Polisi Central Arusha: Shangwe na wimbo wa Taifa vyarindima

Mkuu Derimto.

Kadhia yote hii imesabishwa na mtu mmoja mpenda sifa za kitoto kibaya zaidi viongozi wake badala ya kutumia akili wakajiingiza kichwa kichwa.

Hata mimi wamenishangaza sana hawa viongozi,yaani wameingia kwenye mkumbo wa mnafiki mmoja asiye na akili,SERIKALI YOOTE IKO PAMOJA NA KUBERI.
 
Tunahitaji 'Lemas' watatu Dar. Mmoja ilala, mwingine Kinondoni, Mwingine Temeke. Unfortunately and unexpectedly hivi viatu vimempwaya Mnyika...
 
Jamani bado hali ni tete mkoani Arusha kuliko inavyodhaniwa na wengi.

Nimeweza kutumia uzoefu wangu na kuingia Police Central kuna ulinzi mkali polisi zaidi ya 70 wenye silaha na wengine wanaingia na kutoka.

Hali ni tete sana hakuna ruhusa mtu kuingia eneo la Police Central kwa namna yoyote ile hata kama una shida gani unazuiliwa getini na askari wenye silaha tayari kwa lolote na kama una shida ya kipolisi unaambiwa nenda kwenye vituo vingine vidogo utahudumiwa huko.

Nimeweza kupenya na kuongea na baadhi ya maofisa waandamizi akiwemo Zuberi mwenyewe ambaye alikuwa ameenea uwanjani akiwapanga mapolisi na kuonekana makini na kila kona kwa umakini na tahadhari kubwa kabisa.

Kwa hali ilivyo hapa kaunta hakuna kazi nyingi kama ilivyo kawaida bali
ni nyimbo za Taifa Shange nderemo na vifijo na vigelele vya wanawake walioko mahabusu huku wakimaliza nyimbo na kunza upya kwa kauli mbiu ya Peoples Power kiasi ambacho hata baadhi ya askari wanaonekana kujaribiwa ila majukumu yanawabana lakini wanaonekana kuhamasika na nyimbo hizo.

Nimetoka na kujaribu kutembea baadhi ya mitaa FFU wanazunguka na mapikipiki na wengine kwa miguu wakiingia kila uchochoro kuangalia kama kuna makundi ya vijana na kuyatawanya na inavyoonekana watu wamenyamaza lakini akili zao bado hazijatulia na watakuja na maamuzi mapya ambayo yanaweza kuigharimu serikali na Amani yetu kwa ujumla.

Nimefurahishwa na hao kinamama walioko mahabusu. Sijui serikali inataka nini jamani maana kitu kidogo wamekikuza na punde litakuwa tatizo kubwa.
 
I am afraid to say kwamba Tanzania now is in shambles... Msimu wa kilimo, lakini tunahangaika na mafuta, umeme, migomo, kufilisika kwa serikali, sherehe za 50 years of independence, ufisadi, saisa uchwara na mambo mengi yasiyo na maana
 
Usijali,sifanyi mtihani wa kisw hapa,lkn pamoja na kukosea bado nimeeleweka.Lengo langu lilikuwa ni kueleweka na sio kuandika kisw fasaha.Hata hivyo nashukuru kwa kunifuatilia.

Ulichoandika kinaeleweka vizuri hivyo achana nae anatafuta kukera watu tu.
 
Mbowe amewaingiza wenzake mkenge yeye amekimbia. Muda huu yupo uraiani anakula bata. Kweli wajinga ndio wali wao.
 
Tunahitaji 'Lemas' watatu Dar. Mmoja ilala, mwingine Kinondoni, Mwingine Temeke. Unfortunately and unexpectedly hivi viatu vimempwaya Mnyika...

Lema hauwezi kumlinganisha na Mnyika. Mnyika anafikiria kabla ya kutenda wakati Lema anatenda kabla ya kufikiria.
 
Nimetokea maeneo ya Njiro kuja town kupitia Keep-Left ya Impala, kuingia hadi Clock tower (Arusha hotel) hadi CRDB friends corner kuelekea stendi kuu ya mabasi, sikufanikia kuona Police-Traffic hata mmoja!
wanaogopa kusimama barabarani.
Nimekutana na Deffender zaidi ya Tano zenye polisi wenye sillaha nzito nzito, Mbwa, na mabomu ya machozi.
Nikashuka kuingia ATM ya CRDB pale maeneo ya Friends kona, nikakuta maafisa Usalama wa Taifa zaidi ya watatu wakiwa na Com-Sets zao masikioni, na wengine na radio-calls ndogondogo, wakiwa very busy kutoa report!
Kwa kweli hali si shwari hapa Arusha.
Nimepitia hadi Viwanga vya nmc, hakuna yeyote pale! kuna mabaki ya mipira iliyochomwa jana, na kuni ambazo watu waliota jana usiku.
It is real PIPOZ PAWA!
I SUBMIT WAUNGWANA!
taarifa yako nzuri lakini mwishoni umemalizia kishabiki!
 
Hii ni hatari sana,tatizo viongozi wa nchi watumia masaburi kufikiri,kama serikali ingekuwa makini wangejiuliza haya yote tatizo nini,wangewaita wananchi wakawasilkiliza na kufanyia kazi maoni yao.haiwezekani leo hii unapewa dhamana ya kuwaongoza watu kisha una waita panya!kitendo hiki kinaonyesha dhahiri kina baraka zote za mabwana wakubwa na ndiyo maana wamenyamza kimya hawataki kutoa kauli.Nchi inateketea kwa ujinga na ulevi wa madaraka.Bora ulewe pombe kuliko kulewa madaraka,hii ni hatari kubwa sana.Leo hii waziri Membe anasimama kuwakemea Waingereza kwa kulazimisha kutambuliwa ndoa za jinsia moja,lakini muda mfupi mara baada ya kutoa tamko hilo wanageuka na kumlaki mwana wa mfalme kwa mbwembwe za kila aina,hivi kweli tutafika?kwanini tunaimba kijamaa ili hali tunacheza kibepari,kama kweli ni wakweli kwanini tusitembee kwenye kauli zetu?Leo Mtanzania gani anayeweza kukubali kauli hii itatekelezwa kwa vitendo ili hali bwana kubwa mtoto wa malkia ameingia na kufanyiwa dhifa ya kitaifa ndani ya jmba letu tukufu.


ukichanganya haya yote,mapokezi ya mwana wa mfalme na sakata la Arusha utaamini viongozi wetu wanatumia masaburi kufikiri.Si ajabu leo hii ukasikia baba Rdh kauma pipa huyo majuu kula kuku kwa mrija.Wako wapi waaskofu waliosema kuwa hili ndiyo chaguo la Mungu watokee hadaharani na kuwataka radhi wana wa nchi hii!Pia watueleze sababu zipi zilizo wasababisha kutoa kauli,na kama walinunuliwa basi nchi hii inahitaji huruma ya Mungu kuondokana na ombwe hili la uongozi.

Viongozi wa Chadema kama kweli dhamira ni kuwakomboa wanyonge,msiogope magereza kwani Paulo na Sila waliomba milango ya gereza ikafunguka,nanyi ni wakati wenu kulia kwa vitendo mpaka milango ya gereza itafunguka.Wananchi wana imani nanyi kurudi kwenu nyuma itakwa ni usaliti mkubwa,dhima mliyopewa na wananchi ni kuwaonyesha njia,kazeni buti kwani saa ya ukombozi ni sasa.Aluta Continua mapambano ndo kwanza yanachukua kasi.Mungu ibariki Tanzania,Mungu wabariki Watanzania wasiwe wanafiki katika harakati za ukombozi wa ukoloni mamboleo kutoka kwa mkolono mweusi
 
swala la msingi ambalo Ritz na wenzake akina Mchaga hawaelewi ni kwamba matatizo yanayotokea Arusha si kwa sababu ya CDM ila ni bkoz ya hali mbaya tuliyonayo watanzania. Laiti kama maisha yasingekuwa magumu.............. lema angejikuta jela alone, ila msingi wa hayo yote ni uhalisia wa maisha. Wale mnaofanya propaganda humu kwa kukosoa hadi lugha sielewi mnachotafuta. Wakati mnapeleka mrejesho huko kwa wanaowatuma kufanya hiyo kazi waeleze ukweli. Tariq Azziz wakati anampa ushauri Saddam hakumweleza ukweli kinachoendelea ktk uwanja wa mapambano, mpaka mzee kazingirwa bila taarifa. Nyie wanaowatuma mnawalaghai pia inavyoonekana.
 
Mbunge gani hujui ku spell neno "aahirishe"? Siku moja utakuja kumwomba Spika aharishe kwenye kikao!

wewe ndio unahisi unakijua kiswahili fasaha? Kama huna kazi ya kufanya nenda kaungane na wenzako kumkaribisha Prince Charles
 
Back
Top Bottom