PPF Group Endowment Saga: THE FINAL REPORT

Status
Not open for further replies.
For reasons only known to a ghost sipati hii attachment. only cover photo. au mwanakijiji unachagua nani awe na access ya hii link:) ?

acha hizo bwana.. mbona watu wanajinoma wenyewe huko waliko?
 
Nimejikuta nimesoma hii ripoti kama asilimia 80.
Inasikitisha sana..Inaonesha ni kwa jinsi gani watu walivyokuwa binafsi.. Mameneja wamepindisha sheria ili tu wajilipe karibu milioni mia mbili (200,000,000) kila mmoja.

Yaani HR anatakiwa aende jela moja kwa moja kwa kutafsiri mikataba vibaya....eti anasema Chief Accountant 'was not happy with the payments'...pia anasema alipaswa awajibike moja kwa moja kwa Director of Finance ambaye pia alimuonya CA kwa nini hakulalamika kwake instead akaandika barua kwa DG..

Watanzania wenzangu, hizi hela ni nyingi sana. Hebu fikiria mtu anafanya kazi ya mkataba kwa miaka mitatu or so, anaondoka na mamia ya mamilioni, halafu anaajiriwa tena kwa kuongeza mkataba, akitegemewa kulipwa tena hayo mamilioni kwa mara nyingine..

Sina mengi ya kusema, lakini huwezi kuamini Tanzania ni maskini, kwa jinsi watu wanavyojua kula pesa..tutapiga sana kelele, lakini watu wanakula nchi kiulaini kabisa.

Ajira zenyewe za kupeana.. mtoto wa Saidi Mwema, Musiba, n.k! Sijui, lakini ningependekeza mtu achukue maamuzi mazito kwa faida ya nchi.
 
Does this mean kwa sababu JF haikualikwa kwenye mkutano wa PPF na MEDIA ndio maana imetolewa?

ERIO inaonekana ame under estimate JF kwa kiwango kikubwa sana
 
MMMJ,Kama utakumbukja hii issue ilikuwa raised Bungeni mwaka 2007 na Halima Mdee , na serikali kama kawaida yao wakapindisha , na iliunganishwa kwa pamoja na wafanyakazi wa Bandari ambao wanachukua nyingi kuliko hizi kwa mikataba hiyo hiyo ya miaka 3 .

Kamati ya Mashirika ya umma inapaswa kulifanyia kazi hili kwani PPF ni miongoni mwa mashirika yaliyoko kwenye utendaji wake wa kazi .

Haiwezekani Prof.anaandika vitabu mpaka anazeeka kwa miaka 30 akistaafu halipwi hata nusu ya hawa jamaa tena kwa miaka 3 tuu kuna haja wafanyakazi wachukue hatua kwani wanaibiwa na mifuko hii.
 
nimeisoma vizuri hiyo attachment, aisee tanzania yetu watu wanajua kuimega na mungu kama yupo ipo siku atasikia kilio cha watanzania.
ni ufisadi uliotukuka
 
For reasons only known to a ghost sipati hii attachment. only cover photo. au mwanakijiji unachagua nani awe na access ya hii link:) ?
hapo juu ya cover photo kuna kibox kidogo kimeandikwa download with an arrow pointing downward, click that nadhani utaweza kuiaccess document na uwe na PDF downloaded in your pc as document iko kwa PDF format.
 
Ahsante Mwanakijiji...

JK - hili swala huhitaji ushahidi mwingine zaidi ya report hii. Tafadhari chukua hatua ya kuwaonea huruma hawa watanzania maskini kwa kuanza kuwashughulikia hawa watuhumiwa. Wafute kazi, kisha ruhusu tume ya Bunge kama ile ya Richmond/Downs ifamie pale PPF kwa uchunguzi.

Inasikitisha sana kuwa nchi hii imefanywa "Shamba la Bibi" kama waswahili wasemavyo. Nchi inakuwa mahali pa watu kujichumia Pesa na kuanza mbele. Kwa hahika, siku zinahesabika.
 
Thank you Sir! Naendelea kusoma huku nikipoza koo na maji ya bomba!
 
Asante Mkuu. Nimeisoma na kutafakari yaliyomo.
Aidha kwa vile zama zile nami nilijinoa JKT kwa mujibu wa sheria kabla ya kuendelea na elimu ya juu ndani na nje ya nchi, imebidi nijiulize kama sacrifices zetu miaka ile zilkuwa za kuwaandalia mafisadi 'maisha ya peponi' hapa Tanzania.

