Pombe zinazouzwa kiholela mtaani na madukani zinawamaliza vijana, mamlaka chukueni hatua za haraka

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
Licha ya Sheria ya Vileo Sura ya 77 ya Mapitio ya Sheria za Tanzania ya Mwaka 2002 kuelekeza taratibu mbalimbali za kufanyabiashara ya vileo, lakini kwa siku za hivi karibuni kuna viashiria na mazingira ambayo yanaonekana kwenda kinyume mwongozo huo hali ambayo inaacha tafakuri.

Miaka kadhaa iliyopita Serikali ilipiga marufuku matumizi ya pombe za kwenye viroba maarufu kwa jina la 'viroba', pombe hizo zilikuwa zikiuzwa kiholela hali ambayo ilikuwa inaweka hatarini nguvu kazi za Taifa kupitia watumiaji, hata Wanafunzi baadhi ya walidaiwa kutumia pombe hiyo kwa kuwa ilikuwa inapatikana katika mazingira rahisi.

Ni miaka sasa imepita tokea zuio hilo litolewe, lakini hivi karibuni kumeibuka pombe nyingi ambazo zinazalishwa na kuwekwa kwenye chupa ndogo za plastiki, mfano double Kick, Smart Gin, Black Gin…

Pombe hizo zinauzwa kiholela mtaani ambapo asilimia kubwa kwenye Jiji la Dar es Salaam, wafanyabiashara wengi wa bidhaa za kila siku za matumizi ya nyumbani za rejareja ni nadra kuwakuta hawauzi pombe hizo.

Kwenye maeneo mengine hasa yenye mikusanyiko na sehemu za vijiwe baadhi ya vibada vimejengwa na vinauza pombe ya aina hiyo muda wote bila kuzingatia muda na taratibu nyingine zinazotokana miongozo.

Madhara ya kuuza pombe hizi bila utaratibu ni makubwa hasa kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa, kuna vijana wanaanza kunywa pombe hizo asubuhi na mapema na kushinda vijiweni hali ambayo mbeleni kama haitatafutiwa ufumbuzi ikaja kuzalisha wahalifu wengi mtaani kutokana na uteja wa pombe hizo bila kufanya kazi.

Pia kuuzwa kwa pombe hizo kiholela hasa kwenye maduka ya huduma za kijamii za kila siku inaweka uwezekano kwa Watoto au wanafunzi kujihusisha na matumizi ya pombe mapema, ikiwa ni kutokana na pombe hizo kupatikana kwa wepesi muda wote.

Ni muhimu mamlaka husika zikafatilia na kufanya uchambuzi wa kina kubaini athari zinazotokana na suala hilo, pombe hizo kwa sasa imekuwa sawa na viroba vilivyobadilishiwa vifungashio.

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Ninapoishi mimi kwa nyuma kuna bimdashi anauza hizi vitu yaani full kero na walevi wake kuanzia asubuhi hadi night. Polisi wenyewe wanawekwaga mfukoni wanapozwa wanaachia harakati zinaendelea kwahiyo raia unachagua uhame ilo eneo au uwavumilie.
 
Inaumiza sana hasa kwa wazazi ila ndo ivo serikali kwao zina faida wanatarajia business zikue
 
Kufa kufaana kuna mjuba huko Babati anamiliki kiwanda cha kutengeneza baadhi ya aina hizo za vinywaji vya bei rahisi kajenga Bungalow hatari sana. Huyo jamaa akiona hii post yako atakuchukia atakuona mnaa flani.
 
Kinachoua vijana ni ukosefu wa ajira, pombe ni matokeo ya vijana kukosa mwelekeo

Kama umesoma na umetumia elimu yako kuwaza hivi, basi hujasaidika

Kama vijana wanaoharibika mtaani ni pamoja na wale wenye kazi maalum basi naomba npate hukum chapchap apa jf.
 
Watoto wadogo wa umri wa sekondari wamekua wahanga wakubwa Sana wa hivi vipombe vya kwenye vichupa vidogo, akiwa hana hela ya kununua kichupa kizima anapimiwa nusu, wazazi ongezeni uangalizi kwa watoto wenu msitegemee serikali kuchukua hatua yoyote kwenye hili hii haigusi familia zao wenye mamlaka wanachojali ni maokoto ya Kodi tu.
 
Ni kweli kabisa. Hapa Kimara Korogwe vibanda vinauza pombe kali pamoja na bia saa za usiku hadi mapema asubuhi. Yaani hiyo sheria ni kama haipo.

Yote haya na uoza mwingine ni matokeo ya serikali mbovu ambayo imelala na inafanya kazi kwa mtindo wa "bora liende." Sidhani viongozi wanafahamu hata kama sheria.ya namna hiyo ipo. Inasikitisha. Kazi kubwa wanayoiweza ni ile ya kudhibiti upinzani kinyume na sheria na Katiba ya nchi.
 
Kufa kufaana kuna mjuba huko Babati anamiliki kiwanda cha kutengeneza baadhi ya aina hizo za vinywaji vya bei rahisi kajenga Bungalow hatari sana. Huyo jamaa akiona hii post yako atakuchukia atakuona mnaa flani.
Hata yule Bilionea wa Moshi pia mishe zake si kuuza izo pombe chafu juzi kati alipewa tuzo ya mlipa kodi bora
 
Kinachoua vijana ni ukosefu wa ajira, pombe ni matokeo ya vijana kukosa mwelekeo

Kama umesoma na umetumia elimu yako kuwaza hivi, basi hujasaidika

Kama vijana wanaoharibika mtaani ni pamoja na wale wenye kazi maalum basi naomba np
hapchap apa

Kinachoua vijana ni ukosefu wa ajira, pombe ni matokeo ya vijana kukosa mwelekeo

Kama umesoma na umetumia elimu yako kuwaza hivi, basi hujasaidika

Kama vijana wanaoharibika mtaani ni pamoja na wale wenye kazi maalum basi naomba npate hukum chapchap apa jf.
Hakuna Nchi duniani kila mtu anaweza kuwa na kazi Maalum....Sheria kama zipo zisimamiwe kuokoa vijana esp Wanafunz
 
Licha ya Sheria ya Vileo Sura ya 77 ya Mapitio ya Sheria za Tanzania ya Mwaka 2002 kuelekeza taratibu mbalimbali za kufanyabiashara ya vileo, lakini kwa siku za hivi karibuni kuna viashiria na mazingira ambayo yanaonekana kwenda kinyume mwongozo huo hali ambayo inaacha tafakuri.

Miaka kadhaa iliyopita Serikali ilipiga marufuku matumizi ya pombe za kwenye viroba maarufu kwa jina la 'viroba', pombe hizo zilikuwa zikiuzwa kiholela hali ambayo ilikuwa inaweka hatarini nguvu kazi za Taifa kupitia watumiaji, hata Wanafunzi baadhi ya walidaiwa kutumia pombe hiyo kwa kuwa ilikuwa inapatikana katika mazingira rahisi.

Ni miaka sasa imepita tokea zuio hilo litolewe, lakini hivi karibuni kumeibuka pombe nyingi ambazo zinazalishwa na kuwekwa kwenye chupa ndogo za plastiki, mfano double Kick, Smart Gin, Black Gin…

Pombe hizo zinauzwa kiholela mtaani ambapo asilimia kubwa kwenye Jiji la Dar es Salaam, wafanyabiashara wengi wa bidhaa za kila siku za matumizi ya nyumbani za rejareja ni nadra kuwakuta hawauzi pombe hizo.

Kwenye maeneo mengine hasa yenye mikusanyiko na sehemu za vijiwe baadhi ya vibada vimejengwa na vinauza pombe ya aina hiyo muda wote bila kuzingatia muda na taratibu nyingine zinazotokana miongozo.

Madhara ya kuuza pombe hizi bila utaratibu ni makubwa hasa kwa vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa, kuna vijana wanaanza kunywa pombe hizo asubuhi na mapema na kushinda vijiweni hali ambayo mbeleni kama haitatafutiwa ufumbuzi ikaja kuzalisha wahalifu wengi mtaani kutokana na uteja wa pombe hizo bila kufanya kazi.

Pia kuuzwa kwa pombe hizo kiholela hasa kwenye maduka ya huduma za kijamii za kila siku inaweka uwezekano kwa Watoto au wanafunzi kujihusisha na matumizi ya pombe mapema, ikiwa ni kutokana na pombe hizo kupatikana kwa wepesi muda wote.

Ni muhimu mamlaka husika zikafatilia na kufanya uchambuzi wa kina kubaini athari zinazotokana na suala hilo, pombe hizo kwa sasa imekuwa sawa na viroba vilivyobadilishiwa vifungashio.

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
Kunywa wanywe wao kwa starehe zao kama wewe unavyo paramia ma dada poa sasa mbona unawaonea wivu wenzio tena
 
Back
Top Bottom