Points 10 za ujenzi: Unyevu/damp katika jengo

greater than

JF-Expert Member
Sep 22, 2018
786
1,219
MAKALA YA 3
Karibu katika Makala yenye kuelimisha mambo muhimu kuhusiana na ujenzi wa Majengo.
Leo,tutaangazia juu ya DAMPNESS/Unyevu katika jengo.
Hili ni jambo linalokumba Majengo nchi nzima.

1.Dampness/ Unyevu jengoni: Hii ni hali ambayo sehemu za jengo huonekana na hali ya kulowana au ubichi.
Ambapo utaona:imelowa, ukijani ukijani,ukungu mweusi na hata chumvichumvi.

2.Aina za Dampness ni kuu tatu.
A.UNYEVU UNAOPANDA:huu ni unyevu wa maji unaopanda kutoka kwenye udongo kwenda kwenye jengo kupitia msingi wa jengo au slab ya sakafu.
-vitundu vidogo vidogo kwenye matofali ya kuchoma,block na zege huwezesha maji kupanda juu kutoka ardhini.
-Aina hii hutokea kwenye nyumba zilizo jengwa kwenye maeneo yenye Ardhi yenye kushikilia maji kwa mda mrefu. Mikocheni, Msasani(Bonde la mpunga)Mwanyamala,Mbezi Beach,
-maeneo ambayo ukichimba mita hata 2 unapata kisima cha maji.

3.Falling Dampness/Unyevu unaoanguka:Hii hutokana na kuchururizika kwa maji kutoka juu kutokana na ubovu wa mfumo wa paa,ambapo maji.
-Chanzo kikubwa ni Kuu kuvuja kwa bati,kuziba kwa gutter, ubovu wa mfumo wa gutter,angle ndogo ya kukimbilia maji ya mvua
-Hii hutokea sana kwenye majengo ya mtindo wa "Contemporary",mana mengi ya Majengo yana mfumo mbovu wa paa.
-Kwenye vibaraza vya Zege.
-Majengo yenye paa za zege.

4.PENETRATIVE DAMP/UNYEVU PENYEZI : Hii hutokea kwenye usawa wa ukuta.
-husababishwa na kuta kunyeshewa mvua na kuvuja kwa mabomba ya maji safi na maji taka
Ubovu wa uwekaji tiles vyooni au jikoni.
-miti kuwa karibu na nyumba
-ukuta wa fensi kuwa karibu na nyumba
-usanifu mbovu wa sehemu/Chumba cha jiko.
-Mafuriko

5.Athari za DAMP/UNYEVU
Amini au usiamini, chanzo kikubwa cha kuharibika kwa Majengo ni uwepo wa UNYEVU.
mojawapo ya athari zake ni.
-Kutu kwenye nondo.
-Kuharibika kwa zege
...unyevu ndani ya zege huipa nondo kutu na kusababisha nondo kuvimba na mwishowe nyufa.
-chumvi kwenye matofali na plasta .
-Kuharibika kwa finishings za kwenye sakafu
Mf.tiles ubanduka,

6.Athari nyingine
Kulegea na kubanduka kwa plasta
-Kuvimba kwa mbao
-kumeng'enyuka kwa mbao
-huleta mazalia ya mchwa,na mbu
-kubanduka kwa rangi

- Kupunguka kwa rangi, utaona madoa meupe meupe au michizi meupe katika rangi, hasa kwenye kuta zilizo pakwa rangi ya kijivu.
-hitilafu ya umeme kwenye jengo.
 
Asante.Nakumbuka nyumba nyingi za Mikocheni zinabanduka plasta na rangi na kuta zinakuwa za unyevunyevu muda wote. Ungekuwa umemalizia kwa kuandika solution ingependeza. Usitoe mafundisho ya vitisho kama hawa ''manabii. wa kileo wanavyotishia waumini juu ya majini na wanga, vibwengo na vinyamkera halafu wanaambia suluhisho waende kwenye makanisa yao wanayoyaongoza.
 
7.Udhibiti wa Dampness/Unyevu(Kabla ya Ujenzi)
A) Umbali kati ya jengo na fensi/uzi: weka umbali usiopungua mira 2,
B) Umbali kati ya jengo na miti: umbali usio pungua mita 6 kati ya jengo na miti mikubwa (majani mapana/Daikotiledoni)...
-Umbali usiopungua mita 3 kati ya jengo na miti ya monokotiledoni:miti huzuia mwanga wa jua,hivyo hufanya kuta kulowa mda wote
C) Design/Sanifu nzuri ya jiko
D) Weka Damp proof cousre kwenye msingi:huzuia maji kupanda.
E) Tumia matofali ya block ya mashine: yana mgandamizo mzuri
F) Kutojenga kwenye sehemu yenye kutuwamisha maji...
G)Utumizi wa vidhibiti maji/waterproofing kwenye paa za zege.
H) mfumo mzuri wa kukusanya maji ya mvua.

8.Udhibti wa Dampness katika jengo (jengo lililokamilika).
Kwanza ili uweze kudhibiti, ni lazima ujue chanzo ni kipi.
A) Kukata miti iliyopo karibia na jengo
B) Kutoweka AC(ile mashine yake inayowekwa nje kutoa maji) karibu na ukuta.
C) Marekebisho ya mfumo maji.
D)Marekebisho kwenye mzunguko wa hewa
E) Kuacha ubahiri
Tumia fundi bora/mtaalam na ununue matilio zenye ubora.

9.Vidhibiti maji vinavyoweza kutumika ni
A.matilio za asili ya metal mf.panel za kopa na lid
B.Matilio za asili ya Plastic
Mf.kapeti la Nailoni
C.matilio ngumu zenye matundu madogo sana
Mf.mawe
D.Matilio ya asili ya Lami:
Tar ,kapeti la DPM na EPDM.
E.Kemikali : Acrylic na nyinginezo huwekwa kwenye mchangyiko wa zege au Screed.

10.Kwneye utumizi wa vidhibiti maji ni muhimu kujua maji unaenda kudhibiti sehemu gani ya jengo na asili ya hiyo sehemu.

Nakaribisha maoni na maswali
Pendekezeni kipi cha kujadiliwa toleo lijalo..
NB :Ambatanisha picha ili iwe rahisi kujibu swali lako
 

Attachments

  • images-34.jpeg
    images-34.jpeg
    37.9 KB · Views: 14
Uharibifu wa ukuta kutokana na unyevu
 

Attachments

  • images-32.jpeg
    images-32.jpeg
    21 KB · Views: 14
  • images-33.jpeg
    images-33.jpeg
    12.3 KB · Views: 13
  • images-31.jpeg
    images-31.jpeg
    32.1 KB · Views: 14
  • images-30.jpeg
    images-30.jpeg
    22.6 KB · Views: 13
Karibu katika Makala yenye kuelimisha mambo muhimu kuhusiana na ujenzi wa Majengo.
Leo,tutaangazia juu ya DAMPNESS/Unyevu katika jengo.
Hili ni jambo linalokumba Majengo nchi nzima.

1.Dampness/ Unyevu jengoni: Hii ni hali ya ambayo sehemu za jengo huonekana na hali ya kulowana au ubichi.
Ambapo utaona:imelowa, ukijani ukijani,ukungu mweusi na hata chumvichumvi.

2.Aina za Dampness ni kuu tatu.
A.UNYEVU UNAOPANDA:huu ni unyevu wa maji unaopanda kutoka kwenye udongo kwenda kwenye jengo kupitia msingi wa jengo au slab ya sakafu.
-vitundu vidogo vidogo kwenye matofali ya kuchoma,block na zege huwezesha maji kupanda juu kutoka ardhini.
-unyevu huo na uwezo wa kupanda mpaka urefu wa mita 1.5 kutoka usawa wa ardhi.
-Aina hii hutokea kwenye nyumba zilizo jengwa kwenye maeneo yenye Ardhi yenye kushikilia maji kwa mda mrefu. Mikocheni, Msasani(Bonde la mpunga)Mwanyamala,Mbezi Beach,
-maeneo ambayo ukichimba mita hata 2 unapata kisima cha maji.

3.Dampness/Unyevu inayoanguka:Hii hutokana na kuchururizika kwa maji kutoka juu kutokana na ubovu wa mfumo wa paa,ambapo maji.
-Chanzo kikubwa ni Kuu kuvuja kwa bati,kuziba kwa gutter, ubovu wa mfumo wa gutter,angle ndogo ya kukimbilia maji ya mvua
-Hii hutokea sana kwenye majengo ya mtindo wa "Contemporary",mana mengi ya Majengo yana mfumo mbovu wa paa.
-Kwenye vibaraza vya Zege.
-Majengo yenye paa za zege.

4.DAMP/UNYEVU PENYEZI : Hii hutokea kwenye usawa wa ukuta.
-husababishwa na kuvuja kwa mabomba ya maji safi na maji taka
Ubovu wa uwekaji tiles vyooni au jikoni.
-miti kuwa karibu na nyumba
-ukuta wa fensi kuwa karibu na nyumba
-usanifu mbovu wa sehemu/Chumba cha jiko.
-Mafuriko

5.Athari za DAMP/UNYEVU
Amini au usiamini, chanzo kikubwa cha kuharibika kwa Majengo ni uwepo wa UNYEVU.
mojawapo ya athari zake ni.
-Kutu kwenye nondo.
-Kuharibika kwa zege...unyevu ndani ya zege huipa nondo kutu na kusababisha nondo kuvimba na mwishowe nyufa.
-chumvi kwenye matofali na plasta hapa nadhani mnajua kuwa chumvi huleta madhara kwa megua matofali kidogokidogo
-Kuharibika kwa finishings za kwenye sakafu
Mf.tiles ubanduka,

6.Athari nyingine
Kulegea na kubanduka kwa plasta
-Kuvimba kwa mbao
-kumeng'enyuka kwa mbao
-huleta mazalia ya mchwa,na mbu
-kubanduka kwa rangi
- Kupunguka kwa rangi, utaona madoa meupe meupe au michizi meupe katika rangi, hasa kwenye kuta zilizo pakwa rangi ya kijivu.
-hitilafu ya umeme kwenye jengo.
Well
 
Njia za udhibiti ni nyingi mkuu...
Itakuwa vyema ukatuma picha za sehemu ambapo imetokea ili nitoe ushauri.
images-31.jpeg

Screenshot_20240303_154923_Chrome.jpg

tatizo ni kama hili tu na picha zingine ulizoweka kwenye post. Plasta na rangi zinapukuchika tu. Nifanyaje hapo. Niweke tiles mpaka usawa dirisha?
 
View attachment 2923076
View attachment 2923083
tatizo ni kama hili tu na picha zingine ulizoweka kwenye post. Plasta na rangi zinapukuchika tu. Nifanyaje hapo. Niweke tiles mpaka usawa dirisha?
Fanya hivi nitumie hizo picha kwenye Private me
View attachment 2923076
View attachment 2923083
tatizo ni kama hili tu na picha zingine ulizoweka kwenye post. Plasta na rangi zinapukuchika tu. Nifanyaje hapo. Niweke tiles mpaka usawa dirisha?
Mfano; picha ya kwanza,hapo inaonekana ni ndani
1.Inaweza kuwa Risingi Damp:Maji yanatoka kwenye msingi kuja juu,kwa maana hata floor imelowa kwa mbali.
-Chanzo chaweza kuwa nyumba haina damp proof katika msingi.
Lakini kwa kiwango cha uharibifu inawezekana jengo lipo kwenye eneo la maji maji
2.Inawezekana ikawa Penetrative Damp:yani unyevu unaopenya Kwenye ukuta kwa maana Damp ipo zaidi ya 1.5 kutoka chini.
Labda upande wa pili kuna Tanki la kuhifadhia maji na hawajaa hilo eneo vizuri ili lisipitishe maji
Au limefunikwa na udongo kwa upande huo.



Picha ya Pili
Hiyo ni Rising damp
Tena hilo eneo lina chumvi chumvi
Sasa hapo picha haioneshi hadi chini...
 
View attachment 2923076
View attachment 2923083
tatizo ni kama hili tu na picha zingine ulizoweka kwenye post. Plasta na rangi zinapukuchika tu. Nifanyaje hapo. Niweke tiles mpaka usawa dirisha?
1. Piga takribani 4
2.Piga picha 2 kwa nje na 2 law ndani za kuonesha ukuta huohuo.
3.Picha ioneshe na mazingira karibia na ukuta yaani ardhi na paa
4.Tuma kwenye PM kwa privacy yako zaidi
 
Asante.Nakumbuka nyumba nyingi za Mikocheni zinabanduka plasta na rangi na kuta zinakuwa za unyevunyevu muda wote. Ungekuwa umemalizia kwa kuandika solution ingependeza. Usitoe mafundisho ya vitisho kama hawa ''manabii. wa kileo wanavyotishia waumini juu ya majini na wanga, vibwengo na vinyamkera halafu wanaambia suluhisho waende kwenye makanisa yao wanayoyaongoza.
Mbona nimeweka mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom