Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, amesema ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakuna utamaduni wa kuvuana nguo hadharani, bali kuna utamaduni wa kukosoana kwa lengo la kujenga chama.
"Tunakosoana kwenye vikao" haipaswi kutumiwa kuzuia wengine kutoa maoni yao waziwazi, kwani si wote wanashiriki vikao hivyo. Ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa CCM, mfano bora wa kukosoa ulikuwa Mwalimu Julius Nyerere pamoja na Mzee Karume, ambao waliwahi kutoa maoni yao hadharani hata walipoona mambo hayaendi vizuri ndani ya chama.
Polepole amesema haileti maana mtu kujiona ni mwana CCM zaidi ya Mwalimu Nyerere, ambaye mwenyewe aliwahi kukosoa hadharani kwa nia ya kujenga.
"Tunakosoana kwenye vikao" haipaswi kutumiwa kuzuia wengine kutoa maoni yao waziwazi, kwani si wote wanashiriki vikao hivyo. Ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwa CCM, mfano bora wa kukosoa ulikuwa Mwalimu Julius Nyerere pamoja na Mzee Karume, ambao waliwahi kutoa maoni yao hadharani hata walipoona mambo hayaendi vizuri ndani ya chama.
Polepole amesema haileti maana mtu kujiona ni mwana CCM zaidi ya Mwalimu Nyerere, ambaye mwenyewe aliwahi kukosoa hadharani kwa nia ya kujenga.