Polisi watanda kwa Mo Dewji

Polisi watanda kwa Mo Dewji

Badala ya kutanda kwa majambazi wao unasema wametanda kwa Mo.
Sijaelewa
 
Serikali Iko Macho
Inawajari Wananchi Wake Sana
Serikali Sikivu Ni Hii Hii Tuliyonayo
Anayebisha Ni Mbishi Sana Na Hatutamuelewa
 
Sio kwamba mijamaa umevarishwa magwanda ili mission izidii kukamilika ?
 
Wanaangalia anaongea na nani kulinda siri yao, maana walioongea au kukutana naye baada ya kuachiwa nao wamejikuta wanaitwa kuhojiwa, ' kawaambia nini'?
 
Baada ya sakata la kutekwa kwa mfanyabishara maarufu nchini, Mohammed Dewji Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limemuongezea ulinzi mfanyabiashara huyo
View attachment 910312
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa katika mahojiano yake na www.eatv.tv amesema kuwa wamemwongezea ulinzi mfanyabiashara huyo katika kipindi hiki ambacho bado wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio.

"Katika kipindi hiki ambacho bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio la kutekwa kwake, tumemuongezea ulinzi", amesema Mambosasa.

Mo Dewji alitekwa Alfajiri ya Oktoba 11, katika hoteli ya Colosseum iliyopo Osterbay jijini Dar es salaam na kupatikana baada ya siku tisa katika maeneo ya Gymkhana alikotelekezwa na watekaji, huku pia wakitelekeza gari aina ya Toyota Surf walilolitumia likiwa na silaha kadhaa za moto.
Asije tu akapotea tukaambiwa amepotelea ndani alilokuwemo!
 
wenzetu huwa wanatrain vijana wenye sifa kufanya kazi zisizo hitaji kutekelezwa kimakosa sisi tunatrain watu wasio na sifa kufanya kazi makini ndo maana jeshi letu la polisi litabaki bora tu kulinda na kuiba masanduku ya kura!
 
Na ukumbuke kwamba tarehe kama leo ndio mlimchagua Jiwe kuwa mwenye nchi. Mlimtaka wenyewe
Serikali Iko Macho
Inawajari Wananchi Wake Sana
Serikali Sikivu Ni Hii Hii Tuliyonayo
Anayebisha Ni Mbishi Sana Na Hatutamuelewa
 
Mbona roma hawakumuwekea ulinzi baada ya kutekwa
Au ndo matumizi ya 1bilion
 
Wanazuia asihojiwe na waandishi wa habari
 
watakuwa wanaulinda mdomo wake ili ubaki uko closed! usije ukafunguka!
 
I think there are lots of dots ambayo watanzania tukijua itakuwa shida..
Let's the police take control of the enviroment
 
Back
Top Bottom