Polisi Central Arusha: Shangwe na wimbo wa Taifa vyarindima

Ningeshauri huyo prince Charles ahairishe hiyo ziara yake ya Arusha..Aende akatembee Kilombero Wakulima wa Miwa na Mpunga..

Mi naona bora aje kwetu huku Lindi na Mtwara sijui kwa nini wanampeleka maeneo mazuri.
Jana ilitakiwa wampeleke Tandale au Tandika ajione hali halisi ya Mtanzania sio kumpakia kwenye Panton lililo pakwa rangi siku moja kabla ya kulipanda
 
Mkuu Derimto.

Kadhia yote hii imesabishwa na mtu mmoja mpenda sifa za kitoto kibaya zaidi viongozi wake badala ya kutumia akili wakajiingiza kichwa kichwa.
 
Ningeshauri huyo prince Charles ahairishe hiyo ziara yake ya Arusha..Aende akatembee Kilombero Wakulima wa Miwa na Mpunga..
ha ha ha, hajui kilimo huyo Regia, amekulia katika jumba la dhahabu kila kona.
 
Jamani bado hali ni tete mkoani Arusha kuliko inavyodhaniwa na wengi.

Nimeweza kutumia uzoefu wangu na kuingia Police Central kuna ulinzi mkali polisi zaidi ya 70 wenye silaha na wengine wanaingia na kutoka.

Hali ni tete sana hakuna ruhusa mtu kuingia eneo la Police Central kwa namna yoyote ile hata kama una shida gani unazuiliwa getini na askari wenye silaha tayari kwa lolote na kama una shida ya kipolisi unaambiwa nenda kwenye vituo vingine vidogo utahudumiwa huko.

Nimeweza kupenya na kuongea na baadhi ya maofisa waandamizi akiwemo Zuberi mwenyewe ambaye alikuwa ameenea uwanjani akiwapanga mapolisi na kuonekana makini na kila kona kwa umakini na tahadhari kubwa kabisa.

Kwa hali ilivyo hapa kaunta hakuna kazi nyingi kama ilivyo kawaida bali
ni nyimbo za Taifa Shange nderemo na vifijo na vigelele vya wanawake walioko mahabusu huku wakimaliza nyimbo na kunza upya kwa kauli mbiu ya Peoples Power kiasi ambacho hata baadhi ya askari wanaonekana kujaribiwa ila majukumu yanawabana lakini wanaonekana kuhamasika na nyimbo hizo.

Nimetoka na kujaribu kutembea baadhi ya mitaa FFU wanazunguka na mapikipiki na wengine kwa miguu wakiingia kila uchochoro kuangalia kama kuna makundi ya vijana na kuyatawanya na inavyoonekana watu wamenyamaza lakini akili zao bado hazijatulia na watakuja na maamuzi mapya ambayo yanaweza kuigharimu serikali na Amani yetu kwa ujumla.

Nakuaminia mkuu.. kama kawa tupe nyuz..))
 
Nimetokea maeneo ya Njiro kuja town kupitia Keep-Left ya Impala, kuingia hadi Clock tower (Arusha hotel) hadi CRDB friends corner kuelekea stendi kuu ya mabasi, sikufanikia kuona Police-Traffic hata mmoja!
wanaogopa kusimama barabarani.
Nimekutana na Deffender zaidi ya Tano zenye polisi wenye sillaha nzito nzito, Mbwa, na mabomu ya machozi.
Nikashuka kuingia ATM ya CRDB pale maeneo ya Friends kona, nikakuta maafisa Usalama wa Taifa zaidi ya watatu wakiwa na Com-Sets zao masikioni, na wengine na radio-calls ndogondogo, wakiwa very busy kutoa report!
Kwa kweli hali si shwari hapa Arusha.
Nimepitia hadi Viwanga vya nmc, hakuna yeyote pale! kuna mabaki ya mipira iliyochomwa jana, na kuni ambazo watu waliota jana usiku.
It is real PIPOZ PAWA!
I SUBMIT WAUNGWANA!
 
Back
Top Bottom