Pombe imekuletea madhara gani maishani mwako?

Pombe imekuletea madhara gani maishani mwako?

Inakera sana pale unaporudi nyumbani, upo vyombo...unalala na mwenzako kila ukicheua inakuwa Kama gari ya pombe imepata ajali kitandani kwenu.......inaumiza sana.
 
Ninafanya online rehab. Kwa wale warahibu wenzangu wa gambe/kilaji/mtungi/kitwanga/mambo/vitu/smart phone/ulabu na majina mengine..ni lazima Tuwe wakweli kuwa pamoja na vifaida vichache vya pombe, madhara ni mengi zaidi.

Kwangu Mimi, imenimalizia pesa, magomvi na watu wa karibu, imeyumbisha ndoa, ajali za Mara kwa Mara, na uzembe usio na msingi.

Kwako wewe mwenzangu, Hebu funguka... Pombe imekuletea madhara gani maishani???
#naachapombe
ukianzisha hiyo Rehab unishtue. kuna jamaa kanipa kitabu nimuuzie.
Capt.PNG
 
mi ninampango wa kuacha pombe na nimekuwa sober for 2months. ila ninadoubt kama ntaweza kuresist ulanzi wa baridi.
Kiongozi, pombe haiachiki kwa Miezi... Mimi nimeshakaa mbali na pombe kwa zaidi ya mwaka ila.........
 
Nina mwaka na miezi mitano tangu nionje tone la pombe na natumaini kuwa sitairudia tena. Kakitambi ka bia ilikoniachia bado napambana nako kishujaa gym na mabarabarani kupiga mbio na naelekea kukatokomeza kabisa. Pombe haina faida!
 
Kiongozi, pombe haiachiki kwa Miezi... Mimi nimeshakaa mbali na pombe kwa zaidi ya mwaka ila.........
ndiyo maana nimesema mpango. ila ninahisi kwamba safari hii nitafanikiwa. tatizo langu nililikuta kwenye kitabu hiki.

2. aina ya pili ya kutawaliwa na pombe ni kushindwa kujizuia. Watu wa aina hii wakishaanza kunywa ni vigumu kuacha mpaka wawe wamezima au wameishiwa hela. Hii inaweza pelekea kusababisha kifo. Sababu kadri unavyokunywa sana ndio unajisahau kwamba unapitiliza kipimo. Watu wengi wa aina hii hufa kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi na kushindwa kupumua.
 
ndiyo maana nimesema mpango. ila ninahisi kwamba safari ntafanikiwa. tatizo langu nililikuta kwenye kitabu hiki.
2. aina ya pili ya kutawaliwa na pombe ni kushindwa kujizuia. Watu wa aina hii wakishaanza kunywa ni vigumu kuacha mpaka wawe wamezima au wameishiwa hela. Hii inaweza pelekea kusababisha kifo. Sababu kadri unavyokunywa sana ndio unajisahau kwamba unapitiliza kipimo. Watu wengi wa aina hii hufa kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi na kushindwa kupumua.
Bwashe, Mimi naacha pombe.
 
Pombe na pombe huez linganisha utamu wa grants na kiroba .....au hennesy na value .....pombe inamadhara kwenye ini inasababisha ini kusinyaa na kupoteza uwezo wa kufanya kazi zake katika mwili .......lakini ni by chance sio kila mlevi hupata
Pombe ukinywa kias unaenjoy Ila inayumbisha mfuko ukiiendekeza ....... sasa kama unahisi inakupumzikia acha ila kama mipango inaenda vyema meza kwa kiasi
 
Bwashe, Mimi naacha pombe.
kila la heri mkuu. pombe ukishindwa kucontrol inaharibu quality ya maisha. mi imenishinda, nakunywaga hadi kunakucha. naona njia pekee ni kuacha. chukua na kitabu kukusaidie.

1. tafuta kinywaji mbadala wa pombe kama vile chai au kahawa.

2.tafuta vitu mbadala vya kufanya kwa wakati ambao unakuwa unakunywa pombe kama vile kusoma vitabu, kuangalia filamu, kushiriki katika michezo au mazoezi.
3.tumia pesa ambazo unaziokoa kutoka kwenye pombe kwa kujiburudisha kama vile kula vizuri au kununua vifaa vya nyumbani. Hii itakusaidia sana katika kuona umuhimu wa kuacha pombe.

