Polisi Arusha wafanya unyama wa Kutisha

Polisi Arusha wafanya unyama wa Kutisha

Sasa risasi inamfyatukia vipi? Kama zinafyatuka hivyo mbona haziwajeruhi askari? Je silaha ni mbovu hazikaguliwi? Au Kijana alitaka kuikwapua ikabidi wam "shoot"? Tunasubiri mujibu ya ripoti..
 
Kijana Richard Peter Lombo (29) ameuawa na polisi wilayani Arumeru kwa kupigwa Risasi kifuani akiwa ndani ya Kituo cha Polisi Usariva Mkoani Arusha baada ya kufikishwa hapo akituhumiwa kwa uhalifu.


Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Longinus Tibishubwamu akizungumzia tukio hilo kwa Njia ya simu amesema kuwa kijana huyo alikuwa kibaka na alitaka kuchukua silaha ya askari lakini katika mvutano huo ukasababisha risasi kufwatuka jambo ambalo kaka yake Issa Juma amesema kuwa ameshuhudia askari akimfyatulia ndugu yake huyo risasi ya kifuani na kufariki papo hapo.


Ndugu wa kijana huyo wakiwemo wazazi wake wamemtaka waziri wa mambo ya ndani ,Kangi Lugola kuja mkoani hapa kufuatialia tukio hilo kwani kinachoelezwa na kaimu kamanda in uongo mtupu na unalenga kuipotosha jamii.


Familia imegoma kuuzika mwili wa kijana wao uliipo Mochware wakilalamikia unyama uliofanywa na askari hao wasiofuata na kuzingatia maadili ya Kazi yao kwa kufanya mauaji ndani ya kituo hicho cha Polisi bila woga na kudanganya kuwa alitaka kuwapora silaha



Sent using Jamii Forums mobile app
Safi sana, Askari ni shujaa anatakiwa apandishwe cheo...!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Askari anapanda cheo kiulaini ajabu.Eti akataka kumnyang'anya polisi silaha!Kwa urahisi tu.Nkt!
 
Kipindi hiki kuna majaribio ya risasi nini? bado lile la itigi
 
Huyo askari apandishwe cheo kama alivyoagiza Mh. Rais wetu
 
Hii imekaa vibaya sana!!
Ila kwanini raia tunaleta mazoea ya kijinga hivi kwa askari wetu,eti bila woga mtu unajaribu kupora silaha ya askari aliyeiva kimafunzo(well trained policeman).


5/5

A well trained policeman anamuua kibaka kwa silaha ipi? Aliyomnyang'anya kibaka au silaha aliyonyang'anywa na kibaka !!?
 
Ni mtoto wa mfanyakazi mwenzetu,ni ndugu wa kijana staff mwenzetu,ni ndugu binamu wa staff wenzetu wawili tena wameenda msibani!Ngoja nifikirie outside the box,Muhalifu apelekwe mpaka kituoni alafu auwawe hapo akiwa mahabusu?kwa nini wasimpige risasi huko njiani waseme alikuwa anatoroka waje wajiletee kesi bila sababu kwa kumuuwa akiwa kituoni?walikamatwa wawili inadaiwa lakini mmoja akatolewa akaambiwa asiseme chochote akitoka,hii nayo haingii akilini,mwenzio apigwe risasi ukishuhudia alafu wewe uachwe?Nani anataka ushahidi huo?Tusipende kuwalaumu polisi bure.Kwani polisi hujitaftia wahalifu au sisi wenyewe ndio tunapelekana huko kituoni?Imagine upige simu polisi majambazi au vibaka wamekuvamia nyumbani kwako polisi wasije?imagine uende kituoni ukatoe malamiko dhidi ya mtuhumiwa wako polisi wakae kimya?Tuwaache polisi wafanye kazi na tupishe uchunguzi wa vyombo vinavyohusika.Hakuna aliyekuwa kituoni,tuache kusikiliza umbea wa mitaani!Poleni sana staff wenzngu,poleni ndugu zangu wafiwa,mungu awape subra katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wenu.Haki ya mtu haipotei,huchelewa tu!
 
hakuna kibaka anaeweza kupora siraha akiwa polisi kama angekua na ujasiri huo asingefika polisi...aisee tunakoenda siko vikesi vya ukibaka unamfyatulia mtu risasi ukiwa kituoni ila ishu ya dhahabu mnatumia Gari ya polisi kusindikiza Mali ya ujanja ujanja na king' ora juu...
 
Back
Top Bottom