Pole sana dada

Pole sana dada

Ni kweli mabinti wa kazi za ndani wanakabiliwa na matatizo mbali mbali ktk kazi zao.Ukatili na ujira mdogo ni sehemu ya matatizo yao.Lakini ukatili kuhamishia kwa viumbe vinyonge kama watoto hii haikubaliki.Tafuta kulipa kisasi kwa hao hao mabosi lakini si watoto.Hii siungi mkono kamwe.....
 
Yani kwa hapo huyo bint amekosea ange deal na wazazi sio mtoto,na hakulazimishwa kazi ukiona sehemu kuna mateso unaondoka atakua ana mamtatizo ya akili sio bure.....

Ulishawahi kutendewa unyama na mtu halafu ukaondoka tu?

Maana binadamu tunajidai ni watakatifu sana wakati na sisi ni wale wale tu ....!!
 
Najua na nimelisema hilo kuwa hakuna kitendo ambacho kinahalalisha alichofanya huyo dada.lakini tatizo latu mara nyingi tunaangalia tulipoangukia na sio tulipojikwaa,inawezekana kabisa huyu dada kilichomfanya akafanya haya ni matokeo ya mateso,yes inawezekana alitakiwa kuondoka tu,je unajua kama hata njia ya kwao anaijua?

Kuna wadada wengine wanachukuliwa huko na kuja kupatiwa makazi kama haya na wanakuwa kama wapo kisiwani tu na hawana cha kufanya,lakini pia hata kama kingekuwepo cha kufanya kwa maana ya kuondoka,yule dada ni binadamu kama wengine,ukifanyiwa ubaya na ukatili kunakuwa na hali ya kutamani kisasi,hiyo ni kawaida kwa binadamu,mara nyingi huyu dada aaliona hawezi kuwaadhibu waajiri wake [kama walimfanyia ubaya] na aliona mnyonge wake ni huyu mtoto masikini ya Mungu]

Huyu mtoto anakuja kuwajibika kwa makosa ya waajiri wake,binti akaamua kumfanya alivyofanya,lengo langu sio kumuondoa huyu binti hatiani bali kujaribu kuangalia wengine ambao walisababisha hili tukio kwa namna moja au nyingine nao kuwajibika na sio kumfanya huyu binti mbuzi wa kafara na kumfanya ndio shetani kuliko shetani mwingine ambae anazunguka tu kwa raha zake na ndio aliyesababisha kwa hakika tukio hili!

mkuu kwa kiasi fulani nimekuwa na mwelekeo kama wewe.Wengi wetu tunaona watoto wa kazi ni kama watu fulani ambao hawastahili. Kuna baadhi ya familia ambazo watoto wa kazi hawajawahi kukaa meza moja na waajiri wao wakala siku zote wanakula jikoni au wanasubiri wamalize kula then wao yeye aanze kula hii inaweza ikawa ndo hatua mojawapo ya kuwaadhiri kisaikolojia hawa watu.Pili watoto wa kazi nao ni binadamu kama sie watoto wengi wanakopwa hela zao na nyingine hawalipwi kwa wakati wakati wewe ukikosa mshahara mwezi unaanzisha migomo.Hivyo ni rai yangu tuwatendee watoto wa kazi kama nasi tunavyotaka watutendee tukipandishwa mishahara au bisahara zinanawiri pia na sie tuwaongezee mishahara.Kama unaweza anza kukaa na wadada wa kazi meza moja mnakula pamoja na ikiwezekana na yeye aanze kuchukua chakula uone mafanikio au mabadiliko katika kuwatunza watoto wetu
 
So me being me, I'm curious now....

Huyo dada naye keshasema ya upande wake?

Sidhani kama anaweza hata kupewa hiyo nafasi ya kusema....hata akiongea ataonekana anaongea kichina tu kwa sababu tulishamhukumu tukamuona ni shetani. Lakini mimi naamini kuna mambo yapo nyuma ya pazia pale si bure
 
Unakuta jitu nene limekaa linaangalia tamthilia halafu eti hata maji ya kuoga linataka lichemshiwe na liwekewe bafuni.

Like seriously?
Na hapa ndipo matatizo yanapoanzia, kila mtu ataka kuwa "bosi". Hata kuandaa chakula cha jioni baada ya kazi, maji ya kuoga ni tatizo.
 
Bora umeliona hata hili!