4.jiwekee mkakati kabla ya kwenda kunywa kuhusu kiasi utakachoenda kunywa na pesa utakayotumia. Usibebe pesa zaidi ya uliyopanga kutumia.
5. tumia glasi ndogo wakati wa kunywa na tumia vinywaji vyenye nguvu ndogo. Utafiti unaonyesha watu hunywa zaidi wakitumia glasi kubwa kuliko wakitumia glasi ndogo.

6.kunywa maji kabla hujaanza kunywa pombe. na unavyokuwa unakunywa pombe hakikisha unakuwa na maji ya kunywa karibu na uyatumie mara kwa mara.
7.jaribu kuepuka vishawishi vya kunywa. Watu wengi huwa tunashawishika kunywa kwenye mazingira fulani au tukiwa na watu fulani. Unachotakiwa ni kugundua ni vishawishi vipi hukufanya unywe na uanze kuviepuka.

8.kuwa na msimamo. Watu wengi ambao hujaribu kuacha pombe hukutana na wakati mgumu wanapopata ofa toka kwa marafiki. Njia sahihi ni kukataa bila kusitasita. Kusitasita kunaweza kukufanya uteteleke katika msimamo wako. Ni vizuri ukatafuta sababu ya kukataa ofa mapema kabla hata ya

kukutana na ofa. Mfano, unaweza ukasema sinywi au siongezi pombe nyingine kwa sababu nataka kupunguza uzito au sababu nyingine ambayo utakuwa umeitengeneza kama ulinzi wako.

9.epuka kunywa pombe ukiwa na kiu au njaa. Hii inapunguza kiasi cha pombe ambacho kitaingia kwenye damu hivyo utapunguza madhara yake. Pia inasaidia kupunguza kasi ya mtu kuwa mraibu/teja wa pombe.

10.hakikisha ndugu na marafiki wanajua kwamba umedhamiria kuacha pombe. hii itasaidia kupata msaada kutoka kwao pia hawatakuwa wanakushawishi sana unywe. Pia hili linaweza kukusaidia kupata marafiki wapya kwani changamoto mojawapo ya kuacha pombe ni kupoteza marafiki.
11. kama unakunywa kwa kutumia glasi hakikisha kinywaji kimeisha kabisa ndo uongeze tena. Hii itakusaidia kujua ni kiasi gani cha pombe ulichotumia.

Kuna watu ambao mbinu hizo hapo juu zimeshindwa kabisa kuwasaidia kuacha pombe. msaada pekee ambao hubaki kwa watu hao ni kutumia dawa. Mara nyingi watu hawa ni wale ambao wanakuwa wametawaliwa sana na pombe na hupata madhara mara waachapo. Matibabu ya watu hawa hufuata hatua tatu muhimu.
 
Mkuu hongera... Mungu akufanikishe.
Ni vita mkuu. Ilifika wakati napiga bia moja inaitwa Dogfish 90 (abv 9%) mpaka sita namaliza peke yangu. Bia moja inauzwa $3.99. Halafu kila siku lazima nipate. Kuja kugundua suruali zote zinabana na matundu ya mkanda wa kiunoni yanazidi kuongezeka. Mateso ya gym na vumbi la barabarani nikikimbia kama mwehu aisee nimekoma. Yaani mtu unaweza kuchakaa, kunenepeana na kujiletea magonjwa kibao (BP, Diabetes, moyo) kwa sababu za kijinga. Hata Dr. wangu amefurahi sana!
 
Ni vita mkuu. Ilifika wakati napiga bia moja inaitwa Dogfish 90 (abv 9%) mpaka sita namaliza peke yangu. Bia moja inauzwa $3.99. Halafu kila siku lazima nipate. Kuja kugundua suruali zote zinabana na matundu ya mkanda wa kiunoni yanazidi kuongezeka. Mateso ya gym na vumbi la barabarani nikikimbia kama mwehu aisee nimekoma. Yaani mtu unaweza kuchakaa, kunenepeana na kujiletea magonjwa kibao (BP, Diabetes, moyo) kwa sababu za kijinga. Hata Dr. wangu amefurahi sana!
inabidi bongo tungeanzisha Alcoholic Anonymous (AA) kupeana mauzoefu ya kushinda pombe.
 
Yn i wish lijitu fulan lije lione ...hovyo kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom