Pongezi kwako Mwanasheria wa NEMC Bw. Mchali Heche

Pongezi kwako Mwanasheria wa NEMC Bw. Mchali Heche

Fede Masolwa

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2013
Posts
529
Reaction score
123
Mr huyu, namuona katika taarifa mbalimbali za habari, akifanya kazi yake kwa ufasaha na weledi katika kulinda mazingira Tz.

Amekuwa akifunga viwanda vingi vinavyokiuka sheria na taratibu za uendeshaji kimazingira nchini

Zaidi ni jasili sana katika maamuzi,nimemuona sasa ITV kwa issue ya kiwanda cha punda Dodoma kamkolomea mmiliki kiume.

Hongera sana kaka kwa kazi safi, na pongezi nyingi kwako...
 


Punda wanafungwa na wanaliwa kama mbuzi na ng'ombe, huyo bwana ana matatizo na wachina.
 
Anaitwa Manchale Heche ni kaka yake John Heche mgombea ubunge Tarime vijijini kwa tiketi ya chadema na alikuwa Luteni wa jeshi kwa kweli huyu jamaa anajitahidi sana katika kufanya kazi na kulinda mazingira ni baadhi ya vijana wachache wanaofanya kazi bila ya rushwa.
 
Sababu zinazotolewa eti nyama ya punda kimaadili haifai ndio sijajua anatumia sheria gani. Halafu kama fursa imekuja zamani ilikuwa haina soko hauoni wanyaturu na wagogo wanaofuga wanyama hao kwa wingi sasa watapata pa kuwauza hasa pale wanapozeeka?
 
Anaitwa Manchale Heche ni kaka yake John Heche mgombea ubunge Tarime vijijini kwa tiketi ya chadema na alikuwa Luteni wa jeshi kwa kweli huyu jamaa anajitahidi sana katika kufanya kazi na kulinda mazingira ni baadhi ya vijana wachache wanaofanya kazi bila ya rushwa.

Basi nimeelewa kwanini kazi yake iko kiweledi sanaa (Lutein), ana maamuzi magumu kwa wakati sahihi
 
Sababu zinazotolewa eti nyama ya punda kimaadili haifai ndio sijajua anatumia sheria gani. Halafu kama fursa imekuja zamani ilikuwa haina soko hauoni wanyaturu na wagogo wanaofuga wanyama hao kwa wingi sasa watapata pa kuwauza hasa pale wanapozeeka?

Tunaongelea uchinjaji wa punda mia mbili kwa siku. Sasa piga kwa wiki, mwezi na hatimaye mwaka
Tanzania hatuna ranchi za punda kwamba tunaweza kuwazalisha kwa ajili ya kuchinja, kile kiwanda ni kikubwa na ni uwekezaji wa muda mrefu
Punda wa Tanzania wanaingia kwenye kundi la endangered species, hawapo sehemu kubwa ya Tanzania, kuruhusu kiwanda cha namna hii bila maandalizi ni kuangamiza kizazi cha hawa wanyama

Hesabu ya tarakimu hii hapa kwa wastani tu wa siku tano za wiki mwezi na mwaka
200×5=1000
1000×5=5000
5000×4=20000
20000×12=240,000
240000×5=1,200,000
Je Tanzania ina punda wa kutosha kuweza kukidhi mahitaji ya hiki kiwanda na soko la china nchi yenye wakazi bilioni moja na zaidi?
Je takwimu na sensa za hawa wanyama zinasemaje?
Hakika jamaa hakukurupuka bali waliokurupuka ni wale walioidhinisha huu mradi kwa maslahi binafsi na rushwa pamoja na hawa hapa jamvini wanaopinga bila kutafakari
 
ni lieutenant sio Lutein au kiswahili andika luteni

Duh! umeona hapo tuu....ni dictionary ya sim imejimix.

Tazama kusudio la mada, acha ushamba....jeshini kuna vyeo vingi kuanzia juu kama jenerali, luteni jenerali, meja jenerali
brigedia jenerali, kanali, luteni Kanali, meja, kapteni, luteni (Lieutenant) , luteni usu.....au nikutajie na vyeo vya askar wa chini ya hapo.

Acha ushamba wa mude, jikite kwenye hoja.
 
Naomba mwenye mawasiliano ya hao wafanyabiashara wa punda, nitawanunua na kuwasafirisha hadi tanga tutawaweka kwenye jahazi hadi comoro, tutawachinja na kuwauza china. Kesho naenda TIC nipate mawasiliano ya hao wachina tukajenge kiwanda Comoro, hii nchi ya ajabu sana.

Mtu kaleta fursa za kibiashara mnaanza roho mbaya. Hebu TDFA watwambie nyama gani inaruhusiwa kuliwa na kwa nini? Heche atuambie Tanzania ina punda wangapi na itachukua muda gani punda kuisha wote nchini? hao punda miambili kwa siku wakowapi? kwenye tv tunaona punda wasiozidi kumi na mifupa ya punda wasiozidi ishirini.

Hii nchi inahitaji watu kama magufuli ndo tutashikishana adabu.
 
Tunaongelea uchinjaji wa punda mia mbili kwa siku. Sasa piga kwa wiki, mwezi na hatimaye mwaka
Tanzania hatuna ranchi za punda kwamba tunaweza kuwazalisha kwa ajili ya kuchinja, kile kiwanda ni kikubwa na ni uwekezaji wa muda mrefu
Punda wa Tanzania wanaingia kwenye kundi la endangered species, hawapo sehemu kubwa ya Tanzania, kuruhusu kiwanda cha namna hii bila maandalizi ni kuangamiza kizazi cha hawa wanyama

Hesabu ya tarakimu hii hapa kwa wastani tu wa siku tano za wiki mwezi na mwaka
200×5=1000
1000×5=5000
5000×4=20000
20000×12=240,000
240000×5=1,200,000
Je Tanzania ina punda wa kutosha kuweza kukidhi mahitaji ya hiki kiwanda na soko la china nchi yenye wakazi bilioni moja na zaidi?
Je takwimu na sensa za hawa wanyama zinasemaje?
Hakika jamaa hakukurupuka bali waliokurupuka ni wale walioidhinisha huu mradi kwa maslahi binafsi na rushwa pamoja na hawa hapa jamvini wanaopinga bila kutafakari
Hayo mahesabu hayana mashiko!! ukumbuke kuwa sii kila mtu anafuga punda kwa sasa, hivyo kama soko la uhakika la wanyama hao nitapatikana basi kila mtu atashawishika kuwafuga na idadi yake itaonezeka. Mbona watu baada ya kuganganywa na wakenya kuwa ufugaji wa kware ni dili mbona kwa kipindi kifupi ndege hao wa porinui ambao hawakuzoeleka kufugwa sasa hivi wameongezeka? Najua sababu kubwa si kwamba ni za kupotea kwa wanyama hao bali ni kule kuwa "obsessed" na imani kwamba kwa utamaduni wake au dini yake wanyama hao hawaliki. Kama wewe hauli waache wenzako wanaoona obora wake wakupe faranga wao wakatafune. Hizi mila zetu ndio zimetuletea umaskini. Wachina wanakula vile mnavyo vishangaa ninyi kumbe kuna siri imejificha kwenye vyakula hivyo ndio maana wanakuwa na akili nyingi , kuishi miaka mingi na kutokuugua hovyo. Watu watumie fursa wafuge punda kwa wingi umaskini ndio bye bye kupitia punda.
 
Back
Top Bottom