Kama ulivyo UFISADI uliokubuhu katika nyanja nyingi nchini mwetu, nimebaki najiuliza kwamba... mimi kama individual nahitaji kufanya nini au kuchukua hatua gani kupambana na mauzauza haya. Ndio ina-udhi mno. Haitoshi tu kisikitika. Je nawezaje kushusha donge nililo nalo kooni? Solution inaweza kupatikana katika kufanikisha ukombozi ifikapo 2015 ingawa hilo nalo is quite an uphill task. Ili nibaki kwenye mada inabidi kwa leo niishie hapa.
 
Nimeisoma na kuelewa kwa upande mmoja.Upande mwingine ni kwamba watumishi wanapopata nafasi ya kujiwekea
nafasi ya kula wanakula sawasawa bila kuacha kiporo.
Sasa hawa walipata nafasi ya kujijadili na kujitengenezea CHAKULA baada ya kustaafu wao na ndicho kinachofanyika serekalini kwasasa.
Mfano huu hauna tofauti na ule wa wabunge wa sisim ambao ulitengeneza CHAKULA kwa wabunge kwa kulipana posho kubwakubwa
na mishahara mikubwamikubwa mpaka Dr Slaa akashangaa bila kujua alikuwepo wakati wa mchakato.
Nkisoma hii report naona kama ni taarifa ambayo inasema kile kilichoamuliwa na board of Directors pia kiko kwenye secular ya serekali na ni maamuzi ya Bunge pia.


Kazi nzuri MM.Mwanakijiji.
 
Shukrani sana M.MKJ kwa kazi nzuri sana.

Nimeisoma kwa haraka haraka hii ripoti, lakini naona imejitosheleza kwa kweli, umechimbua na kuweka mambo hadharani kiasi kikubwa sana. Binafsi nimejifunza vitu hapa, ngoja nitariduia kwa utulivu zaidi ili kupata kujua mambo yakoje ndani ya shirika hili.

Katika hili, kama kuna mtu alikuwa bado ana wasiwasi nadhani sasa atakuwa amefunguka macho na kuona ni namna gani anaweza kuunganisha nguvu na fikra kwa ajili ya kuchangia kuleta mapinduzi ya kweli katika serikali yetu kwa ujumla.

Kama ulivyodokeza kwamba unakwenda kwenye sabbatical, nadhani itakuwa vilevile ni kwa ajili ya tathmini ya kazi kubwa sana na nzuri sana ambayo umekuwa ukiifanya, lakini pia naamini tunatarajia kupata "fikra pevu" mpya kwa ajili ya ukombozi wa nchi yetu na mashirika yetu ya umma.

Mungu aendelee kukubaliki sana, naamini huo mstari wa 1 wafalme umeuelewa vizuri sana na bila shaka umekupa nguvu ya kuendelea kuamsha "imani" za watanzania kwa ajili ya ukombozi wao.
 
Mkuu nimeipata . swafi.

Kwa haraka haraka, penye jina Michael Minja naomba isomeke Michael Mjinja. huyu ni mtu wa Musoma sio Mchagga!

Aisee,

Unaogopa mashambulizi yasije yakageuka kuelekea upande huo, sio?

Nape na acp massawe wanakusumbua kiasi hicho kumbe??

Awe mjita, mkurya ama mchaga anatakiwa kushughulikiwa tu, tukianza kuangakia makabila ya watuhumiwa tutakuwa tunapoteza mwelekeo, na kazi yote nzuri ya mwanakiji itakuwa haina maana tena, hebu jivue gamba katika hili!!
 
Ndiyo maana wakina @NYC tunawaona kama vichaa hapa kuja kuishabikia CCM ni haya marupurupu ndiyo yanawafanya wawe wehu kabisa. Nchi ambayo kila mtu ni mbinafsi haiwezi kuendelea. kwenye foleni za barabarani kila mtu anataka afike haraka kuliko aliye mbele yake aliyetangulia na mwisho wake ni que ndefu kabisa kila siku
 
Katika hii ripoti nzima ni kuangalia kitu ambacho naweza kukiita ni jinsi Ufisadi unavyotengenezwa. This is very typical. Ni kama kuna Chuo cha Ufisadi ambapo watu na suti zao hukaa na kufundishwa kuwa wakishika madaraka basi wafanye x,y, na z ili kujitengenezea ulaji. Mojawapo ya vitu vinavyofanyika sana ni "kuongeza maana" ya taratibu mbalimbali wakati mwingine hata kuweka maana mpya kabisa. Hili tuliliona kwa kina sana kwenye sakata la ATCL ambapo mtu mmoja anatokea katika sehemu mbili zote - sijui hili lina maana gani.

Kinachotakiwa kuwaudhi Watanzania mahali popote ni ule ukimya na utayari wa serikali kutetea visivyoteeka na kulinda visivyolindika. Jibu la serikali ni kusema "taratibu hazikufunjwa" well, walioandika taratibu hizo ndio hao hao waliojilipa sasa watazivunjaje taratibu walizojiwekea ili kula?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom