Pole sana dada

Pole sana dada

Yani kwa hapo huyo bint amekosea ange deal na wazazi sio mtoto,na hakulazimishwa kazi ukiona sehemu kuna mateso unaondoka atakua ana mamtatizo ya akili sio bure.....
 
Mkuu hii kitu inaniuma sana

Binadamu tumefikia kiwango cha hatari sana cha kuona kama sisi ni binadamu lakini wengine asio binadamu .....

Aaaaaaahhhhh ......!!

Mimi umenifurahisha kwa walau kujaribu kutenda haki kwa kuangazia na upande wa pili.

Super big up.
 
"mabosi" wengi huwa ni wakatili kuliko tunavyodhani. Hawa hawa wanaolaani kitendo cha huyu dada kumfanyia unyama malaika huyu, wengi ni wakatili tena kupitiliza kwa wasaidizi wao majumbani huku wakiwalipa as low as 20,000tsh kwa mwezi, huku wakifanyishwa kazi kuliko punda. Hayo nimewahi kuyashihudia.

I can vouch for that!

Nimeshashuhudia wadada wa kazi wakinyanyaswa sana na mabosi wao (baadhi ya ndugu zangu).

Unakuta jitu nene limekaa linaangalia tamthilia halafu eti hata maji ya kuoga linataka lichemshiwe na liwekewe bafuni.

Like seriously?
 
Dude, kuna video ingine binti anamfanyisha katoto ka kiume matendo machafu machafu hadi kichefu chefu. Huyo nae aliteswa akapata nyege za kukifanyia kitoto kichanga ufuska kama ule?

Unaposema dada hakuwa kichaa una maana vichaa ni akina nani? wanaotembea mtaani? walio spitali wamefungwa chains ama unaongea ukibase on just one type of insanity.

We have to accept blame when we are wrong and strive to change things.... this blame shifting games wont land us anywhre.

By the way, as long as am paying you decently and treating you right, I am under no obligation to go the extra mile. Thats a job like any other.

P/s. Sorry if it appears am furious but kama nilivyosema kwenye thread yangu binti alimtishia mwanangu kumchinja na kisu silu ya nne kazini. Mfano silumsilia? Na hapo sijamsema acha kumnyooshea kidole.
 
chochote kile haki-justify kitendo alichofanya yule dada.....kama aliona mateso yamezidi angeondoka,wapo madada wengi tu wanateswa mwisho wanatoroka au wanaomba kuondoka.....kitendo alichofanya ni cha kinyama na anastahili adhabu kali.

Najua na nimelisema hilo kuwa hakuna kitendo ambacho kinahalalisha alichofanya huyo dada.lakini tatizo latu mara nyingi tunaangalia tulipoangukia na sio tulipojikwaa,inawezekana kabisa huyu dada kilichomfanya akafanya haya ni matokeo ya mateso,yes inawezekana alitakiwa kuondoka tu,je unajua kama hata njia ya kwao anaijua?

Kuna wadada wengine wanachukuliwa huko na kuja kupatiwa makazi kama haya na wanakuwa kama wapo kisiwani tu na hawana cha kufanya,lakini pia hata kama kingekuwepo cha kufanya kwa maana ya kuondoka,yule dada ni binadamu kama wengine,ukifanyiwa ubaya na ukatili kunakuwa na hali ya kutamani kisasi,hiyo ni kawaida kwa binadamu,mara nyingi huyu dada aaliona hawezi kuwaadhibu waajiri wake [kama walimfanyia ubaya] na aliona mnyonge wake ni huyu mtoto masikini ya Mungu]

Huyu mtoto anakuja kuwajibika kwa makosa ya waajiri wake,binti akaamua kumfanya alivyofanya,lengo langu sio kumuondoa huyu binti hatiani bali kujaribu kuangalia wengine ambao walisababisha hili tukio kwa namna moja au nyingine nao kuwajibika na sio kumfanya huyu binti mbuzi wa kafara na kumfanya ndio shetani kuliko shetani mwingine ambae anazunguka tu kwa raha zake na ndio aliyesababisha kwa hakika tukio hili!
 
chochote kile haki-justify kitendo alichofanya yule dada.....kama aliona mateso yamezidi angeondoka,wapo madada wengi tu wanateswa mwisho wanatoroka au wanaomba kuondoka.....kitendo alichofanya ni cha kinyama na anastahili adhabu kali.

No one is trying to justify it, at least not Eiyer.

But at the same time it would be remiss to ignore the fact that most of those maids are maltreated by their bosses.

So if we are going to condemn the cruelty of the maids let's also condemn in equal measure, the cruelty of the bosses.

It's only fair.
 
Last edited by a moderator:
Mbona kauli na thread yako inaonesha kuhalalisha alichokitenda huyo mdada wa kazi?

Oa uzae halafu uwe na uhitaji wa maid tuone kama utawaita pumbaf watakaomlaumu maid wako akimuambikiza ukimwi kwa makusudi your lil Junior
 
Kulaani kitendo alichofanyiwa innocent victim ni reaction ya kibinadamu.
Sawa .....
kujiuliza how na why inakuja baadaye sana. Na kama wewe ambavyo umeamua kubase upande wa msichana wa kazi mimi na wengine wengi tumeamua kujikita kwanza kwa innocent victim.
Tatizo la kwanza linaonekana hapa,sijabase kokote ila nataka kila mmoja alione tatizo kwa mapana yake

Binti awajibike kwa tatizo lake na kama hao waajiri wa huyo binti wana matatizo yao na kimsingi kama yapo ndio yatakuwa chanzo basi nao wawajibike kama binti anavyowajibika kwa kupakwa matope na kuonekana kama sio binadamu
Tunazo facts mezani ambazo ni mtoto kateswa kwa vipigo ambavyo ni vya kuua. Na pia reaction ya mzazi baada ya kukutana na hiyo fact, kweli mzazi aligeuka mnyama pia lkn nani asingegeuka mnyama kwa hali ilivyokuwa?
Kutokuwepo kwa mtu ambae asingekuwa mnyama hakuhalalishi unyama alioufanya huyo mwajiri wake na inawezekana tatizo limeanzia kwake ...
speculation ni kuwa binti ameteswa sana na kuamua kumalizia hasira zake kwa mnyonge (innocent victim ). Je ni njia sahihi kufanya aliyoyafanya?
Sio njia sahihi na ndio maana nimesema kuwa sheria ichukue mkondo wake,lakini ni kwanini hamjadili kama aliteswa huyo mtesaji nae achukuliwe hatua?
wanaokutwa na hali kama hiyo hufanya nini? Kwanini asiondoke au asiende police?
Swali hili muulize huyo mwajiri wake kuwa baada ya kuona hilo tukio ni kwanini asingeenda polisi na akaamua kujichukulia sheria mkononi?
Suala la kumalizia hasira waliodhaifu kuliko wewev sio jema kabisa. Nakumbuka mama alishanipiga sana kisa ameudhiwa na mama mkwe wake na wifi zake, of recent nilimkumbushaa au umeudhiwa kazini unakuja mpiga mkeo sio fair.
Sawa lakini pia waliolianzisha nao wachukuliwe hatua ...
Anger management inahitajika kwa watu wengi. Yes binadamu anaweza kuwa shetani inahitaji trigger ndogo tu. So yule binti jwa wakati ule alikuwa shetani, na baba mtoto alikuwa shetani pia.
Sawa .......!!
 
No one is trying to justify it, at least not Eiyer.

But at the same time it would be remiss to ignore the fact that most of those maids are maltreated by their bosses.

So if we are going to condemn the cruelty of the maids let's also condemn in equal measure, the cruelty of the bosses.

It's only fair.

THATS A NO-BRAINER....but what about those maids who are not mistreated but still end up abusing toddlers???
 
THATS A NO-BRAINER....but what about those maids who are not mistreated but still end up abusing toddlers???

Then they are what they are, period, end of sentence.

I'm all about fairness.

*Please, instead of toddlers let's use (young) children*
 
Nlichangia katika uzi uliopita kuwa lazima watu tufikirie nje ya box kwa tukio hili na pia kujifunza haswa tukiangalia hali halisi..ila wakurupukaji wakatukana sana,wanakuambia hata kama binti alikuwa anateswa ila hakutakiwa kumfanyia mtoto vile,sasa unajiuliza kama unakiri kuwa hata kama alikuwa anateswa ila hakutakiwa kufanya vile,ulitaka aweke sumu kwenye chakula au apige nyumba nzima kiberiti akiwa amefunga milango usiku auwe wote sasa??...nikupongeze mtoa mada na wengine kwa kuliangalia hili kwa mapana yake,watu wengi wenye fikra fupi huamua jambo kwa kuangalia matokeo badala ya mzizi wake...bado nasema siungi mkono kitendo chochote cha uhalifu dhidi ya binadamu..
 
umemtazama dada kwa jicho ulilomtazama yule aliyekupa kisa chake. Pole anatakiwa kupewa mtoto na si kuhalalisha ukatili kwa mtoto, ila si vibaya kutoa angalizo kwa namna tunavyowafanya wafanyakazi wa ndani. Dada wa kazi anaweza kuwa na ugonjwa wa akili ukalipuka siku isiyojulikana. Wapo wadada wa kazi wanaoteswa lakini hawawakatili watoto. Wapo ambao hawateswi na waajiri ila wana visirani vinavyotokana na sababu nyingi zikiwamo za kimapenzi - kaachwa na bwana basi hasira kwa mtoto. Wengine wanafanya hizi kazi kwa sababu hawana namna, wamefungashwa na wazazi kuja mjini. Hata uwape nini bado wananuna tu na kazi wanafanya wanavyotaka. Unabembeleza housegirl mpaka unajishtukia. Nimeshakutana nao. Kwa hiyo sababu za ukatili wa wadada wa kazi nyingi.
Pamoja na haya uliyosema bado unamuweka mwajiri kwenye hatia,mwenye jukumu la kukagua ni mtu wa aina gani anamuajiri ni mwajiri na sio mwajiriwa,kama utaajiri kichaa wewe iliemuajiri ndio unapaswa kuanza kupatiwa kibano kabla ya huyo kichaa uliemuajiri

Dada niliyeweka kisa chake kwenye mada nimemtumia kama back up tu na sio sababu ya kuhalalisha klitendo cha huyu dada
Nimewahi kuwa na housegirl mkatili kwa mtoto. Hakuwahi kuonyesha kuwa na roho mbaya. kwa miezi mitatu aliyokaa nilijitahidi kumpa mahitaji yote muhimu. Anakula ninachokula mimi jioni, mchana anakula anachotaka yeye maana sipo. Analala kwenye chumba chake mwenyewe na malazi ni masafi. Jumapili anaenda anakojua yeye kwa mapunziko. Jumapili moja akanirudia saa 5 usiku. Nikauliza kulikoni nikadanganywa nilivyodanganywa maisha yakaendelea.

Mtoto wangu wakati huo akiwa na mwaka na miezi 3 alikuwa mbishi wa kula na kulala. Yule dada akawa ananiambia wewe anakusumbua sana. Mimi wala hanisumbui. Nikachukulia watoto wote hudeka wakiwa na mama zao. Kuna kipindi nikawa nikirudi home mtoto anaenda jikoni ananiletea kiboko usawa wa rula hivi. Wakati huo hawezi kuongea vizuri. Ananionyesha kile kiboko lakini nilivyokuwa mpuuzi hata sikufikiria kama kilikuwa kinamhusu. Siku moja nikiwa namnyonyesha akawa anapeleka sana mkono makalioni. Wakati nambadilisha diaper nakuta kuna mstari umevimba. Nikashangaa, nikamwita dada kumuonyesha akaniambia labda mdudu. Nikajiuliza huyu mdudu gani anapita kama rula. Kwa umri wa mtoto na upole wa dada sikuwaza habari ya kuchapwa. Siku ya siku jirani akaniita na kunipa habari kuwa mtoto wangu anachapwa sana na msichana wa kazi. Sikuwa na sababu ya kubisha maana dalili nilishaziona nikapuuza. Nikarudi nyumbani nikamtimua yule binti.

Kutokana na huo uzoefu wangu siwezi kusema moja kwa moja kuwa mayaya wanakatili watoto kwa sababu nao wakakatiliwa na waajiri. Mwajiri anaweza kumlamba miguu yaya na bado yaya akafanya vituko. Ukatili hutokana na "frustration" inayotokana na mtu kutofikia malengo yake fulani. Tuliangalie hili swala kwa upana zaidi. Ila kama mnataka tuangalie sababu moja ya waajiri, sawa.
Kesi hii ni kesi ambayo nayo ina historia yake,kuishi vizuri na hawa wadada sio kuwapa chakula na malazi tu,unatakiwa uwe rafiki yake na ujaribu kuwa kama mama,dada au hata rafiki yake wa karibu sana ili uweze kuzungumza nae na aweze kukuambia shida zake nyingi

Hawa watu wanatoka kwenye mazingira ya aina tofauti sana,kitendo cha kumuacha na mwanao,akufulie,akupikie na mengine kama hayo ni mambo muhimu sana ambayo yanapaswa kufanywa na mtu muhimu sana,huyu sio wa kudharau hata kidogo!
 
Najua na nimelisema hilo kuwa hakuna kitendo ambacho kinahalalisha alichofanya huyo dada.lakini tatizo latu mara nyingi tunaangalia tulipoangukia na sio tulipojikwaa,inawezekana kabisa huyu dada kilichomfanya akafanya haya ni matokeo ya mateso,yes inawezekana alitakiwa kuondoka tu,je unajua kama hata njia ya kwao anaijua?

Kuna wadada wengine wanachukuliwa huko na kuja kupatiwa makazi kama haya na wanakuwa kama wapo kisiwani tu na hawana cha kufanya,lakini pia hata kama kingekuwepo cha kufanya kwa maana ya kuondoka,yule dada ni binadamu kama wengine,ukifanyiwa ubaya na ukatili kunakuwa na hali ya kutamani kisasi,hiyo ni kawaida kwa binadamu,mara nyingi huyu dada aaliona hawezi kuwaadhibu waajiri wake [kama walimfanyia ubaya] na aliona mnyonge wake ni huyu mtoto masikini ya Mungu]

Huyu mtoto anakuja kuwajibika kwa makosa ya waajiri wake,binti akaamua kumfanya alivyofanya,lengo langu sio kumuondoa huyu binti hatiani bali kujaribu kuangalia wengine ambao walisababisha hili tukio kwa namna moja au nyingine nao kuwajibika na sio kumfanya huyu binti mbuzi wa kafara na kumfanya ndio shetani kuliko shetani mwingine ambae anazunguka tu kwa raha zake na ndio aliyesababisha kwa hakika tukio hili!

huyo binti ni mkatili tu.....wapo wengi wa aina hio wana abuse watoto bila yao wao kuteswa na wana familia, maids ni watu kama sisi kuna wakatili na wema huyu ni KATILI I CALL HER MNYAMA.....nimelelewa na madada hawa na nawapenda na kuwaheshimu ila huyu ni mnyama....ukatili wa wazazi hauwezi kumsukuma binadamu wa kawaida kumuadhibu mtoto yule kiasi hiki....ange revenge kwa wazazi in one way or another ningeweza kuelewa hio kulipiza kisasi lakini kwa kale katoto,ni ukatili tu.
 
Binti awajibike kwa tatizo lake na kama hao waajiri wa huyo binti wana matatizo yao na kimsingi kama yapo ndio yatakuwa chanzo basi nao wawajibike kama binti anavyowajibika kwa kupakwa matope na kuonekana kama sio binadamu


Sio njia sahihi na ndio maana nimesema kuwa sheria ichukue mkondo wake,lakini ni kwanini hamjadili kama aliteswa huyo mtesaji nae achukuliwe hatua?

Swali hili muulize huyo mwajiri wake kuwa baada ya kuona hilo tukio ni kwanini asingeenda polisi .!!

Eiyer umesema 'kama yapo' maana yake hatuna uhakika ni speculation tu. Tufanyie kazi speculation? Ilhali kuna some ugly facts tayari.

Of course sheria itafuata mkondo na ndio maana kuna wanasheria wa serikali.

Wito ambao ungeutoa ni kuwe na ngo ambayo inafuatilia kwa karibu maslahi na haki za wadada wa kazi. Au hata desk police kama ilivyo kwa desk la gender violence.. lkn kumtetea binti kwa assumption kwa kitendo kile ni kitu ambacho binafsi sikiungi mkono.
ungekuwa mmama mwenye watoto na unapata adha ambayo watu wanaipata kidogo ningekuelewa
 
Yani kwa hapo huyo bint amekosea ange deal na wazazi sio mtoto,na hakulazimishwa kazi ukiona sehemu kuna mateso unaondoka atakua ana mamtatizo ya akili sio bure.....

Sio wasichana wote wanao teswa na Wenye nyumba hufikiri kwa haraka bora waondoke! Wengi wao kutokana na shida walizo nazo wanaona bora wabaki lakini kama tujuavyo binadamu muda mwingine tunakuwa kama wanyama hivyo nao wanahamua kuwafanyia watoto wetu!

Mtoa mada ana lengo la kutufanya tufikiri upande mwingine wa waajiri wao na ni wangapi huwatendea vyema hawa watoto wa watu tunao waleta watusaidie kazi zetu?

Kwakweli huyu Dada wa Uganda amepitiliza na amefanya kitendo cha kikatili sana na hakikubaliki kabisa!

Lakini Mimi nataka tujaribu kufikiri nje ya haya yaliyo tokea maana unaweza kutwa liteswa sana ndio akaona na yeye amalize hasira zake japo hili halikuwa suluhu!
 
Umenena Eiyer! Nilipo ona hile video kwa Mara ya kwanza nilisikitika sana na ni video ambayo siwezi kurudi kuangalia maana inasukitisha sana mtoto kufanyiwa vile!

Lakini baadae nilianza kujenga picha juu ya hili tukio!
Kwanza ningekuwa Mimi cha kwanza ninge hitaji apimwe akili yule binti Maana nilijenga picha ya mtu mwenye tatizo la akili!

Pili nilijenga picha ya binti wa kazi anaye teswa sana na wenye nyumba hivyo analipiza kisasi kwa mtoto wa wanao mtesa na kumnyanyasa!

Pia nilijenga picha yakuwa huyu binti huteswa sana na Mama mwenye nyumba kiasi kwamba amepata tatizo la kisaikolojia na la kiakili maana tumezoea ni kawaida Wamama walio wengi kuwanyanyasa wafanyakazi!

Kwakweli nilikosa jibu nilipo pata taarifa kuwa huyu mtoto alikuwa anaishi na baba yake pamoja na housegirl tuu!

Bado niliendelea kujiuliza ni lini Mama mwenye nyumba aliachana na Mumewe kama walishawai kuishi pamoja?

Mama mwenye nyumba hakuwai kuishi na huyu binti wa kazi kabla ya kuondoka?

Nini hufanyiwa huyu mfanyakazi na Baba mwenye nyumba na wana maahusiano gani na mfanyakazi?

Nilijiuliza hayo Maswali kwakuwa asilimia 99% ya mateso ya wadada wa kazi huyapata kwa wa Mama wenye nyumba!
Na kuhakikishia kabisa kati ya wanawake 100 ni wanawake 3 wanaweza ishi na wafanyakazi wa ndani kama watu muhimu kwao!


Katika hili ni wazi kabisa kuna sababu za msingi kabisa yule mfanyakazi kufanya yale kama itathibitika hana tatizo la kisaikolojia au la kiakili! Wafanyakazi wandani wananyanyaswa sana tena uzuri Mimi nimeshuhudia sana hili lakini ukisema unaonekana una interest!

Yani unakuta hawapewi muda wa kupumzika na mshahara bado mdogo na wengine wana kopwa kabisa hadi mshahara!

Wafanyakazi hawa wanateswa sana na wanao watesa ndio hao hao huwa wakwanza kusema wana uchungu sana na huruma sana kumbe ni unafiki tuu!

Kwakweli kitendo alicho mfanyia mtoto hakikubaliki lakini kwa upande mwingine hawa watu nao hupata mateso sana kwa sisi wenyewe tunao laani kitendo chake!

Mkuu kuna wababa wengine ni wakatili kuliko hata wamama

Wanawabaka na kuwaingilia kinyume na maumbile hawa mabinti tena bila ridhaa yao .....

Ni hatari mkuu .....!!
 
Yani kwa hapo huyo bint amekosea ange deal na wazazi sio mtoto,na hakulazimishwa kazi ukiona sehemu kuna mateso unaondoka atakua ana mamtatizo ya akili sio bure.....

Unadeal vipi na mtu mzima mwenzio ambae pengine hata kumsogelea tu uongee nae neno moja tu unatakiwa ujipange wiki nzima??
 
So me being me, I'm curious now....

Huyo dada naye keshasema ya upande wake?
 
Back
Top Bottom