Haya ni mapenzi, uzinzi, uasherati au kitu gani?
Ni mara ya tatu kukutana na huu msala wa watu kubeba picha na video za ngono kwenye flash derives zao. Wa kwanza alikuwa kavulana fulani, nilikachimba mkwara nikakaambia nenda zako usirudie tena kubeba uchafu huo kwenye flash disk yako. Mwingine alikuwa ni mdada anafanyia kazi bank, nakumbuka alinitext "Hivi unanichukuliaje kunikuta nimebeba hizo picha?". Nilimjibu "utakuwa unatumia bundle kubwa sana, au tigo wanakupa bure nini, maana niliona picha zao pia!"
Wa tatu bosi wangu tena mwanamke. Issue iko hivi:
Laptop yangu nimeifanyia configuration kudetect malware (including porn videos and photos, kwa kutumia possible key words zinazoweza kuwepo kwenye source files, hapa kwa kawaida ni metadata au links zilikodownlodiwa), na ikidetect nimeiset kufungua folder lenye haya mavitu kwa kupoup, huku ikidispaly message:
"Wicked files detected, they are subject to deletion in few seconds, this decision is not negotiable and cannot be undone", hiyo ni warning message yangu.
Sasa siku moja asubuhi na mapema bosi wangu akaja anakimbiakimbia, namheshimu, dah "tafadhali naomba unisaidie kuna hizi data hapa nimehangaika nazo kweli, nataka kuzifanyia statistical analysis, ngoja nikuletee flash uhamishe na kufanyia kwenye laptop yako". Akanieleza kwa kifupi nimsaidie kuzifanya nini, halafu fasta kaenda ofisini kwake kuleta flash (ngo ngo ngo ...., kelele zilizofanywa na high heels zake).
Kuichomeka flash kwenye port hivi (sikutegemea kabisa kama huyu madam angebeba hayo madude kwenye flash), duh, OoOOOoOOOps! Folder limefunguka (amelipa jina "Personal Data") huku laptop ikidisplay hiyo message "Wicked files .....".
Madama "OOoohh jamani, hayo manini tena funga basi na wewe, jamani mambo mengine muangalie basi".
Mie nikajifanya niko busy na simu, mara bahati nzuri kuna jamaa kanipigia nikatoka nje kupokea, nikawa naongea halafu nazidi kusogea mbali na tulipokuwa (nilitaka niende mbali zaidi ili nikacheke). Kadri nilivyosogea mbali nilifunguka kwa kicheko, njiani nikakutana na jamaa yangu mwingine anakuja ofisini, nikampa mkanda kwa ufupi halafu naye akawa ancheka. Ikabidi nimwambie tafadhali tuliza mzuka maana utaua bendi. Jamaa alishindwa kabisa kuacha kucheka, ilibidi tusiende ofisini muda ule, tukaamua kwenda kutafuta breakfast kwanza kwenye mgahawa fulani upo karibu na sehemu ya kazi.
Nilirudi kwa kunyata, nikakuta laptop yangu imetolewa battery halafu wala haijarudihshiwa (atakuwa alishindwa kuizima, maana, nilivyokuwa nimeiset asingeweza kucancel au kuswitch off mpaka imalize kudelete).
Wakati nafikiria kwenda kumwuuliza secretary kama bosi yupo, bahati nzuri vuuuuuu, secretary kaingia ofisini kwetu "mmemfanya nini bosi mbona kakasirika hivi leo?". Nikamwuuliza yupo? Akaniambia kaondoka amesema kapata dharura, nikasema afadhali!
Ilikuwa Ijumaa iliyopita. Jumanne - kesho kutwa najua ataniita, na mie siku hiyo nitafika ofisini asubuhi sana ili kama atakuwa amefika tuyamalize kabisaa!
Nitamwambia hiyo flash yako usiwe unawapa watoto maana watoto wa siku hizi ni watundu sana wanaweza kujaza vitu ilimradi tu. Kuhusu ilivyopopup, nitamwambia kuna watu wamefanya uhuni wameiwekea flash software ili ukiichomeka kwenye usb port inafunguka automatically na kuiambia computer ifute baadhi ya mafaili!
Yaani majibu au kujitetea kwangu itakuwa ni full drama kutegemea na upepo na mood yake kuhusu hilo tukio.
Dunia ina mambo sikutegemea kabisa huyo mdada/madam kuwa na hizo movies kwenye flash. Kutokana na nilichokishuhudia juzi, jana niliamua kubadilisha signature yangu ya Jf na kutoa ujumbe kama unavyouona hapo chini.
Please Jf members "Say no to wicked things on your eyes!".