Polisi Mbeya: Mwenye taarifa za alipo Mdude azitoe

Polisi Mbeya: Mwenye taarifa za alipo Mdude azitoe

Haya mambo ya kusema baadhi ni kama kutaka kuwaisolate watu fulani fulani ,sijui kwa manufaa na nani? .

Polisi wote wa nchi hawana jema kama una mtu wa karibu kaa nae mbali mzee otherwise kuna siku litakukuta Manjagu sio kabisa yaani.
Mwaka juzi nilimkataa polisi kumpangisha wale madalali walijichanganya baada ya kuhoji kazi yake..hawa polisi huwa sina urafiki nao kabisaa
 
Waliotoa taarifa kuwa ni polisi ndo wamemchukua wahojiwe inawezekana wanawafahamu hao polisi
 
Washamuua mwamba,nchi ngumu sana hili. Wanataka wote tuimbe na kuabudu,Bibi Kizimkazi kaweka pamba masikioni. Rest in peace 🕊️ mdude,bei uliyolipa kwa kuwa outspoken ni kubwa sana.

Safari hii sidhani kama watafanya mistake kama ya kwa mzee kibao,wata hakikisha hata kucha za mwamba hazipatikani. Halafu unakuta hii mijamaa leo imeenda msikitini,kesho na kesho kutwa kanisani kusali huku mikono yao imejaa damu za watanzania.
 
Kwa matukio yaliyopita mabaya ya watu kujeruhiwa,kuuwawa na hili la Mdude kupotezwa na polisi sina hakika kama yu hai ilitosha kabisa watanzani nchi nzima kufanya maandamano kupinga uchafu huu ila ni bahati mbaya sana sisi wananchi TUMELOGWA tumejikita na umbeya kwa Mange pamoja na Simba na Yanga.
 
Back
Top Bottom