Trust None
JF-Expert Member
- Feb 12, 2018
- 1,260
- 4,415
Jeshi la Polisi leo April 2, 2021 wametoa ufafanuzi juu ya kauli waliyoitoa kuhusu shamra shamra za kusheherekea sikukuu za Pasaka.
‘Taarifa ya Jeshi la Polisi niliyoitoa jana (pamoja na mambo mengine) ilisema tuna imani kama kila Mwananchi atafuata Sheria na kujiepusha na vishawishi vya kufanya uhalifu, Ibada ya Pasaka itamalizika salama na hatutegemei zile Sherehe na Shamrashamra tulizozizoea kipindi cha miaka ya nyuma kuwepo katika kipindi hiki, kwa bahati mbaya taarifa hiyo ilipokewa na tafsiri tofauti kuwa Jeshi la Polisi limepiga marufuku Sherehe za Pasaka”– David Misime-SACP, Msemaji wa Polisi
“Jeshi la Polisi halijapiga marufuku Sherehe za Pasaka na ndio maana hata jana Ibada ya Sikukuu ya Alhamisi Kuu ilifanyika Nchi nzima bila bughudha yeyote na Askari wetu waliovaa sare za Polisi na waliovaa kiraia walikuwa doria kuhakikisha amani, utulivu na usalama unakuwepo”
“Jambo ambalo hatutegemei kuliona ni zile shamrashamra kubwa kama vile Matamasha na Makongamano ya Pasaka na kwa bahati nzuri wanaoyaandaa kila mwaka kwa utu wao wa Kitanzania, hekima na busara zao hatujasikia wakitangaza maandalizi ya Matamasha hayo”
“Ibada za Sherehe za Pasaka kwenye Makanisa, Sherehe za Kifamilia, Hitma, Familia kuungana na kwenda kutembelea sehemu mbalimbali na kusherehekea Pasaka hakuna aliyekataza ili mradi unachofanya kinaendana na kufuata utu, busara, hekima, Sheria , kanuni na taratibu za Nchi”
PIA SOMA:
CHANZO: Millard Ayo
‘Taarifa ya Jeshi la Polisi niliyoitoa jana (pamoja na mambo mengine) ilisema tuna imani kama kila Mwananchi atafuata Sheria na kujiepusha na vishawishi vya kufanya uhalifu, Ibada ya Pasaka itamalizika salama na hatutegemei zile Sherehe na Shamrashamra tulizozizoea kipindi cha miaka ya nyuma kuwepo katika kipindi hiki, kwa bahati mbaya taarifa hiyo ilipokewa na tafsiri tofauti kuwa Jeshi la Polisi limepiga marufuku Sherehe za Pasaka”– David Misime-SACP, Msemaji wa Polisi
“Jeshi la Polisi halijapiga marufuku Sherehe za Pasaka na ndio maana hata jana Ibada ya Sikukuu ya Alhamisi Kuu ilifanyika Nchi nzima bila bughudha yeyote na Askari wetu waliovaa sare za Polisi na waliovaa kiraia walikuwa doria kuhakikisha amani, utulivu na usalama unakuwepo”
“Jambo ambalo hatutegemei kuliona ni zile shamrashamra kubwa kama vile Matamasha na Makongamano ya Pasaka na kwa bahati nzuri wanaoyaandaa kila mwaka kwa utu wao wa Kitanzania, hekima na busara zao hatujasikia wakitangaza maandalizi ya Matamasha hayo”
“Ibada za Sherehe za Pasaka kwenye Makanisa, Sherehe za Kifamilia, Hitma, Familia kuungana na kwenda kutembelea sehemu mbalimbali na kusherehekea Pasaka hakuna aliyekataza ili mradi unachofanya kinaendana na kufuata utu, busara, hekima, Sheria , kanuni na taratibu za Nchi”
PIA SOMA:
Polisi Tanzania: Hatutegemei kuona sherehe za Pasaka wakati Nchi bado ipo kwenye maombolezo
Jeshi la Polisi nchini limesema halitegemei kuona sherehe na shamrashamra za Pasaka kama za kipindi cha nyuma katika kipindi hiki ambacho nchi bado ipo kwenye maombolezo ya kuondokewa na Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. ==== Ndugu wanahabari, kama mnavyojua bado taifa letu lipo katika siku 21...
www.jamiiforums.com
CHANZO: Millard Ayo