huyu Meshaki akiwa uhasibu alikula sana pesa ya kodi za majengo na hakufanywa kitu, kutokana ushirika wake na DG Erio. Uhusiano wao nikiutaja hapa hii thread itafutwa leo hii.

B. Martin Mmari: Mkurugenzi wa Fedha ameweka vibaka wake idara ya fedha wanatafuna michango na kumgawia, hili sio siri wafanyakazi karibu wote wanajua. Hata hili la Gisella ni michongo ya MMari lila Gisella hakumgawia akalala nazo mbele.

Mwaka 2004 alitengeneza mazingira na kufanikiwa kununua viwanja vinne vya PPF vilivyokuwa na thamani ya Tshs 56Milion lakini akanuna kwa Tshs 16milion vyote vinne.

C Hosea Kashimba: Huyu ni Chief Internal Auditor. Kila akigundua huwafuata waharifu wamgawie na kulizima soo. Wanaomkomalia huchochea wafukuzwe

Mwaka 2004, Mkurugenzi wa fedha aliponunua Viwanja vinne kiujanja ujanja, akagawiwa viwili ili asihoji. Vijana wanaangalia tu ndio maana nao wakipata mwanya wanavuta kwenye shamba la bibi PPF

Mwaka 2008 Alilipwa Tshs 220 milioni kinyume na taratibu za PPF malipo ya Group endowment ambayo hulipwa kwa mstaafu tu sio aliyekazini kama yeye. Vijana wanaangalia tu. Kama serikari inawaogopa wakubwa basi na wao wakaamua kudokoa mafao ya wazee wasio na hatia. Tatizo in kutamani jinsi mabosi wanavyo ifaidi PPF wakati wadogo wanakufa njaa na kuscramble kwenye daladala.
 
Huyu mdada ni soo. Alikuwa NMB Moro akatimulia kwa sababu ya kulamba fweza.
 
Makubwa Kafukuzwa na Ijumaa kakamatwa na polisi.adi jana alikuwa anasota rumande jamani omba Mungu asikupe uroho na tamaa ya pesa.Maana huyoo mama alikuwa na kila kitu na mme wake ni mwanajeshi.ila safari hii PPF wamemkamata utamu.28Mls zimuponza.Watatajana vizuri pana chezea pesa za mafao ya watu.
huyu demu wizi alishazoea siku nyingi. kule morogoro alikuwa anaiba kutoka kwenye akaunti za watu ambao siku nyingi hawajachukua pesa benki, anafoji sahihi analasmba mshiko akaja akanaswa akafukuzwa. alikuwa nmb wami branchi.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom