Polisi Tanzania inanuka rushwa

Polisi Tanzania inanuka rushwa

Nashangaa wote mnatoa tuhuma kwa polisi kupokea rushwa sijaona hata mtu mmoja akiwahimiza madereva wasiwape polisi rushwa wakati kila mmoja wetu tunafahamu kuwa mtoa rushwa na mpokeaji wote wanahatia. Nadhani kuikomesha rushwa ni kitu kidogo nikuwambia madereva waache kutoa rushwa kwa askari kinyume cha hapo tutabaki kuimba wimbo wa rushwa kama wendawazimu.

Polisi wamezidi njaa
 
Takukuru ni wasanii wale, kama wangekuwa wanafanya kazi zao basi rushwa isingeendelea kushamiri nchini.

Hilo wazo zuri. Lakini pia ni vema watu wa TAKUKURU kujaribu kuingia field. Yani nina uhakika lazima watamkamata trafiki hasa kipindi hiki cha sikukuu. Kutoka Dar wakifika Chalinze tayari watakua wameshakamata tukio la Rushwa maana haya mambo yanafanywa nje nje bila kificho.
 
Inawezekana pia watoa rushwa hawana elimu ya kutosha kuhusu haki zao. Lakini upande wa polisi wao ndio wanajua lakini kwa nini wao wanavunja sheria hadharani? Hivi asilimia 99% ya magari ni mabovu kama unavyodai ndio ticket ya kupokea rushwa?

Hakuna raia asiyejua kutoa/kupokea rushwa ni kosa. Waambie wabunge wenu wabadilishe sheria hizi ambazo zinaurasimu katika kuanzisha au kuendesha biashara au kitu chochote maana ndizo zinazochangia kuchochea rushwa. Hata kama mimi ningechukua hiyo rushwa kama basi lako halistahili kuwepo kwa road na wewe umeliweka hivyo ni sawa na kusema nimekuja kukupatia chako niendelee na changu.
 
rushwa itaendelea kuwepo na kuwepo...tatizo la rushwa inabidi tuanzie juu ya mabilions....syo hao wachukua rushwa dagaa
 
Kwanza mimi sio mtoto nimeshuhudia kwa macho yangu. Ikaniuma kwa ajili ya nchi yangu. Kwa nini rushwa imekua hadharani kiasi hiki? Tunaipeleka wapi nchi yetu? Trafiki hawana hata aibu.
piga kelele kwa serikali iwaongezee masilahi huenda kero hizo zikaisha
 
Kama gari bovu sheria si zipo? Kwanini kujishusha hadhi kazi yao kwa ajili ya sh 2000? Hata kama njaa polisi wamezidi. Na Kwanini usimamishe gari halafu unazunguka nyuma ya gari?
unaona wanafaidi sana? wivu tu nenda na ww ukaombe kazi hiyo
 
Nimekuwa safarini siku mbili hizi na nimeshuhudia rushwa nje nje imekuwa kama tuko Nigeria vile. Yaani traffic police wanasimamisha magari halafu hawaji kwenye gari konda anazunguka nyuma ya gari anampa hela. Na hiki kipindi naskia wanatafuta hela ya sikukuu ni wamejaa humo barabarani usiseme.
Kilichoniuma ni kuwa kimsingi polisi ndio wasimamizi wa sheria lakini wanachukua rushwa huku raia wakishuhudia. Hali hii inatisha. Mbaya sana. Hata watoto wadogo wanaona wanajifunza nini? TAKUKURU Wapo na hawaoni haya yanayotokea. Mbaya!!!

Huo ni ukweli usiopingika.

Inabidi hatua za haraka sana sichukuliwe la sivyo hili jeshi la polisi litaipeleka hii nchi pabaya. Wengi wa mapolisi si waaminifu.
 
Takukuru ni wasanii wale, kama wangekuwa wanafanya kazi zao basi rushwa isingeendelea kushamiri nchini.


mdau BAK TAKOKURU hawawez kuimaliza rushwa,wala wanasiasa hawawez kuimaliza rushwa,wala katiba haitamaliza rushwa,ila sisi wananchi wenyewe,soma pia PhD Thesis ya Dk.Hoseah inazungumzia CORRUPTION IN TANZANIA
 
Last edited by a moderator:
Wamezidi sasa maana hata madereva wanalalamika maana imebidi apunguze dau alianza na buku mbili akashuka hadi jero kaona karibu kila kituo wapo. Na traffic wasivyo na haya wanachukua tu.

MamaBeata usiumize kichwa rushwa nchi hii imeshindikana
 
Last edited by a moderator:
Rushwa mnatoa wenyewe, hakuna polisi anayelazimisha utoe rushwa. Kama una kosa kwa nini usikubali ulipe faini, badala yake unakimbilia kutoa rushwa. Hata mimi ningekuwa polisi ningepokea maana pesa mnatoa wenyewe bila kulazimishwa.
 
Back
Top Bottom