Pongezi zikufikie RC Paul Makonda

Rajabu Msechu

Member
Apr 13, 2016
35
18
Ahlan wa Sahlan wanafamilia ya jukwaa la siasa, pasipo kupoteza muda ningependa kumpa pongezi za dhati mkuu wa mkoa wetu Mh. Paul Makonda kwa jitihada zake anazozifanya kila uchwao ikiwa ni katika kuhakikisha mkoa wa Dar es salaam unakuwa na sifa nzuri na kuigwa.

Nikianza kabisa na suala zima la walimu kutolipa nauli kwenye mabasi, hili wazo alilolitoa kipindi akiwa RC ni wazo zuri na linafaa kabisa kuungwa mkono licha mpaka sasa utekelezaji wake haujaanza kushika hatamu, lakini nina amini kabisa itafika pahala jambo hili litafanikiwa.

Kingine ni suala zima la kuonyesha nia ya kuwaondoa wadadapoa na ombaomba mjini ambao wamekuwa ni kero kubwa hasa kwa wananchi, sipo hapa kuwabeza, lah! Bali nina amini hakuna nchi yeyote Dunia ambayo imehalalisha ombaomba au madada poa.

Kwa kumalizia ni motisha aliyotoa kwa Polisi ya kuwazawadia kiasi cha shilingi Milioni endapo watafanikiwa kuwakabili wahalifu wanaotumia silaha za moto yani nikimaanisha Majambazi, ingawa wazo lake hili limepingwa na watu wengi mmojawapo nikiwa mimi, bali naamini kwa maoni ya wananchi atalifanyia kazi suala hili.
 
Pongezi nyingi kwako mkuu wa mkoa wa DSM kutuondolea kirusi hiki, Kebwe! kijana mdogo lkn umekomaa kifikra, tunakuombea uongezewe ulinzi lkn pia Mwengezi MUNGU azidi kukubariki.
 
Bongo usipowajibika utasemwa, ukiwajibika utasemwa sana, anajipendekeza! Kuna jamaa hapa wanajisahau hadi wanasema na presida anajipendekeza (si ndio hiyo mnasema anataka sifa ).....Hongera sana DC Makonda, tupo tunaotambua juhudi zako!
 
Mmmhhhh......naogopa sana lakini RC YUKO SAHIHI. Kuhusu wakwepa kodi wa Kariakoo na wauza madawa RC kula nao sahani moja.
 
Bongo usipowajibika utasemwa, ukiwajibika utasemwa sana, anajipendekeza! kuna jamaa hapa wanajisahau hadi wanasema na presida anajipendekeza (si ndio hiyo mnasema anataka sifa ).....Hongera sana DC Makonda, tupo tunaotambua juhudi zako!
Mkuu katika jamii watu kama hao, hawakosekani.
 
Makonda anaweza kuwa kiongozi mzuri.
Bado hoja yangu inasimama kwenye kuanzisha mfumo ambao hautegemei kauli na matamko ya kiongozi.
Kuwa na nchi ambayo unategemea ubora wa kiongozi ni hatari sana.
Embu jiulize Kuna Amina Magufuli wangapi Tanzania?!
 
Ngoja tuendlee kuangalia utendaji wake , akiendlea hivi hivi basi 2025 tunampa mikoa yote tz.

Tulidanganyika sana na Lowasa, kumbe vijana wachapakazi wapo bhana. Mwingne mwenye kasi nzuri ni John Mongela.

Mh. JPM Nina mtihani mmoja nae tu sasahv, akiushinda basi mie kila uchwapo ntakua napiga magoti kumuombea kwa Mungu yaliyo mema, ila akilishindwa , ntamdharau na kumlaani daily. Ni juu ya ile tender ya mda mrefu kuliko zote tz, tender ya 2011 hadi Leo 2016. Malipo yamefanyika lkn kazi haijafanyika. Si nyingne ni ya LUGUMI na AFIS
 
Back
Top Bottom