Sasa huoni kama njia aliyotumia huyo binti kushout out (juu ya 'kuteswa' kwake) imekuwa ni tatizo zaidi ya kuteswa? Imagine kwenda jela na kunyea debe wakati angeweza hata kutoroka akaiba say pesa au vitu ajilipe kama alikuwa hata mshahara halipwi.
 
Sidhani kama anaweza hata kupewa hiyo nafasi ya kusema....hata akiongea ataonekana anaongea kichina tu kwa sababu tulishamhukumu tukamuona ni shetani. Lakini mimi naamini kuna mambo yapo nyuma ya pazia pale si bure

Na huo ndo ubaya.

Ndo maana mimi nimemwelewa kabisa Eiyer.
 
Dude, kuna video ingine binti anamfanyisha katoto ka kiume matendo machafu machafu hadi kichefu chefu. Huyo nae aliteswa akapata nyege za kukifanyia kitoto kichanga ufuska kama ule?
Matatizo ya hawa wadada huwa yana chanzo zaidi ya kimoja,ni jukumu la mwajiri kukagua mtu anaemuajiri kumlelea mwanae ni mtu wa aina gani

Huyo ambae anafanya kitendo hicho bosi wake anaweza kuwa chanzo kwa maana moja au nyingine,kumyima binti yako wandani haki yake ya kuwa na mahusiano ni kosa na linaweza kuleta mambo haya,lakini pia bado inaweza kuwa chanzo sio hiki pekee ...
Unaposema dada hakuwa kichaa una maana vichaa ni akina nani? wanaotembea mtaani? walio spitali wamefungwa chains ama unaongea ukibase on just one type of insanity.
Hapana,nimesema kuwa huyu dada kama angekuwa ni kchaa basi asingekaa nao muda wote huo,lakini pia hata kama mfano angekuwa ni kichaa basi huyo mwajiri wake asingekuwa na haki ya kumuadhibu namna ile kwasababu huyu alifanya hivi bila ridhaa yake lakini pia bado huyu mwaajiri wake anatakiwa apewe kibano kwa kutokukagua huyu mtu ana background gani kabla ya kumpa dhamana ya kulelea mtoto

Yote yanamrudia tu .....
We have to accept blame when we are wrong and strive to change things.... this blame shifting games wont land us anywhre.
Sina lengo la kumbebesha lawama asiestahili,nimesema na ninasema kuwa huyo dada kama ni mzima kiakili ni lazima awajibike kwa makosa yake,lakini kama kuna mtu mwingine ambae nae anaweza kuhusika kwa namna mopja au nyingine nae awajibike pia ....
By the way, as long as am paying you decently and treating you right, I am under no obligation to go the extra mile. Thats a job like any other.
Unamlipa kiasi gani?

Kinatosha?
P/s. Sorry if it appears am furious but kama nilivyosema kwenye thread yangu binti alimtishia mwanangu kumchinja na kisu silu ya nne kazini. Mfano silumsilia? Na hapo sijamsema acha kumnyooshea kidole.
Sijui kama hata ulikagua sababu iliyopelekea hilo kutokea ......!!
 
Mbona kauli na thread yako inaonesha kuhalalisha alichokitenda huyo mdada wa kazi?

Oa uzae halafu uwe na uhitaji wa maid tuone kama utawaita pumbaf watakaomlaumu maid wako akimuambikiza ukimwi kwa makusudi your lil Junior

Hujaelewa nilichoandika,soma upya ....!!
 
Nlichangia katika uzi uliopita kuwa lazima watu tufikirie nje ya box kwa tukio hili na pia kujifunza haswa tukiangalia hali halisi..ila wakurupukaji wakatukana sana,wanakuambia hata kama binti alikuwa anateswa ila hakutakiwa kumfanyia mtoto vile,sasa unajiuliza kama unakiri kuwa hata kama alikuwa anateswa ila hakutakiwa kufanya vile,ulitaka aweke sumu kwenye chakula au apige nyumba nzima kiberiti akiwa amefunga milango usiku auwe wote sasa??...nikupongeze mtoa mada na wengine kwa kuliangalia hili kwa mapana yake,watu wengi wenye fikra fupi huamua jambo kwa kuangalia matokeo badala ya mzizi wake...bado nasema siungi mkono kitendo chochote cha uhalifu dhidi ya binadamu..

Mkuu we acha tu ....

Kama watu wanaona kuwa sio sawa huyo binti kufanya hayo,je wanaona sawa yale ambayo binti amefanyiwa? [kama yapo]

Huku hawagusi kabisa

Nasema hivi,kila mtu awajibike kwa uhalifu alioufanya na sio mmoja kuonekana malaika na mwingine aonekane shetani kwa kitendo kile kile!
 
Sasa huoni kama njia aliyotumia huyo binti kushout out (juu ya 'kuteswa' kwake) imekuwa ni tatizo zaidi ya kuteswa? Imagine kwenda jela na kunyea debe wakati angeweza hata kutoroka akaiba say pesa au vitu ajilipe kama alikuwa hata mshahara halipwi.

Hindsight is 20/20!

But without hearing from the girl it would be impossible for us to discern what was really going on in that household that perhaps made her go postal.

It's very possible she wasn't in the right frame of mind.
 
Yan huna hata haya unaona alichomtendea malaika huyo ni haki? Huo ni upuuzi, cdhan kma wew ni great thinker! Hata kma boss kamuudhi ndo amdhuru mtoto??? haiingii akilini. Unajua mtoto wangu ameniumaje? Me mwenyew kumpga mwanangu naogopa af just a maid aje anifanyie hivyo mwanangu??? Mfyuuu!! Nakunyonga kwa mkono wangu
 
Yan huna hata haya unaona alichomtendea malaika huyo ni haki? Huo ni upuuzi, cdhan kma wew ni great thinker! Hata kma boss kamuudhi ndo amdhuru mtoto??? haiingii akilini. Unajua mtoto wangu ameniumaje? Me mwenyew kumpga mwanangu naogopa af just a maid aje anifanyie hivyo mwanangu??? Mfyuuu!! Nakunyonga kwa mkono wangu

Mkuu sidhani kama kuna mtu amehalalisha hapa. Anachojaribu kuelezea mtoa mada ni kuwa makini jinsi mnavyowatreat hawa mabinti. Tenda wema utendewe
 
Yan huna hata haya unaona alichomtendea malaika huyo ni haki? Huo ni upuuzi, cdhan kma wew ni great thinker! Hata kma boss kamuudhi ndo amdhuru mtoto??? haiingii akilini. Unajua mtoto wangu ameniumaje? Me mwenyew kumpga mwanangu naogopa af just a maid aje anifanyie hivyo mwanangu??? Mfyuuu!! Nakunyonga kwa mkono wangu

Hivi wewe umeelewa hata kilichoandikwa?

Stop reacting viscerally. Try to read and understand.
 
huyo binti ni mkatili tu.....wapo wengi wa aina hio wana abuse watoto bila yao wao kuteswa na wana familia, maids ni watu kama sisi kuna wakatili na wema huyu ni KATILI I CALL HER MNYAMA.....nimelelewa na madada hawa na nawapenda na kuwaheshimu ila huyu ni mnyama....ukatili wa wazazi hauwezi kumsukuma binadamu wa kawaida kumuadhibu mtoto yule kiasi hiki....ange revenge kwa wazazi in one way or another ningeweza kuelewa hio kulipiza kisasi lakini kwa kale katoto,ni ukatili tu.

Alichokifanya huyo jamaa baada ya kuona alichofanyiwa huyo mtoto ni cha kibinadamu sio?
 
Nyuzi za hapa zote mita mia mbili, du, nitarudi
 
Eiyer umesema 'kama yapo' maana yake hatuna uhakika ni speculation tu. Tufanyie kazi speculation? Ilhali kuna some ugly facts tayari.

Of course sheria itafuata mkondo na ndio maana kuna wanasheria wa serikali.

Wito ambao ungeutoa ni kuwe na ngo ambayo inafuatilia kwa karibu maslahi na haki za wadada wa kazi. Au hata desk police kama ilivyo kwa desk la gender violence.. lkn kumtetea binti kwa assumption kwa kitendo kile ni kitu ambacho binafsi sikiungi mkono.
ungekuwa mmama mwenye watoto na unapata adha ambayo watu wanaipata kidogo ningekuelewa

Nani ameshampa huyo dada nafasi hata ya kujitetea ili dunia ijue upande wa pili wa shilingi?

Nani hata amemkamata huyo jamaa ambae ni tajiri wa huyo dada kwa kipigo alichompa huyo dada?

Kama tunakubali ni ubinadamu tu uliompelekea huyo mwajiri kumpiga huyo dada ni kwanini huo ubinadamu tunauondoa kwenye suala la huyu binti na tunamuona ni shetani?

Hiyo "speculation" inawezekana kabisa kwa silimia nyingi ikawa ni kweli .....!!
 
Back
Top Bottom