Anaweza kuongoza lakini siyo rahisi kama mnavyofikiria hasahasa kwenye nchi kama
Korea-Kaskazini: Sehemu yoyote ile ambako wanaangalia
THE CULT OF PERSONALITY huwa haiwi rahisi kwa jinsie
KE kufika juu kirahisi.
Tunaweza kujitia moyo kwa kuwaangalia watu kama
Margaret Thatcher lakini ni lazima ujue historia na tamaduni ya nchi kama Uingereza: Demokrasia ya nchi ya Uingereza ndiyo komavu kuliko Demokrasia yoyote ile ambayo wewe umewahi kuisikia na ina miaka zaidi ya
(700) Mia Saba.
Pia tamaduni za Uingereza ni tofauti kabisa na Korea-Kaskazini au Marekani.
Uingereza hata kabla ya kuwepo taifa la Ujerumani na Marekani walishakuwa na viongozi wanawake kama
Malkia Elizabeth wa I tokea mwaka
1558; tena wakawa Malkia mwingine Victoria tokea mwaka 1837 huko na hadi leo Uingereza inaongozwa na
Malkia Elizabeth wa II.
NB 1: Kipindi cha
Malkia Elizabeth wa I na
Victoria Uingereza ndiyo ilikuwa ndiyo dola kubwa na lenye nguvu hapa duniani. Sasa nchi kama hii kwanini waone kitu cha ajabu au waogope kuongozwa na mwanamke ??? Marekani mwenyewe anayejiita nid Demokrasia komavu anaogopa kutawaliwa na mwanamke (Huu ndiyo uhalisia hata ukilia utabakia tu kuwa uhalisia)
NB 2: Korea-Kaskazini iliharibiwa kitamaduni na utawala wa Japan na imetoka kwenye Ukoloni wa Japan mwaka
1945 baada ya Vita vya Pili vya dunia. Mwaka
1947 na kuendelea wakaingia kwenye mfumo wa Kidikteta na Kikomunisti hadi leo; sasa wewe unataka kusema kwamba nchi ambayo haijawahi kuwa na historia ya mwanamke kiongozi huko nyuma na bado iko chini ya Udikteta inaweza kumruhusu mwanamke awe kiongozi kirahi-rahisi tu ??? (Please be realistic and serious).
NB 3: Kitu ambacho mnasahau tena ni kwamba Mfumo wao wa Kiutamaduni na Kielimu (
WESTMINSTER INFLUENCE)wa Uingereza ndiyo uliweza kuathiri hata makoloni yake kama
India na
Pakistani hadi kuwashawishi kuona kwamba kuwa na kiongozi mwanamke kama
Indira Gandi na
Benazhir Bhutto ni kitu cha kawaida sana (Tafadhali soma historia vizuri) Lakini Ukweli mchungu ambao wengi hatuutaki kuusema ni kwamba kwenye nchi nyingi za Kiislamu wanawake huwa hawapewi kipaumbele kutokana na tamaduni na dini. Hata
India mnamo
Karne ya 13 (wakati ni Dola la Kiislamu ilishwahi kuwa na Sultana Mwanamke anaitwa
Raziya al-Din au Razia Sultana lakini wanaume wa Kiislamu hawakukubali kuwa na kiongozi mwanamke na kuamua kumuua.
NB 4: Waswahili tunasema ukiona "vinaelea ujue vimeundwa": Usichukulie vitu kwa ujumla-jumla
(Generalization of things) na kufuata kauli kama Kama "
Fulani kaweza na mimi basi naweza" bila kujiuliza maswali ya Msingi kama:
- Kwanini fulani kaweza kufanikiwa katika kile kitu ??
- Je, mazingira yangu yanalingana na fulani ili niweze kumuiga ???
- Je, nikimuiga fulani na mimi nitapata mafanikio kama yake ???
- Je, nikijaribu kufanya kama fulani nitawaathiri vipi wanaonizunguka ???
Always try to be
EMPIRICAL ask yourself this question "
WILL IT WORK WITH ME AND AVERT MY CIRCUMSTANCES ???" and stop clinging to these
crude and
clumsy Humanist Theories like
FEMINISM. Good things do not just brood out of oblivion my friend.