Genekai
R I P
- Feb 9, 2010
- 12,514
- 5,003
huu ni upuuzi, watz ni watu wa aman
Amani au woga?
huu ni upuuzi, watz ni watu wa aman
mkuu, hilo si jibu la matatizo yaliyopo hapa nchini. serikali ibaki kati na isiegemee upande wowote
Twaweza pata wapi hz CD na DVD?
wakati MOU inasainiwa mwaka 1992, nchi ilikuwa inafuata mfumo wa chama kimoja. kumbuka pia nafasi karibu zote nyeti zilishikwa na wakristo ukiachilia mbali nafasi ya urais ambayo ilikuwa chini ya mzee ruksa. hivyo kila kitu yeye alikubali tu na ndo maana hayati nyerere alimwachia nchi kwa vile alimwona ni dhaifu hivyo hataweza kupinga maamuzi ya kanisa
kikwete amekata mirija ya MOU na ndo maana maaskofu wamemchukia. wamefuta pia na ile kauli yao kuwa kikwete ni chaguo la mungu na askofu kilaini aliyetamka maneno hayo katupwa huko bukoba na ameambiwa asitokee kwenye media kuongea chochote
Gazeti linaeleza CD zinapatikana Buguruni_Chama. Ila sijui hilo neno Chama linasimama badala ya chama gani.
Zambia Rais sata alisema yeye ataongoza nchi kwa kutumia amri za Mungu.Ukianza na mungu utamaliza na Mungu
moto umetapakaa dunia nzima utauzimaje?kama hata hao wenye nguvu hawawezi kuuzima.vitu vingine viko organised na mtu kama wewe is just a tool to reach the agenda.mkuu kama hawataki kukemea tufanyeje, wamebaki kutoa matamko yaliyojaa taarabu tu....
kama vipi huu moto tuuzime kwa damu zetu kabla hawajaliza mda wao
mwinyi si muislam kasema kila mtu achinje na ale kile anachotaka ,tena lhaji kabisa!!sioni sababu yakugombea kuchinja wanalao jambo
exactly dini inayoua kwa makombora kutoka kwenye ndege za kisasa na aircraft carrier ndo ya haki.Mungu kwa maksudi aliacha dini safi na ya kishetani zishindane lakini dini ya haki itajulikana mwishoni
kikubwa tu huyo alie toa hizo mikanda kama ni kweli anatakia kuhojiwa anamanisha nini kwa maneno yakeSOURCE: JIBU LA MAISHA
DATE: Sunday, May 12, 2013
ISSN: 1821-6463, No. 241
PAGE: 115
HEADLINE: ASKOFU PENGO AZIDI KUTISHIWA
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Kwa matoleo kadhaa ya nyuma tumeripoti matukio ya kichochezi ya kusambazwa kwa CD na DVD zinazochochea utengano baina ya wakristo na waislamu nchini. Tumefanya hivyo kwa tahadhari kubwa na hata wakati mwingine kujitahidi kujiepusha na kuchapisha habari hizo.
Hata hivyo, tunalazimika kuripoti matukio haya ili kuzikumbusha mamlaka zenye dhamana zichukue hatua kali dhidi ya makundi haya ambayo yanaonekana moja kwa moja ni maadui wa umoja wa watanzania.
Katika kile kinachoonekana nia utaratibu maalumu, imetolewa CD mpya iliyopewa jina Ndege wote walie akilia bundi uchuro ambay pamoja na mambo mengine inaonyesha picha ya Askofu Kardinal Polycarp Pengo ikiwa na maandishi yanayosomeka WANTED ikiambatana na maneno makali ya kulaani Kanisa Katoliki na hata mengine, huku picha ya mtu anayechinjwa ikitumika kama logo inayojirejea kila wakati.
Juhudi za kumpata mtu anayeonekana katika DVD hiyo akitajwa kama Imam Hamza Omary, ili kufafanua ujumbe uliopo ndani ya mkanda huo hazikfanikiwa.
DVD hiyo ambayo JIBU LA MAISHA lina nakala yake inaonyesha mhadhiri akinukuu aya za Kuran na kuwaalika wenzake kwenye kile alichokiita Jihad (baadhi ya yale yanayosemwa hatuwezi kuyaandika kutokana na sababu za kimaadili)
Katika hilo Imam Omary anasema serikali imekuwa ikiegemea upande wa maaskofu na mabaraza yake, lakini si kwa waislamu.
Mkanda huo umeonyesha baadhi ya mazoezi makali ya vijana wa Kiislamu ingawa haionyeshi yanafanyika wapi.
Mhubiri huyo aliyashutumu pia mataifa ya kimagharibi akidai yamekuwa yakitoa silaha na kuwagombanisha wao kwa wao pasipo wenyewe kujua na hilo limeonekana kwa Saddam Hussein.
Aidha alionekana akidai kuwa jambo kubwa na la hatari kwa waislam wa sasa ni kutoongelea kabisa suala la Jihad, na hilo limekuwa donda ndugu.
Bila kupepesa maneno, Imam huyo alitaja viongozi ambao alidai eti wamekuwa wakibadili yale waliyokubaliana na waislam na wamekwenda kinyume kutokana na kutiwa msukosuko.
Vingozi na wasaniasa wanaotajwa katika DVD hiyo ni pamoja na Waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe, Katibu Mstaafu wa CCM, Yusufu Makamba, na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Alipomaliza hilo alimgeukiwa Rais wa Uganda, Museveni na kudai yeye ni kiongozi wa Afrika Mashariki anayetaka kuhakikisha anaungoa uislam kupitia mashehe kwa juhudi zote.
Aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow, anatajwa kwenye mkanda huo, lakini JIBU LA MAISHA halitaongelea kilichoongelewa humo.
Yusuf Makamba ambaye ni muislam, wanadai naye mwaka 1998 akiwa Mkuu wa Mkoa Dar, wakati wao wakisema nchi inatawaliwa kwa mfumo Kristo, yeye alipinga na hilo likaonekana kuwa yuko kinyume na uislam.
Mwinjilisti Cecil Simbaulanga ambaye amekuwa akipita huku na kule kutetea wakristo ili wajue haki zao anatajwa kuwasisitiza wakristo kuchinja nyama wakati inajulikana siku zote kwamba waislamu ndiyo wenye kufanya jambo hilo hapa Tanzania.
.
Wakati hayo yakitokea, tukio la kurushwa bomu katika Kanisa la Parish of St. Joseph the Worker (Olasiti), mkoani Arusha, linarandana na maudhui ya kile kinachoelezwa kwenye mikanda kadhaa inayotolewa na watu wanaoaminika kuwa na imani kali ikionyesha chuki ya wazi dhidi na kanisa hilo.
Ndani ya DVD kadhaa zenye mlengo mmoja ambazo zimezagaa maeneo kadhaa jijini Dar, hasa maeneo ya Buguruni_Chama, inaelezwa kukamatwa kukamatwa kwa maaskofu ili kuwachinja ikiwa muislam atafanyiwa ubaya wowote au kuuliwa.
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Mungu kwa maksudi aliacha dini safi na ya kishetani zishindane lakini dini ya haki itajulikana mwishoni
exactly dini inayoua kwa makombora kutoka kwenye ndege za kisasa na aircraft carrier ndo ya haki.
Kwa ufupi mkuu huo mwisho utausubiri sana tu.wajukuu wako watapita na kuja wajukuu za wajukuu zako na bado utakua ukisubiri.