Chizi Fureshi
JF-Expert Member
- Oct 26, 2010
- 1,718
- 457
Acha kuropoka wewe. Nenda pale magomeni ukaimbe taarabu.
Naona Wanabodi wengi wanamponda mtoa hoja kwamba hoja yake haina mantiki kwa vile haina ushahidi. Anyway Mimi binafsi hili swala si mara ya kwanza kuliskia. Siku moja nilikuwa natoka Mbeya nilipanda Sumry na bahati nzuri nilikaa seat ya mbele nyumba ya dereva upande wa kordo. Tulikuwa tunapiga sana story na Dereva, Kondakta na Utingo. Na abiria wengi walidhani labda nami nilikuwa Staff. Tulipofika hotel ya AL-Jazera kwa ajili ya kula tulishuka nikaenda kula nao kule wanakokula madereva na makondakta.
Frankly speeking baada ya maongezi ya muda mrefu yule dereva (Sitamtaja jina kwa usalama wake) aliniambia kwamba Mh Pinda nae ameweka share zake kwenye kampuni ya Sumry. Sikuamini lakini nilichukua tu hiyo habari na kukaa nayo kichwani.
Baadae kama mwezi mmoja ukapita, Gazeti la MwanaHalisi nalo likaripoti kwamba Pinda amewekeza katika kampuni ya Sumry kupitia Kampuni yake inayoitwa 'MOVERS TRANSPORT (Kama sijakosea)'. Sasa kama tumeweza kuamini kwamba Bibi Kiroboto anashare kwenye SUPER FEO na William Lukuvi nae anashare kwenye UPENDO Trevallers Coach kwa nini tusimwamimi franktemu123 wakati wadau walioleta habari za SUPER FEO na UPENDO hawakuwa na ushahidi?
TUMBIRI (PhD, Hull University - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
Wewe kweli tumbiri kweli kweli. Hio elimu yako kubwa ulioyo nayo haikusaidii kabisa. Huo ndio ushahidi uliotumwa uulete hapa na aliekutuma? Mwambie kuwa mipango yake imesha shindwa akakae tuu kwao hana lake hawezi kutudanganya kirahisi hivyo. Huu uzushi umeshindika mkuu njoo tuu na mada nyingine.
lete ushahidi wa madai yako...
Alfred Ngowi,
Nimeamini kweli ni vigumu binadamu kukata mkono unaomlisha!
TUMBIRI (PhD, Hull University - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
Wanajmvi huyu jamaa kwa nje anaonekana msafi kiundani ni mchafu kupitiliza toka aukwae u-PM amekomaa kuchota pesa zetu na kuzipeleka kwenye SUMRY EXPRESS na sasa wameona kama wanashtukiwa wamenunua kampuni ya MBEYA EXPRESS kupotezea. Hebu cheki ule Uwanja wa ndege MPANDA ulivyotengenezwa fasta. Pia, alitaka Yambesi awe Katibu mkuu kiongozi kwa sababu wanatoka wote RUKWA mzee Luhanjo akamzidi kete kwa kumpendekeza best yake mzee OMBENI. Kuweni makini na huyu mtu nje anajifanya anamwaga chozi kumbe fisadi kiaina. Zaidi anajidai anapigia debe kilimo kwanza kumbe ndo anapofisadi kuanzia Matreka,Mbolea etc.......MKUU TUMEKUSHTUKIA
Wadau mnataka evidence ya Risiti/Mkataba ulioandikwa jina/saini yake au? yaani unafikiri yeye ni mjinga kiasi hicho? lengo la kuandika hapa ni watu wajue na wenye uwezo wa kuchimba zaidi afanye hivyo usitegemee mtu mmoja awe na habari complete. uliona wapi hiyo. Sijatumwa na mtu mimi ni mwananchi mwenye uchungu na nchi yangu na jinsi pesa/rasilimali zinavyoliwa na wajanja wachache
Atakula nini akitoka madarakani? mwache ale akishiba ataacha!
Sasa wewe Tumbiri aka DR MAJUNGU uache uzushi na ushambenga na misemo yako ya taarabu. Hapa sio mahali pa mipasho ya upashkuna, ni mahali pa Great Thinkers ndugu. Tafuta mada nyingine nasio hio ya uzushi na upashkuna DR MAJUNGU wewe..
Alfred Ngowi,
Hapa ni JamiiForums Jukwaa la siasa siyo mahala pa uzushi, majungu wala ushambenga. Hii thread imefika hadi page ya 3 mods wameridhika na content zake hatimae wameamua kuiacha. Kama unaona post haina mantiki kwa nini usibonyeze Report Abuse utoe hoja zako kwa Mods waiondoe thread badala yake wewe na wenzako mmebaki tu kupayuka majungu, majungu, majungu, majungu bila kupeleka hoja kwa Mods. Ushahidi wa Gazeti la MwanaHalisi pamoja na Oral evidence kutoka kwa watu wa karibu na kampuni husika tumewaletea bado mnaendelea kubisha, mnataka tuwabebe kuwabembeleza hadi mkubali?
Kwanza nyie mnaodai kwamba thread ni ya majungu mnawakosea heshma mods wote wa jukwaa hili mnatuaminisha kuwa hata wao wanashangilia haya Majungu? Ifikie hatua tukubali taarifa nzuri na mbaya za wapendwa wetu maana na wao siyo malaika.
TUMBIRI (PhD, Hull University - UK),
tumbiri@jamiiforums.com
Hao watu wakaribu na hizo media unazijua wewe. ingekua vyema na habari za ukweli kama unge wataja majina hao watu unaosema wakaribu. ndio maana nasema huu ni uzushi tuu "DR" Huwezi kuacha kutoa majina na habari iliyo kamili na kusema eti kwasababu za usalama. iliniamini wataje majina. kwasababu mimi mwenyewe nawafaham baadhi ya wafanyakazi wa SUMRY. Wataje majina hao kama ni kweli.
Alfred Ngowi,
Nina wajua kwa majina na Kondakta niliongea nae kwenye simu nadhani last month aliniambia ameahamia SAI BABA EXPRESS. Sasa unataka nikutajie majina yao ili washughulikiwe kwa kutoa siri za kampuni au? Sitakuwa nimewatendea haki kuwataja mahala hapa. Sipo tayari kuwataja Kaka maana najua watafukuzwa kazi but taarifa yangu ni ya uhakika. Na hata huyu Kondakta aliyehamia SAI BABA simtaji maana atakuwa chanzo cha kumjua huyo dereva.
Haya wewe unakataa habari ya MwanaHalisi mbona Pinda mwenyewe hakukana ile habari hadi leo na mbona hakwenda mahakamani au MCT kudai kudhalilishwa na gazeti husika?
TUMBIRI (PhD, Hull Univeristy - UK),
tumbiri@jamiiforums.com