View attachment 523359
UkitazamaTV, kusikiliza radio ama kusoma magazeti ukakutana na habari inayolihusu jeshi letu la police lazima, habari hiyo lazima itakuwa ni ya kihalifu ama kutoa makatazo ama matamko.
Mimi sijawahi kuona kwenye media eti police wametoa msaada wa kitu ama huduma fulani kwa jamii kwa lengo la kujenga uhusiano mwema na general public. Mbona ikulu wanatoaga mbuzi, unga na michele walau mara moja moja (sio vibaya) kwa vituo vya watoto yatima wakati wa sikukuu na sherehe za kitaifa.
Hii inashindikana vipi kwa police? Kitengo na mahusiano ya jamii (PR) kipo kweli ndani ya jeshi letu la police? Kama kipo mbona sioni kama wanafanya kazi yao kwa ufanisi? Kama wanafanya kazi zao inavyopaswa wanafanyia wapi? Mbona hatuwaoni kwenye media (tv, magazeti na redio) kwa kuwa through media ndio njia pekee Police wanaweza kuitumia kujisafisha.
Mimi naona wakati ndio sasa kwa kamanda sirro kuboresha utendaji wa idara ya PR ya Police ama kuunda idara hiyo kama haipo ( mimi sijui kama ipo).
Nawasilisha
Si taasisi nyingi za kiserikali (zisizo za kibiashara) zinazotoa kipaumbele kwa kitengo/idara za PR. Nadhani hii inatokana na kutotambua kwa undani umuhimu wa PR katika taasisi yoyote. Polisi wamekuwa na Idara ya Uhusiano tangu miaka mingi. Kabla ya huyu mama Advera, kulikuwa na afande alijulikana kwa jina la Mwamunyange. Ni ndugu na Mwamunyange, mkuu wa jeshi mstaafu.
Kipindi kile ile idara ilijikita zaidi kuchapisha jarida la ndani la Polisi (news letter) ambalo walikuwa wanalitoa kama sikosei mara nne kwa mwaka (quartely), pamoja na kusambaza habari na matukio ya kipolisi kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Kazi hii ilifanywa sana na afande mmoja alijulikana kama Mohamed Mhina. Baadaye huyu afande alihamia Zanzibar. Sijui siku hizi yuko wapi. Hata wakati huo idara ile haikujikita sana kwenye shughuli za Corporate Social Responsibility (CSR) ambao ndio msingi wa andishi lako.
Ninachokiona, inawezekana ama kitengo kile ndani ya polisi kimekuwa kikiongozwa na na maafande ambao hawana taaluma hiyo, au pengine wana taaluma lakini bajeti ya kutekeleza mawazo/mapendekezo (concepts/proposals) wanayowasilisha inakosekana, na hivyo kujikatia tamaa na kubaki kusubiri kuagizwa kuzungumza na waandishi wa habari.
Nimesema, kuna uwezekano kwamba wasemaji wanaoongoza vitengo hivyo hawana taaluma kutokana na ukweli kwamba, kuna dhana kuwa mtu yeyote anaweza kuwa msemaji wa taasisi kama ambavyo kumekuwepo na dhana kwamba mtu yeyote anaweza kuwa mwandishi wa habari.
Idara ya PR ikiongozwa na mtu asiye mwanataaluma kwa vyovyote haiwezi kutimiza wajibu wake sawa bali kitakachofanyika ni zile kazi ndogondogo za kusema kile kinachoagizwa kusemwa au kuandika taarifa kwa vyombo vya habari ambazo nazo wahariri watazitumia kwa sababu tu ya unyeti wa taasisi (polisi) na pengine taarifa yenyewe,lakini si kwa namna zinavyoandikwa kuweza kushawishi wahariri kuzitumia na wasisitupe kwenye 'kapu la uchafu'.
Kazi hata zile za kutoa misaada mbalimbali zinatakiwa zifanyike kwa malengo maalum ambayo yanaweza kuainishwa vizuri na mtu mwenye taaluma. Utoaji misaada au ushiriki kwenye matukio mbalimbali ya kijamii ni lazima ufanyike kwa utaratibu na matokeo yake yafanyiwe tathmini, mambo ambayo mtu asiye na taaluma hawezi kufanya.
Kuna mambo kama mchangiaji mmoja alivyodokeza, jeshi la polisi kuwa na program za kupeleka elimu kwa wanafunzi kuhusu mambo mbalimbali kuhusu jeshi hilo pamoja na umuhimu wa kulinda amani (labda?), ni mambo ambayo yanatakiwa kuandaliwa kitaalamu ili yawe na tija. Haya hayawezi kuandaliwa na afande ambaye amepelekwa kitengo hicho bila kuwa na taaluma hiyo.
Hayo ni maoni yangu, inawezekana polisi wanayo maelezo mazuri zaidi kulingana na hoja yako mkuu.