Polisi wa barabarani na weledi wao.

Infopaedia

JF-Expert Member
Oct 28, 2011
1,231
1,487
Screenshot_20230220-101701~2.png

Habari zenu wana jamii. Leo nimeona tuongeee kidogo kuhusu hawa askari wetu wa úsalama barabarani.

Ukiangalia hicho kiambatanisho hapo juu, hilo ni Kosa la barabarani ambalo askari amemuandikia dereva. Japo kuwa hilo Kosa inaonekana ni la kujitungia tu, lakini shaka yangu si juu ya hilo. Kinachonisikitisha ni weledi na namna ya kufikiri ya huyu askari wa barabarani. Kumbuka huyu amepewa dhamana ya kusimamia sheria za barabarani na kutupunguzia kero watumiaji wa hizi barabara.

Kwa kichwa cha huyu askari, hakuna msaada wowote ama tija kwetu sisi au wateja wake. Ameandika kwamba Kosa ni "kushindwa kufunga mkanda wa úsalama" au "kushindwa kuvaa kofia ya úsalama". Hapa sijui wana jamii mnaelewa nini. Yawezekana mimi ni huu uzee ndio unanifanya nisielewe.

Hayo makosa yana asili ya gari na pikipiki na haiwezekani mtu kuwa na gari na kufanya hayo makosa mawili. Ni wazi aliamuwa kutunga tu. Nina uhakika anajua haya ni makosa ya vyombo viwili tofauti, lakini bado akaamuwa kuandika. Hapo ndipo ninapotia mashaka sana juu ya jeshi letu la police.

Kama nilivyosema awali, kwa police kuamua tu kutunga Kosa hainisikitishi sana. Kinachotia hofu na simanzi ni weledi na mawazo ya huyu askari wakati anaandika hili Kosa na adhabu yake. Aliandika akijua si kweli lakini anaamini huyu mtanzania atalipa tu.

Kama ni hivyo ndugu zangu, kuna shida kubwa katikati ya hili jeshi letu la úsalama barabarani. Shida ya kimfumo, weledi, na maadili. Kuna haja ya kuliangalia upya hili jeshi. Jeshi haliwezi kupata ama kuwa na tija iwayoyote kutoka kwa askari wenye mtazamo na akili kama hizi.

Watanzania wengi hatupendi usumbufu, kwa tabia yetu hiyo police kama hawa na wengine wengi huamua kututumia, ama kwa faida yao au kwa ujinga tu na kuridhisha kiburi chao.

Binafsi katika pilika zangu za kusaka tonge, huwa natumia muda mwingi nikiwa na raia wa kigeni. Ninapokutana na maafisa wa serekali nikiwa na hawa raia wa nje, huwa naipata wakati mgumu sana kuanzia kuitetea serekali yetu kwa hawa wageni. Yaani ni lazima mtu wa serekali afanye kituko cha kipumbavu tu. Huwa sependi kukubali serekali yetu ionekane ya kijinga kwa wageni.

Basi naanza kujitutumua na kiingereza changu cha kuungaunga. Jamani mnatuchosha sana.

Kwa Kosa kama hilo hapo juu naanzaje kulitetea jeshi letu!!! Hapo pana tatizo kubwa la kimfumo, weledi, na maadili.

Lakini endapo atatokea kiongozi wa jeshi kuelezea hilo Kosa, a naweza akaja na maelezo mepesi sana kiasi kwamba unaweza dhani muandishi wa hiyo fine na huyo kiongozi wa jeshi, ni mtu mmoja.

Wakatabahu
Infopaedia
 
Sasa kama askari yule wa kesi mboe alikua hajui hata muongozo wa kipolisi unasemaje na bado akapandishwa cheo unadhani hawa wengine watakuaje
 
Mkuu unaelewa maana ya 'or' na 'and'?

Hayaendi pamoja hayo mkuu. Futa huu uzi kutunza heshima yako

Na pia mkuu unasahau kuwa hayo makosa na namna ya kuyaandika ni tayari yako set. Traffic police anaselect na drop arrow tu. Unamuonea tu kusema hana weledi jinsi alivyoandika
 
Mbona maelezo yanaeleweka ,maana apo imewekwa kwenye kundi moja ,kumaanisha ,kosa la kutofunga mkanda faini yake ni hiyo ,pia kosa la kutovaa kofia ngumu faini yako ni hiyo hiyo.au Mimi ndio sijaelewa
 
Kuna kukariri na kuelewa. ..alitakiwa atofautishe kua kwakua huyu dareva anaendesha gari basi maelezo yahusu gari na si pikipiki.
Kingine inaweza kua majibu yamejazwa tayari kwenye ile mashine anayoprint risit hivyo yeye anachagua namba kutokana na kosa ilayeye hajazi maelezo yyt
 
Kwenye kijitabu cha mwongizo kinachoonyesha makosa mbalimbali hayo makosa mawili yameandikwa sehemu moja kuonyesha ya gharama sawa ya faini. Sasa yeye amevopy yote mawili kama yalivyo akambambikizia mtu kama yalivyo.
Asante sana kwa ufafanuzi kaka. Tunarudi kwenye weledi wa huyu askari wa barabarani. Kuna shida kubwa kwenye hichi chombo. Na haya ni mambo tunayoweza kuyaona huku nje. Kuna mengi ya huko ndani, nadhani ni hatari zaidi na uvundo zaidi.
 
Asante sana kwa ufafanuzi kaka. Tunarudi kwenye weledi wa huyu askari wa barabarani. Kuna shida kubwa kwenye hichi chombo. Na haya ni mambo tunayoweza kuyaona huku nje. Kuna mengi ya huko ndani, nadhani ni hatari zaidi na uvundo zaidi.
Tatizo askari wetu wamekaa kiuonevu na kimaslahi zaidi.
Kwa wenzetu kuna onyo kulinganisha na historia yako yakufanya makosa na ukubwa wa kosa husika.

Sasa huku kwetu askari anakukamata sababu umekanyaga kidogo zebra crossing kukiwa hakuna hata mtu anaevuka. Anashupaza shingo kabisa kama umeua na faini juu.
 
Kiongozi;
Inaonekana aliyepewa adhabu hakuwa amefunga mkanda kitu ambacho ni sahihi kupewa adhabu husika.
Kuhusu helmeti kuonekana kwenye maelezo ya adhabu ni kuwa; Kule kwenye formati ya makosa yameorodheshwa kwa magrupu
Mfano:
1. Mtoto akichelewa shule; hakufagia uwanja; adhabu yake ni fimbo tatu: Sasa hapo kama mtoto aambaye hakufagia uwanja adhabu yake itakuwa kwa hicho kifungu cha fimbo tatu. japo aliwahi shule lakini Hakufagia uwanja
2. Mtu ambaye hajafunga mkanda; bodaboda ambaye hajavaa kofia, adhabu yake ni shs 30,000. inamaana Boda boda akikamatwa atalipa 30,000 japo haimaanishi hakuwa amefunga mkanda. (najua wataziboresha kwa kuwa hivi karibuni boda wamepunguziwa faini hadi 10,000.

Muhimu: Pale askari anapo kuandikia kosa haandiki kila kitu, ana angalia tu kosa lako lipo kifungu gani; ana click hivyo makosa yote yenye adhabu iliyo kwenye hicho kifungu hutokea.
 
Pole sana mkuu kwa changamoto uliyokumbana nayo. Hao askari wetu vile vimashine (POS) wamepeww tayari vimelishwa (feed) makosa na namba zake. Askari haandiki kosa hilo yeye anaangalia tu namba kwenye mashine na inadisplay kile kilichokuwa kimewekwa mfumoni. Inatakiwa warekebishe mfumo.

Askari wetu kwanza lugha hiyo wataiweza kweli kuandika?😀😀
 
Mbona maelezo yanaeleweka ,maana apo imewekwa kwenye kundi moja ,kumaanisha ,kosa la kutofunga mkanda faini yake ni hiyo ,pia kosa la kutovaa kofia ngumu faini yako ni hiyo hiyo.au Mimi ndio sijaelewa

Kwa maelezo yako hayo, unadhani hapo mtenda kosa kakosea lipi kati ya hayo mawili?

Shuleni hua tunaenda kufanya nini hasa?
 
Mbona maelezo yanaeleweka ,maana apo imewekwa kwenye kundi moja ,kumaanisha ,kosa la kutofunga mkanda faini yake ni hiyo ,pia kosa la kutovaa kofia ngumu faini yako ni hiyo hiyo.au Mimi ndio sijaelewa

Kwa maelezo yako hayo, unadhani hapo mtenda kosa kakosea lipi kati ya hayo mawili?

Shuleni hua tunaenda kufanya nini hasa?
 
Kwa maelezo yako hayo, unadhani hapo mtenda kosa kakosea lipi kati ya hayo mawili?

Shuleni hua tunaenda kufanya nini hasa?
Kwani kakutwa anaenda piki piki au gari?yeye mwenyewe hajui?niongeze Basi,hivi shuleni ulienda kuchukua ujinga?ukiendesha gari unavaa kofia ngumu?ukiendesha piki piki unavaa mkanda?Yani ata mtoto mdogo angekucheka
 
Kiongozi;
Inaonekana aliyepewa adhabu hakuwa amefunga mkanda kitu ambacho ni sahihi kupewa adhabu stahiki.
Kuhusu helmeti kuonekana kwenye maelezo ya adhabu ni kuwa
Kule kwenye formati ya makosa yameorodheshwa kwa kwa magrupu
Mfano:
1. Mtoto akichelewa shule; hakufagia uwanja; adhabu yake ni fimbo tatu: Sasa hapo kama mtoto aambaye hakufagia uwanja adhabu yake itakuwa kwa hicho kifungu cha fimbo tatu. japo aliwahi shule lakini Hakufagia uwanja
2. Mtu ambaye hajafunga mkanda; bodaboda ambaye hajavaa kofia, adhabu yake ni shs 30,000. inamaana Boda boda akikamatwa atalipa 30,000 japo haimaanishi hakuwa amefunga mkana. (najua wataziboresha kwa kuwa hivi karibuni boda wamepunguziwa faini hadi 10,000.

Muhimu: Pale askari anapo kuandikia kosa haandiki kila kitu, ana angalia tu kosa lako lipo kifungu gani; ana click hivyo makosa yote yenye adhabu iliyo kwenye hicho kifungu hutokea.

Mimi nilichotaka kuwauliza tu wenzetu;
Hivi adhabu ya kuonya Madereva huku Tanzania haipo kwenye sheria za barabarani?
Unakuta mtu amepita sehemu ya 50 akiwa 55 ana andikiwa kosa, Siku moja niliandikiwa Kosa kwa kuwa wakati naingia highway kwenye mataa, nimewahi kuhama kuingia highway...wakati hapakuwa na gari lolote linakuja....
Laiti wangejua kuwa, ukimsimamisha mtu ukamuonya (kwa makosa madogo madogo) anaogopa na kuwa mwangalifu kuliko hata kumpiga faini!
Asante sana kaka. Umenifumbua macho. Ndio maana nilikuwa napata mashaka sana juu ya weledi wake. Kama mtu kaweza kuandika hii lugha namna hii, inawezekana vipi ashindwe kutofautisha!!!. Kumbe ni mambo ya ku-click. Hiyo pia ime-explain jambo jingine ambalo sikulitaja kwenye andiko langu. Kosa ambalo nilisimamishwa halina uhusiano kabisa na hayo ya helmet na mkanda.
Yawezekana Kosa langu halipo kwenye system hivyo akaamuwa kuchagua Kosa lolote. Bado kuna shida.
 
Kingine inaweza kua majibu yamejazwa tayari kwenye ile mashine anayoprint risit hivyo yeye anachagua namba kutokana na kosa ilayeye hajazi maelezo yyt
"Ndio wazo ambalo nami limenijia, namba ya kosa ndiyo imeleta kile kilichotokea.

Kama ni hivyo, ilibidi kwenye hiyo mashine iwe na hatua ya ziada ya kuchagua chombo cha usafiri kama gari au pikipiki ili kusiwe na mkanganyiko kwenye print out."
 
Pole sana mkuu kwa changamoto uliyokumbana nayo. Hao askari wetu vile vimashine (POS) wamepeww tayari vimelishwa (feed) makosa na namba zake. Askari haandiki kosa hilo yeye anaangalia tu namba kwenye mashine na inadisplay kile kilichokuwa kimewekwa mfumoni. Inatakiwa warekebishe mfumo.

Askari wetu kwanza lugha hiyo wataiweza kweli kuandika?😀😀
Asante sana kaka. Umenifumbua macho. Ndio maana nilikuwa napata mashaka sana juu ya weledi wake. Kama mtu kaweza kuandika hii lugha namna hii, inawezekana vipi ashindwe kutofautisha!!!. Kumbe ni mambo ya ku-click. Hiyo pia ime-explain jambo jingine ambalo sikulitaja kwenye andiko langu.
Kosa ambalo nilisimamishwa halina uhusiano kabisa na hayo ya helmet na mkanda, haswa ndiyo kitu kilichonikera zaidi.
Yawezekana Kosa langu halipo kwenye system hivyo akaamuwa kuchagua Kosa lolote. Nikisema nimesingiziwa Kosa nitakuwa nimekosea?? Bado kuna shida.
 
Back
Top Bottom