Power structure ya North Korea

Power structure ya North Korea

Malcom Lumumba

Always try to be EMPIRICAL ask yourself this question "WILL IT WORK WITH ME AND AVERT MY CIRCUMSTANCES ???" and stop clinging to these crude and clumsy Humanist Theories like FEMINISM. Good things do not just brood out of oblivion my friend.
Huwa nakubali sana chambuzi zako kaka Malcom Lumumba, hususani JI&IF humu. Ulipoondoka nilisononeka, ila tangu urudi imekuwa shule tena baada ya likizo. Pamoja sana mkuu.
 
Bahati mbaya sana first born wake ni mwanamke sijui itakuwaje!
Lakini yote tisa Korea Kaskazini haifahamiki kirahisi na sisi watazamaji wa nje!
Wachunguzi wengi walihisi kwamba uongozi wa nchi angepewa Kim Jong-Chul kaka yake na Kim Jong-Un lakini 2009 akatangazwa Kim Jong-Un kama mrithi. (The Country is full of surprises)

Japo kuna mlengo ambao unawaza kama wewe.
Wanasema kwamba Kim Jong-Un akiondoka basi kutakuwa na ombwe kubwa sana la kiuongozi (Power Vacuum) ambayo itasababisha makundi madogo madogo kupigania madaraka na mwishowe nchi yote itasambaratika. RAND CORPORATION hadi walifanyia utafiti hili jambo na Dr. Bruce W. Bennet akaliandika chapisho la zaidi ya kurasa 300 hivi.
(Nimeliambatanisha hapa chini)

Ni maoni mazuri lakini ili kuelewa hali ya kisiasa ya Korea Kaskazini ni lazima tuangalie historia yake kwa jicho la tatu kabisa. Professor Noam Chomsky anasema kwamba Korea Kaskazini iko tofauti kisiasa na Iraq, Libya na Afghanistan; Marekani atakuwa anakosea sana kama anahisi Korea Kaskazini itaanguka baada ya Kim Jong-Un kuondoka. Mfano mzuri kabisa Korea Kaskazini ilikumbwa na Baa la njaa mwaka 1994-1998 na mamilioni ya watu walikufa sana na kibaya zaidi nchi ilikuwa na vikwazo vikali lakini Serikali ya Kim haikuyumba. NATO, Korea Kusini na Japani walitegemea ule ndiyo ungekuwa mwisho lakini hakuna kitu. (Jamaa wanadunda mpaka leo)

KTanzania baada ya vita ya Kagera njaa ilifanya wakiana Zacharia Hanspope wamfurumushe Mzee Nyerere: Kibaya zaidi Nyerere akafa na nchi yote haina mwelekeo mpaka leo. POLITICAL TEXTURE za nchi ziko tofauti sana kwa hiyo kutaka kutabiri yatakayotokea Korea Kaskazini kwa kulinganisha maanguko ya Saddam Hussein, Slobadan Milosevic na Muhammar Qaddafi ni mawazo ya mwenda wazimu (FALSE HYPOTHESIS kutengeneza FALSE INFERENCE)


NB 1: Baada ya Vita ya Kwanza ya dunia viongozi kama Lloyd George, Georg Clemenceau na Vitario Orlando walihisi kwamba wakimuua Vladmir Illyich Ulyanov Lenin ndiyo utakuwa mwisho wa Urusi ya Kisovyeti (Walisema kwamba bila Lenin wakomunisti hawana kichwa na yeye ndiyo kila kitu pale). Lenin alipigwa Risasi na hicho ndicho kikawa chanzo cha kuwaunganisha zaidi Wakomunisti nchini humo, bahati mbaya akafa mwaka 1924 kwa Kisukari na Majeraha ya Risasi yasiyopona lakini Urusi ya Kisovyeti na Kikomunisti kama ilivyo Korea Kaskazini ikadumu hadi mwaka 1991.

NB 2:Wakorea Kaskazini wanaweza kumtoa Kim Jong-Un hata leo lakini ukweli ambao haufichiki ni kwamba hata kiongozi ambaye atakuja baada ya Kim Jong-Un atakuwa na kitu kimoja kinacholingana na familia ya Kim (Chuki dhidi ya Wamarekani na Mataifa ya Magharibi). Wakorea wanakumbuka vizuri sana ambacho Marekani aliwafanyia mwaka 1953-1953 (Unnecessary Use of lethal force to target civilian objectives Contrary to the Geneva Conventions of 1949 and Hague Rules of 1907) Hata aingie nani Madarakani Marekani uadui hauwezi kuisha. Professor John Mearsheimer anasema hivi "Katika sehemu zote za dunia, historia huwa haifi kwenye nchi za Mashariki ya Mbali" kifupi huwa hawasahau maadui zao.

CC: Bukyanagandi , Red Giant , izzo , MSEZA MKULU, Consigliere, herikipaji , Complex , mtembea kwa miguu , Gide MK , gwijimimi , Dotworld , py thon , Bilionea Asigwa, Econometrician , kilwakivinje , Mbimbinho , God Heals, kichakaa man, Lelommassy
Duuuh sorry for the inconveniences, nilipoanza kusoma bandiko hili...nikahisi ni wewe kiongozi. Asante kwa maarifa.
 
Hao jamaa wa NK watakubali kweli waongozwe na mwanamke?

Mwanamke ataweza kuchimba biti kama mwanaume?

Sijui suala la sexism likoje huko NK.
Huyu Kim ana Dada yake ambaye ana cheo kikubwa sana katika jeshi nadhani anaweza kuvaa viatu Vya Kaka yake bila shida yoyote kwani wanaelewana sana wawili Hawa pia Kim anamuamini sana huyo Dada yake ndio maana amempa nafasi kubwa tu jeshini
 
Hivi kwa mfano ikitokea kesho 'Little rocket man' anakufa, ni nani huko North Korea atashika hatamu za uongozi?

Manake nijuavyo huko NK 'little rocket man' ndo kila kitu.

Na yeye bado ni bwana mdogo sana. Hata kama ana watoto basi hao watoto watakuwa ni wadogo mno kuweza kurithi uongozi wa hiyo nchi.

Nahisi kutakuwa na mtafaruku mkubwa sana....
Kwani kabla hajashika madaraka ulikuwa unajua nani angekuwa kiongozi
Hapo kuna mtu anaandaliwa kwa siri na unaweza kukuta yuko Ulaya anasoma na hajulikani
Chezea korea kaskazini wewe
 
Kwani kabla hajashika madaraka ulikuwa unajua nani angekuwa kiongozi
Hapo kuna mtu anaandaliwa kwa siri na unaweza kukuta yuko Ulaya anasoma na hajulikani
Chezea korea kaskazini wewe

Kabla baba yake hajafariki ilikuwa inajulikana kuwa huyu wa sasa ndo angemrithi huyo baba yake kwa sababu alikuwa ni mkubwa vya kutosha.

Sasa yeye huyu hana watoto wakubwa wa kuweza kumrithi.
 
Back
Top Bottom