Msukuma_De_Great
JF-Expert Member
- Nov 26, 2016
- 1,185
- 974
Hivi polepole bado yupo?
wewe ndio wa kupuuzwa kwa sababu wewe ni mpuuzi siku zote.Nimemsikiliza jana kijana mwenzangu ndugu Humphrey Polepole akizungumza kwa niaba ya ccm juu ya mambo kadhaa aliyoyaita makubwa nchini, mambo hayo ni mauaji ya Kibiti na Ripoti ya Makanikia.
Nimelazimika kulichambua hili kwa mtindo wa makala kwa nia ya kumkanya na kumwambia Polepole awe na adabu na heshima kwa Watanzania, sisi sio wajinga kama anavyotupimia kipimo alichonacho ambacho ni wanachama wenzake ndani ya ccm.
Nimesikitika kuona kijana huyu anawaita Watanzania ni wapuuza wale tunaounga mkono juhudi za rais huku tukihoji kwamba wizi wote huu katika raslimali umefanywa na Chama cha Mapinduzi, hivyo tukitaka makada wa chama hicho wasimvuruge Rais anapojaribu kupambana na hali hii.
Natataka nimrejeshe nyuma kijana huyu kwa lengo la kumfunza ama kumkumbusha na kisha kumkanya awe na adabu mbele ya umma hasa linapokuja suala la maslahi mapana ya nchi itikadi na mihemko yake iishie viunga vya Lumumba.
Mwaka 1998 wakati makampuni makubwa ya uchimbaji madini ya ASHANTI yalipoingia mikataba na serikali ya Tanzania iliyokuwa chini ya mwenyekiti wa ccm na rais wa Tanzania Benjamin William Mkapa, chama cha mapinduzi kililiridhia kwa kauli moja, serikali yake kuingia mikataba hiyo na kikahubiri hadharani kwamba taifa sasa linanufaika, Hivyo tunapohoji ushiriki na uratibu na unufaika wa ccm katika raslimali za nchi yetu, Polepole anapata wapi kibri chakutuita sisi wapuu?
Kwamfano Mgodi wa Golden Pride ambao umemaliza dhahabu yote tani 76 katika eneo la Lusu wilayani Nzega. Kampuni ya Resolute ya Australia iliwekeza dola 370 milioni kuanzia mwaka 1998 (mkataba wao ulisainiwa 25th June 1997). Katika kipindi cha uhai wa mgodi, miaka 14, Kampuni hii imeuza dhahabu ya thamani ya dola za kimarekani 3.3 bilioni, Muulizeni Polepole kama anafahamu kampuni hii ililipa mrahaba wa shingapi mpaka madini yalipoisha? Haya yote yamefanyika chini ya ccm
Lakini sivyo tu, rejea hansadi za Bunge juu ya hotuba za Upinzani zote tangu bunge la kwanza la vyama vingi, upinzani wamekuwa wakipiga kelele uwazi wa mikataba hii ambayo yote husainiwa Ikulu ya Tanzani, yani wizi wote mkubwa katika nchi hii huratibiwa Ikulu tangu Mwalimu Nyerere alipotutoka tu. Polepole anaweza kuwa hajui kwakuwa ameingia juzi kwenye siasa ya nchi hii anafikiri kuongoza ccm ni kuongoza zile NGOs zake za pale Mwenge za utetezi wa haki za mashoga.
Suala lingine alilozungumza Polepole na kujinasibu ni kiongozi wa chama cha watu ni suala la Mauaji ya Kibiti huku akimtisha Waziri wa Mambo ya Ndani na IGP katika taarifa yake. Na zaidi akajikita kutuhumu vyama vya siasa kwamba vimekaa kimya. Nataka nimkumbushe, vyama vya siasa havijakaa kimya, vyama vya siasa vina platform yake ya kutolea kauli za kitaifa na njia hii havipangiwi na chama kingine yaani chama cha kihalifu ccm,
Mauaji ya Kibiti ni uhalifu mkubwa, una kila elements za kubashiri aina zake, mauaji haya hayahitaji kukurupuka kisiasa, kwakuwa kwakufanya hivyo waweza kujikuta yanageuzwa kuwa matukio ya kisiasa au ya kidini kws vyovyote yanavyoweza kuchukuliwa, Yanahitaji vyombo vya kiuchunguzi ndivyo vishughulike nayo, na sio matamko ya kisiasa kama polepole anavyotaka iwe, wala hayahitaji matamko ya kidini labda katika muundo utakao kutanisha imani zote pawe na sauti moja, nje ya hapo yatajengwa mazingira na kuitwa mauaji ya kidini. Polepole kwa mambo haya ni mchanga, walionyamaza na kuacha vyombo vya dola vifanye kazi anawaona wapuuzi ile yeye ndiye mjanja na mzalendo,
Nataka nimkumbushe tu katika utawala wake ccm, Anafahamu kwamba Ben Saanane maarufu kama Ben-Rabiu Wa Saanane ni mwezi wa sita huu amepotea/ametekwa? Ipo wapi kauli ya chama chake katika hili?
Anafahamu kwamba Bagamoyo miili saba iliokotwa kwenye viroba ikazikwa pembeni ya mto mithiri ya mbwa? Ipo wapi kauli ya chama yeye akiwa msemaji? Anafahamu kwamba Lugumi imekiuka mkataba wa makubaliano na wizara ya mapolisi juu ya ufungaji ya mitambo ya kielekroniki vituo vya polisi na kampuni hiyo ilishalipws pesa zote kufunga vituo zaidi ya 200 lakini mpaka dakika hii ni vituo vinne tu ndivyo vimefungwa? Ipo wapi kauli ya chama yeye akiwa msemaji? Mnafiki mkubwa huyu..
Manunuzi ya Ndege, ujenzi wa barabara za Mwenge > Moroko, Mwanza Airport nk zimeidhinishwa cha Bunge lipi nchini? Ipo wapi kauli ya chama katika hili yeye akiwa ni msemaji?
Namsihi sana Polepole awe na adabu mbele za Watanzania, Chama cha Mapinduzi katiks suala la madini na mengineyo yote, kabla ya kusimama hadharani na kujitia kuwatusi watanzania kwamba wapuuzi kinatakiwa kutuomba radhi watanzania kwa uhalifu mkubwa na uhujumu uchumi wa nchi yetu tangu 1997 mpaka leo hii...
Polepole alitakiwa jana kuitumia nafasi ile kuliomba radhi taifa kwa chama chake kutubaka bila ridhaa yetu kwa miaka 18 mpaks leo katika raslimali zetu, lakini kwakuwa kijana keshakunywa madaraka ya kulevya basi kaishia kututukana tu huku akijiita ccm mpya.
Na Yericko Nyerere
Naona hata huelewi nini nimekiandika ila ndiyo hali tuliyonayo kwasasa wache Mkapa atuite wapumbafu maana ndiyo kipaji chetu watanzania.Ni lazima mkubali dude lenu limeoza siku nyingi, sasa linaendelea kuwanukia watanzania wote...
kaka tulisema hivyo hivyo baada ya list of shame lakini watanzania wakatuletea Magufuli. Angalia sana ulimi wako mkuu huzungumzii watanzania wote unazungumzia washabiki wa kisiasa waliojaa mitandaoni hata hapa JFMamilioni ya watanzania tayari wamesha wapuuza ccm
Yeye mwenyewe anajiita kijana, sasa tufanyeje?!Polepole sio kijana
Watanzaniakaka tulisema hivyo hivyo baada ya list of shame lakini watanzania wakatuletea Magufuli. Angalia sana ulimi wako mkuu huzungumzii watanzania wote unazungumzia washabiki wa kisiasa waliojaa mitandaoni hata hapa JF
is this view has anything to do with CHADEMAism?CHADEMA Ilikufa rasmi siku walipobadili gia angani na kumchukua Mr White hair na kumuacha Dr. Slaa
Mi nilishampuuza tangu alipokubali kuwa mkuu wa wilaya as if si yeye aliyekuwa akihubiri ITV wakati wa mchakato wa katiba mpya juu ya mamlaka ya rais na msururu wa viongozi wasio na kazi. Mnafiki sana kakaangu huyuWenye akili tulimpuuza hata kabla hajatoa hicho kijitamko chake.
Mmmmh.hyo kesi nyingine mkuu.Wakati tunaungana, ni vema pia tukajuwa kuwa aliyetufikisha hapo ni CCM na serikali yake.Na kwa kweli ili haya yasijirudie tena huko mbele njia pekee ni kuitoa CCM na serikali yake madarakani kwa namna yoyote kupitia sanduku la kura, ikishindikana hats kwa maombi tujaribu.
Ina maana umesahau kuwa Sumaye na lowasa ni wapinzani siku hizi!Acha uongo... Wapinzani wasiwe salama kwa uchafu uliofanywa na watu wengine? that is shit..
Tumuunge mkono Mhe.Rais kwa kupigania rasilimali za nchi zisipotee lakini tuzuie wajinga wachache wanaotaka kubeba jambo hili kisiasa. Nimemsikia Polepole akiwalaumu watanzania na viongozi wa dini eti wamekaa kimya wakati rasilimali za nchi zikiibiwa.Nimemsikiliza jana kijana mwenzangu ndugu Humphrey Polepole akizungumza kwa niaba ya ccm juu ya mambo kadhaa aliyoyaita makubwa nchini, mambo hayo ni mauaji ya Kibiti na Ripoti ya Makanikia.
Nimelazimika kulichambua hili kwa mtindo wa makala kwa nia ya kumkanya na kumwambia Polepole awe na adabu na heshima kwa Watanzania, sisi sio wajinga kama anavyotupimia kipimo alichonacho ambacho ni wanachama wenzake ndani ya ccm.
Nimesikitika kuona kijana huyu anawaita Watanzania ni wapuuza wale tunaounga mkono juhudi za rais huku tukihoji kwamba wizi wote huu katika raslimali umefanywa na Chama cha Mapinduzi, hivyo tukitaka makada wa chama hicho wasimvuruge Rais anapojaribu kupambana na hali hii.
Natataka nimrejeshe nyuma kijana huyu kwa lengo la kumfunza ama kumkumbusha na kisha kumkanya awe na adabu mbele ya umma hasa linapokuja suala la maslahi mapana ya nchi itikadi na mihemko yake iishie viunga vya Lumumba.
Mwaka 1998 wakati makampuni makubwa ya uchimbaji madini ya ASHANTI yalipoingia mikataba na serikali ya Tanzania iliyokuwa chini ya mwenyekiti wa ccm na rais wa Tanzania Benjamin William Mkapa, chama cha mapinduzi kililiridhia kwa kauli moja, serikali yake kuingia mikataba hiyo na kikahubiri hadharani kwamba taifa sasa linanufaika, Hivyo tunapohoji ushiriki na uratibu na unufaika wa ccm katika raslimali za nchi yetu, Polepole anapata wapi kibri chakutuita sisi wapuu?
Kwamfano Mgodi wa Golden Pride ambao umemaliza dhahabu yote tani 76 katika eneo la Lusu wilayani Nzega. Kampuni ya Resolute ya Australia iliwekeza dola 370 milioni kuanzia mwaka 1998 (mkataba wao ulisainiwa 25th June 1997). Katika kipindi cha uhai wa mgodi, miaka 14, Kampuni hii imeuza dhahabu ya thamani ya dola za kimarekani 3.3 bilioni, Muulizeni Polepole kama anafahamu kampuni hii ililipa mrahaba wa shingapi mpaka madini yalipoisha? Haya yote yamefanyika chini ya ccm
Lakini sivyo tu, rejea hansadi za Bunge juu ya hotuba za Upinzani zote tangu bunge la kwanza la vyama vingi, upinzani wamekuwa wakipiga kelele uwazi wa mikataba hii ambayo yote husainiwa Ikulu ya Tanzani, yani wizi wote mkubwa katika nchi hii huratibiwa Ikulu tangu Mwalimu Nyerere alipotutoka tu. Polepole anaweza kuwa hajui kwakuwa ameingia juzi kwenye siasa ya nchi hii anafikiri kuongoza ccm ni kuongoza zile NGOs zake za pale Mwenge za utetezi wa haki za mashoga.
Suala lingine alilozungumza Polepole na kujinasibu ni kiongozi wa chama cha watu ni suala la Mauaji ya Kibiti huku akimtisha Waziri wa Mambo ya Ndani na IGP katika taarifa yake. Na zaidi akajikita kutuhumu vyama vya siasa kwamba vimekaa kimya. Nataka nimkumbushe, vyama vya siasa havijakaa kimya, vyama vya siasa vina platform yake ya kutolea kauli za kitaifa na njia hii havipangiwi na chama kingine yaani chama cha kihalifu ccm,
Mauaji ya Kibiti ni uhalifu mkubwa, una kila elements za kubashiri aina zake, mauaji haya hayahitaji kukurupuka kisiasa, kwakuwa kwakufanya hivyo waweza kujikuta yanageuzwa kuwa matukio ya kisiasa au ya kidini kws vyovyote yanavyoweza kuchukuliwa, Yanahitaji vyombo vya kiuchunguzi ndivyo vishughulike nayo, na sio matamko ya kisiasa kama polepole anavyotaka iwe, wala hayahitaji matamko ya kidini labda katika muundo utakao kutanisha imani zote pawe na sauti moja, nje ya hapo yatajengwa mazingira na kuitwa mauaji ya kidini. Polepole kwa mambo haya ni mchanga, walionyamaza na kuacha vyombo vya dola vifanye kazi anawaona wapuuzi ile yeye ndiye mjanja na mzalendo,
Nataka nimkumbushe tu katika utawala wake ccm, Anafahamu kwamba Ben Saanane maarufu kama Ben-Rabiu Wa Saanane ni mwezi wa sita huu amepotea/ametekwa? Ipo wapi kauli ya chama chake katika hili?
Anafahamu kwamba Bagamoyo miili saba iliokotwa kwenye viroba ikazikwa pembeni ya mto mithiri ya mbwa? Ipo wapi kauli ya chama yeye akiwa msemaji? Anafahamu kwamba Lugumi imekiuka mkataba wa makubaliano na wizara ya mapolisi juu ya ufungaji ya mitambo ya kielekroniki vituo vya polisi na kampuni hiyo ilishalipws pesa zote kufunga vituo zaidi ya 200 lakini mpaka dakika hii ni vituo vinne tu ndivyo vimefungwa? Ipo wapi kauli ya chama yeye akiwa msemaji? Mnafiki mkubwa huyu..
Manunuzi ya Ndege, ujenzi wa barabara za Mwenge > Moroko, Mwanza Airport nk zimeidhinishwa cha Bunge lipi nchini? Ipo wapi kauli ya chama katika hili yeye akiwa ni msemaji?
Namsihi sana Polepole awe na adabu mbele za Watanzania, Chama cha Mapinduzi katiks suala la madini na mengineyo yote, kabla ya kusimama hadharani na kujitia kuwatusi watanzania kwamba wapuuzi kinatakiwa kutuomba radhi watanzania kwa uhalifu mkubwa na uhujumu uchumi wa nchi yetu tangu 1997 mpaka leo hii...
Polepole alitakiwa jana kuitumia nafasi ile kuliomba radhi taifa kwa chama chake kutubaka bila ridhaa yetu kwa miaka 18 mpaks leo katika raslimali zetu, lakini kwakuwa kijana keshakunywa madaraka ya kulevya basi kaishia kututukana tu huku akijiita ccm mpya.
Na Yericko Nyerere