Porokwa apasua jipu la CCJ

hivi hili la mwanzilishi, lina faida gani kwa siasa zetu? Waanzilishi wa CDM, CUF, NCCR ni kina nani? Maana ukiachana na uanzilishi, hivi wangapi wametoka upinzani kwenda CCM na vice versa? Inasaidia nini hii katika siasa zetu?

Watanzania kweli wagumu kuelewa mambo rahisi kabisa! Tatizo hapa ndugu yangu Anfaal ni kwamba hao wa vyama vingine vyote ulivyotaja walikuwa open kabisa, hawakujifichaficha kama hawa wa CCJ, isipokuwa Mpendazoe tu. Kama Nape, Mwakyembe na Sitta walianzisha CCJ (kitu ambacho ni haki yao kikatiba) -- kwa nini wajifiche? Ni wanafiki tu!
 
Hongera Parokwa kwa kutujuza, "...Nilikutana mara kadhaa na Mh. Nape Nnauye, Mh. Dk. Harrison Mwakyembe na Mh. Fred Mpendazoe."

Majina ya Waanzilishi yapo kwa Msajiri wa Vyama, hapa JF msiponzwe na siasa za majitaka za Mapacha 3 wanamtumia POROKWA agange njaa.
 
hivi hili la mwanzilishi, lina faida gani kwa siasa zetu? Waanzilishi wa CDM, CUF, NCCR ni kina nani? Maana ukiachana na uanzilishi, hivi wangapi wametoka upinzani kwenda CCM na vice versa? Inasaidia nini hii katika siasa zetu?
Ni muhimu kuwajua kwasababu ni viongozi wa kitaifa mfano leo Mbowe tusikie kahamia CCM au CUF halafu tuache kujadili kwa sababu wengi wanahama vyama, wewe hata ukihama vyama 21+ huna impact yeyote kwanza hatukujui.
 
Majina ya Waanzilishi yapo kwa Msajiri wa Vyama, hapa JF msiponzwe na siasa za majitaka za Mapacha 3 wanamtumia POROKWA agange njaa.

You are wrong there!!!!!!! Si lazima majina yote ya waanzilishi yawepo katika daftari la msajili! Narudia, siyo lazima! Watajwa walihusika 100 pwercent ila hawakutaka kwanza majina yao yajulikane hadi chama kingepata permanent registration ili wajitokeze, na baadhi yao -- kama vile Sitta -- kugombea urais.

Kwa nini hutaki kuona along these lines?
 
TUJIKUMBUSHE......

Porokwa na Lowassa wana siri moja

Na Saed Kubenea
Imechapwa 09 June 2010


DANIEL ole Porokwa, amenaswa na nyavu za mbunge wa Monduli, Edward Lowassa. Polokwa wa zamani siyo wa leo. Wanasema amefaulu kumeza ndoana. Kama ni matatizo yatatokea tumboni lakini siyo kooni. Mwanachama huyo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), aliyekuwa ameahidi kumpokonya kiti Lowassa, sasa anasema hatagombea ubunge.

Ni zaidi ya miaka miwili sasa tangu Porokwa atambe kuwa atagombea ubunge katika jimbo la Monduli, mkoani Arusha; lakini sasa amevunja ahadi yake. Aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam, Jumapili iliyopita, kuwa amefikia uamuzi huo wa kujitoa katika kinyang'anyiro baada ya kushauriwa na wazee wa kimila kutoka kabila la Wamasai ambao hufahamika kwa jina la Malaigwanani.


Porokwa ametaja sababu tatu anazosema zimemfanya kuchukua uamuzi wa kutogombea ubunge jimboni mwake.Kwanza, amesema amefanya hivyo baada ya kutambua kuwa Lowassa ndiye kiongozi mkuu wa kimila wa wazee wa kimasai – Malaigwanani.


Hivyo basi, akiwa kijana aliyelelewa vizuri na anayezitambua mila za kabila lake, hakuona busara kushindana na kiongozi wa kimila – Lowassa.

Pili, Porokwa amesema ameamua kuachia ngazi kutokana na kutambua kwamba chini ya uongozi wa Lowassa, jimbo la Monduli limepiga hatua kubwa kimaendeleo na kwamba safari hii ndiyo itakuwa ngwe ya mwisho kwa Lowassa kuwatumikia wananchi wa Monduli.


Tatu, amesema amefikia uamuzi huo kutokana na upendo mkubwa alionao kwa familia yake, hasa mke wake ambaye tangu alipotangaza azima ya kugombea ubunge wa Monduli, amekuwa mtu wa majonzi kutokana na kutotaka mume wake (Porokwa) agombee ubunge.

Sababu hizo tatu zimezua mjadala mkubwa. Sababu ya pili inaonekana moja kwa moja kuwa alikabidhiwa aitaje; siyo yake.

Sababu ya kwanza inaonekana kuwa kisingizio tu, kwani Porokwa amekuwa Mmasai miaka yote ya maisha yake. Hawezi kudai kuwa leo ndio anagundua kuwa anastahili kuheshimu wakuu wa kabila lake.

Sababu ya tatu ndiyo inazaa utata zaidi. Kitu gani kinafanya mke wake apende Lowassa aendelee kuwa mbunge kuliko yeye (mume wake), hasa katika mazingira ya mafao?

Siyo rahisi sana kumbishia Porokwa kwa sababu alizotoa; lakini hapa kuna kila sababu ya kujenga mashaka.


Kwanza, si kweli kwamba Porokwa amejiondoa katika harakati za kuwania "ubunge wa Lowassa" kwa sababu ya kutambua kuwa Lowassa ndiye kiongozi Malaigwanani. Ni Porokwa huyuhuyu anayesema amejiondoa kuwania ubunge Monduli, kwa kuheshimu mila za Kimasai, ambaye alikuwa anahubiri hadharani kuwa Lowassa si Mmasai. Amenukuliwa mara nyingi na vyombo vya habari akisema Lowassa hastaili kuwa kiongozi wa Wamasai kwa kuwa Lowassa siyo Mmasai. Mara zote Porokwa amekunuliwa akisema Lowassa anatoka kabila la Wameru.

Ni Parokwa huyu aliyetaka kupeleka kundi la waandishi wa habari jimboni kwa Lowassa kuthibitisha madai kwamba Lowassa ni Mmeru na kwamba umasai anaojipachika ni wa "kuchonga."

Alisema wazazi wa Lowassa walihamia Monduli miaka mingi iliyopita na kwamba hata jina la Lowassa linadhihirisha madai yake; si miongoni mwa majina ya Kimasai. Sasa kama hili ndilo alilolisema huko nyuma, hiki anachikisema leo kimetokana na msukumo upi?


Kama si hivyo, madai yake ya awali yalilenga nini; kumchafua Lowassa au kulikuwa na ukweli ndani yake? Kama alilenga kumchafua, nani alimlipa kwa kazi hiyo na alilipwa kiasi gani kufanya kazi ambayo leo hii anaikana?

Sasa amebadilika. Amezaliwa upya katika imani tofauti inayolenga kumpigia debe Lowassa. Tayari wengi wanauliza: Amenunuliwa? Hapa ndipo suala la kulipwa au kutolipwa linapopoteza maana: kulipwa ili uchemke na kulipwa ili upoe? Kwa gharama ipi, kwa kiasi gani cha shilingi mtu aweza kujikana mbele ya mke, watoto na jamii yake?Kwa kujua hili, Porokwa aliharakisha kuwaambia waandishi wa habari kuwa hakuhongwa kufanya alichofanya.
Vyovyote itakavyokuwa, wengi watabaki wakijiuliza ni kitu gani ambacho kimeleta mabadiliko katika akili ya Porokwa na kufanya uongo anaokana kuwa ukweli anaotaka tuamini.

Hoja ya Porokwa kuwa ameamua kuachia ngazi baada ya kutambua kuwa chini ya uongozi wa Lowassa, jimbo la Monduli limepiga hatua kubwa kimaendeleo, haingii akilini. Ni kijana huyu aliyetuhumu Lowassa kuwa hajafanya kitu chochote cha maana Monduli.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari mwishoni mwa mwaka jana, alinukuliwa akisema, "Lowassa hajafanyia kitu wananchi wa Monduli, zaidi ya kutumia mgongo wa wananchi wa Monduli kujinufaisha binafsi."

Alisema hata ule uwaziri mkuu aliokuwa anashikilia, haukusaidia wananchi wa Monduli. Alidai uwaziri mkuu huo, ulimsaidia Lowassa na familia yake tu. Kama haya ndiyo alitamka hadharani wakati huo, mangapi ambayo ameyatamka kwa siri na ambayo wale aliowaeleza bado wanayakumbuka?


Kwa mara nyingine, siyo rahisi kutilia mashaka majonzi ya mke wa Porokwa kila mumewe anapotaka kuchukua "ubunge wa Lowassa."


Hii ina maana tangu mwaka 2005, Porokwa alipotaka kugombea, mkewe amekuwa kwenye "majonzi makubwa" kuona mume wake anataka kupokonya kiti cha Lowassa. Majonzi ya "mama" katika vita hivi vya panzi wa kisiasa, yaweza kuthibitishwa na mama huyohuyo; si Porokwa au hata Lowassa. Bali kama ni kweli, majonzi hayo yaweza kuthibisha mvuto na mguso wa kisiasa wa aina yake hata kwa wasio na fursa ya kupanda jukwaani.

Kuna madai kwamba Parokwa aliondoa jina lake katika kinyang'anyiro cha 2005 baada ya kuahidiwa na Lowassa kuwa atapewa nafasi ya "mkuu wa wilaya." Hata hivyo, hakufanikiwa kupata nafasi hiyo kwa madai kuwa hakuwa na elimu inayohitajika kwa nafasi hiyo. Badala yake Parokwa aliibukia Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Tengeru, mkoani Arusha ili kupata elimu ambayo inadaiwa ndiyo Lowassa alitaka. Lakini wakati anamaliza masomo yake Tengeru, Lowassa alikuwa tayari ameshapoteza uwaziri mkuu wake. Hii ilifuatiwa kuhusishwa kwake katika kashfa ya mkataba wa Richmond. Hapa ndipo ndoto ya Porokwa ilionekana kufunikwa na wingu jeusi ambamo alifurukutia kwa madai ya "Lowassa siyo Mmasai."


Kimsingi hakuna anayelalamika kwa hatua ya Parokwa kuvunja ahadi yake ya kugombea ubunge Monduli. Hata andishi hili haliwasilishi malalamiko, bali linatoa sura nyingine ya wanaozaliwa upya kisiasa. Kijana huyu wa Monduli atakumbukwa kwa kuwasilisha malalamiko mbele ya rais, akituhumu Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba kumuondoa katika nafasi yake ya katibu msaidizi wa CCM, wilayani Hanang.

Hii ilifuatia madai ya Porokwa kuwa Makamba alinukuliwa akimueleza George Mkuchika, naibu katibu mkuu wake kwamba "mwenyekiti (Jakaya Kikwete) amekasirika sana."

Kauli hiyo ilihusishwa na kuteuliwa kwa Porokwa kuwa katibu Hanang na kwamba Kikwete hakupenda uteuzi huo. Je, katika hali hiyo, wale waliokwenda kwa rais kumtetea Parokwa, anawaweka katika mazingira yapi mbele ya Lowassa? Bali mnofu wa kauli za Porokwa umo katika maneno haya: "…nimeamua kuachia ngazi baada ya kuona kuwa hii ndiyo itakuwa ngwe ya mwisho kwa Lowassa kuwatumikia wananchi wa Monduli." Amepata wapi ushahidi wa jambo hili kama siyo kwa Lowassa? Je, inawezekana amekutana na Lowassa na wakaahidiana "kitu" katika siku za usoni?


Tangu Porokwa aseme kuwa hii ni mara ya mwisho kwa Lowassa kuwa mbunge wa Monduli, Lowassa hajakana. Je, Lowassa atagombea nini mwaka 2015 kama "msemaji wake" anasema hatagombea ubunge? Je, atagombea urais?Hivi Porokwa ana uhakika gani kuwa Lowassa atashinda nafasi anayotaka kugombea? Amemhakikishia vipi kuwa iwapo atashindwa hatarudi kutaka ubunge wake?

Kwa hiyo kama Lowassa na Porokwa waliteta na kukubaliana, lolote laweza kufanyika – kwa Lowassa kutorudi Monduli au kurudi iwapo mipango yake ya masafa marefu haikufanikiwa. Jambo moja litabaki kuwa chungu. Majonzi ya mke wa Porokwa hayataisha hadi ithibitike kuwa Porokwa hampingi Lowassa. Hilo nalo ni somo.


Porokwa ambaye pia ni Mwenyekiti mstaafu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (VCCM) mkoani Arusha,
Alisema tayari ameanza kufanya maandalizi ya kumtafuta Lowassa, ili amuombe radhi.
 
Majina ya Waanzilishi yapo kwa Msajiri wa Vyama, hapa JF msiponzwe na siasa za majitaka za Mapacha 3 wanamtumia POROKWA agange njaa.

Usilete hoja zilizo cheap kabisa. Msajili hawezi katika orodha yake kuwa na wote wanaoanzisha chama. Mapema miaka ya 90 mimi (na mamia Wtz wengine) nilihudhuria mkutano pale diamond jubilee Hall ulioanzisha NCCR-Mageuzi. Lakini jina langu halikuwapo katika orodha ya msajili.

 
Majina ya Waanzilishi yapo kwa Msajiri wa Vyama, hapa JF msiponzwe na siasa za majitaka za Mapacha 3 wanamtumia POROKWA agange njaa.

Watanzania kweli wagumu kuelewa mambo rahisi kabisa! Tatizo hapa ndugu yangu Anfaal ni kwamba hao wa vyama vingine vyote ulivyotaja walikuwa open kabisa, hawakujifichaficha kama hawa wa CCJ, isipokuwa Mpendazoe tu. Kama Nape, Mwakyembe na Sitta walianzisha CCJ (kitu ambacho ni haki yao kikatiba) -- kwa nini wajifiche? Ni wanafiki tu!

hivi hili la mwanzilishi, lina faida gani kwa siasa zetu? Waanzilishi wa CDM, CUF, NCCR ni kina nani? Maana ukiachana na uanzilishi, hivi wangapi wametoka upinzani kwenda CCM na vice versa? Inasaidia nini hii katika siasa zetu?

Ni kweli tupu. Hakuna kudanganyana. Mimi si gamba, ni mwanaCCM halisi. Mmoja wa Mwiko wa CCM ni kuseme ukweli. Katika mkutano wake huu, Porokwa ameeleza hivi, "Nimeamua kuyasema haya baada ya kuwasikia Mh. Nape na Dk. Mwakyembe wakimkana Mh. Mpendazoe na kimsingi wakikana chama chao – CCJ.
Napenda kuwaambia Watanzania, kwamba CCJ ni chama kilichoanzishwa na kuasisiwa na viongozi hao wawili, pamoja na Mh. Sitta kama ambavyo Mpendazoe alivyoeleza.

hii ina maana waliotajwa ni wanafiki
wanauchu wa madaraka kwa kutaka kotekote
walipopewa madaraka wakatulia hivyo sio wapambanaji kwa manufaa ya wananchi bali manufaa binafisi
mwisho hawa sio viongozi thabiti hawana msimamo na wananyumbishwa na maslahi binafsi.
hivyo hii ni habari muhimu tena sana, ndio maana sitta anasema yeye ni mtaji wa uraisi maana anaona kwamba yeye tu ndiye anayefaa kuwa raisi wa nchi hii, anapigania tumbo lake tu.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Me nilijua jana akina Mwakyembe na Six walikuwa na ajenda ya sri kurdisha kadi za CCM kumbe kujadili umaskini unaolikumba taifa hili. Boti limeshatoboka watachota maji hadi wakome!!!!!!!!!!
 
Watz wengi mno wanamuamini. Watu wa magamba tu ndiyo wanamuona hafai, mchochezi, hutaka kumfungia gazeti, hutaka kumpofua macho etc. Katika magazeti serious, lake laongoza kwa mauzo hapa nchini. Usibishe.

Mkuu Counter Punch hilo suala nimeliekeza kwa Wale Amabo huwa hawamwamini Kubenea lakini naona leo wamekimbilia Kutafuta Makala za Kubenea
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Butola, hata kikwete alinaswa na lowasa pasaka..swala tushajua wale vigogo sita ambao walikuwa wanatambiwa kuwa wapo ccj.,..sasa kama sio sita,mwakyembe nape n.k nitajie ni wakina nan hao vgogo 6?
 
Hapa ndio sasa pamefikia patamu!Maana watatajana sana tu!Lakini si inasemekana Porokwa yuko ile kambi ya wale wa siku 90 wenye hasira na akina Mwakyembe!Sasa mbona hakuna msemaji maalumu!
 
usiwe mvivu wa kuelewa

kinachozungumziwa hapa ni dhana ya unafiki na undumilakuwili kwa viongozi wetu ....period

Hapa hamna cha unafiki wala undumilakuwili! Huyo jamaa ni kundi la mapacha watatu na ametoka kule kwa Lowasa ndo maana ameamua kuwaponda kina Sitta.Nani asiyejua kuwa Sitta na wenzake wamepigwa vita sana ndani ya CCM mpaka ikafikia hatua ya kutaka kumfukuza? Ulitegemea asiwena wazo la kuchomoka ccm wakati anapigwa vita na maswahiba wa JK?

Mi sioni tatizo lolote kwa kina Sitta kwani hata wewe mwenyewe ungejaribu kuondoka.Huu mchezo mchafu ulioanzishwa na mapacha watatu umelenga kuwaokoa wao tu.Nawasapoti kina Sitta kwani wameonyesha uvumilivu wa hali ya juu kupambana na mafisadi ndani ya chama.Wasikatishwe tamaa na haya maneno ya watu waliokosa hoja! Sasa hivi watz wan hali ngumu ya maisha na migao ya umeme isiyokwisha hivyo tunahitaji ufumbuzi wa matatizo yetu!
 
Watanzania kweli wagumu kuelewa mambo rahisi kabisa! Tatizo hapa ndugu yangu Anfaal ni kwamba hao wa vyama vingine vyote ulivyotaja walikuwa open kabisa, hawakujifichaficha kama hawa wa CCJ, isipokuwa Mpendazoe tu. Kama Nape, Mwakyembe na Sitta walianzisha CCJ (kitu ambacho ni haki yao kikatiba) -- kwa nini wajifiche? Ni wanafiki tu!

lakini ndio siasa hiyo Mkuu, si kila kitu kinafanyika hadharani
 
Hapa hamna cha unafiki wala undumilakuwili! Huyo jamaa ni kundi la mapacha watatu na ametoka kule kwa Lowasa ndo maana ameamua kuwaponda kina Sitta.Nani asiyejua kuwa Sitta na wenzake wamepigwa vita sana ndani ya CCM mpaka ikafikia hatua ya kutaka kumfukuza? Ulitegemea asiwena wazo la kuchomoka ccm wakati anapigwa vita na maswahiba wa JK?

Mi sioni tatizo lolote kwa kina Sitta kwani hata wewe mwenyewe ungejaribu kuondoka.Huu mchezo mchafu ulioanzishwa na mapacha watatu umelenga kuwaokoa wao tu.Nawasapoti kina Sitta kwani wameonyesha uvumilivu wa hali ya juu kupambana na mafisadi ndani ya chama.Wasikatishwe tamaa na haya maneno ya watu waliokosa hoja! Sasa hivi watz wan hali ngumu ya maisha na migao ya umeme isiyokwisha hivyo tunahitaji ufumbuzi wa matatizo yetu!


Mkuu Matatizo ya Watanzania, Umeme, maji huduma Mbaya za kijamii na nyingine yamesababishwa na CCM na si Mapacha watatu. So juhudi zozote za CCM za kutaka kujitaka ( hata kuwatosa Mapacha watatu) ni Lazima Zilaaniwe. CCM should Die. CCM inapaswa Kufa na si Kuhuishwa
 
Hapa ndio sasa pamefikia patamu!Maana watatajana sana tu!Lakini si inasemekana Porokwa yuko ile kambi ya wale wa siku 90 wenye hasira na akina Mwakyembe!Sasa mbona hakuna msemaji maalumu!
Hata ka Porokwa yuko ile kambi ya 90 days hiyo haibadilishi mantiki kuwa six, nape na mwakyembe ni wanafiki wanaopigania matumbo yao kwa kigezo cha kutetea wanyonge kama walifikia stage ya kuiengineer uanzishwaji wa chama kingine ni wazi walioona CCM hakuwafai lkn still wako pale baada ya kuahidiwa vyeo this is big hypocrisy tushawajua wanafki wakubwa na wenye uchu wa madaraka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom