Planet Bongo na WCB

Planet Bongo na WCB

koncho77

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
7,790
Reaction score
10,413
Leo kipindi cha Planet Bongo huku Dj Summer na yale manjonjo yake balaa tupu kule Dula Planet mwenye Bongo yake mara paap nikasikia goma la Rayvanny na Zuchu Number One limechezwa hewani nimefurahi mnooo maana yake bifu limeisha kati ya EA RADIO na WCB
 
Sidhani Kama WCB siku hizi wana mabifu sana kama kipindi kile na naona mabifu yanaeleke mwisho
 
Sisi kama konde gengi tunasema bifu iendelee🐒🤣🐒
 
Pia watangazaji wengi tu wa wasafi plus Rayvanny walishaojiwa kwenye kile kipindi kinachorushwa na Salama Jabiri tena this year kwahiyo hakuna bifu Kati yao.
 
Sidhani Kama WCB siku hizi wana mabifu sana kama kipindi kile na naona mabifu yanaeleke mwisho
Wao wenyewe wameanza kugonga ngoma za Kondegang.

Nahisi mwakani mabeef yatakuwa yamepungua sana maana sasa hivi wajanja wengi.

Check Nandy kakusanya wasanii, kashawishi TCCL na Clouds na jafanya Nandy Festival kwa mafanikio.

Hata ukimbania wewe haisaidii, monopoly waliyo enjoy Clouds enzi za Ruge haipo tena.
 
Kiukweli tu, zile media houses kama EA Radio&Tv na Clouds, na hata huyu mfata mkumbo bw Millard Ayo wamesalimu amri kwasababu zifuatazo:

1. Ukuaji kimuziki ikiwemo kutoa hit songs kwa wasanii waliochini ya Label ya WCB, kumepelekea hizi media kupata pressure kwa wasikilizaji wao kwa nyakati tofauti kuomba baadhi ya ngoma za wasanii wa hii label kuchezwa ktk vipindi vyao

2. Uwepo wa Wasafi redio&Tv, ambao umechangia kupunguza uMungu watu kwenye hizi media IPP na Clouds, kwani hii media imepata mapokezi mazuri kwa halaiki ya watu hvyo kupelekea hata wasanii wa WCB kutotegemea tena media kama Clouds, EA Radio nk eti wapeleke nyimbo zao ndipo wasikike

3. Skendo karibu kubwa kubwa na zinazokiki zinahusu wasanii wa WCB, hvyo kuwafanya wasikilizaji wengi kuwa na shauku ya kutaka kusikia ishu zao ambapo fursa ya kusikia mambo yao utaipata kwenye Wasafi radio.
Na hii ilipelekea mpaka kipindi cha Shilawadu kupoteza watazamaji kwakuwa waliacha kuripoti mambo ya akina Diamond na wenzake ilhali hawa ndio gumzo la nchi kwa sasa.

Hizi ni baadhi tu ya sababu zilizopelekea hawa jamaa kusalimu baada ya kuwabania kwa kipindi kirefu wasanii hawa wakijua hawatotoboa, lakini mapinduzi waliyoyafanya hasa Diamond na uongozi wake kina Sallam Sk na Tale umewapa milleage kubwa sana kimuziki África na dunia
 
Back
Top Bottom