Pinda na umiliki wa Sumry Express

Pinda na umiliki wa Sumry Express

Status
Not open for further replies.
yale mabasi yenye picha y penguine yanaitwaje? huwa yanapiga ruti za dar-mbeya na dar-tunduma.

yale ni tajiri mmoja anaitwa supar feo wa songea japo inasemekana na mama Makinda ana mkono wake.!
 
yale ni tajiri mmoja anaitwa supar feo wa songea japo inasemekana na mama Makinda ana mkono wake.!

hilo jina(super feo) lilinitoka....sio kwamba inasemekana...ni kweli mama ni mmoja wa wamiliki....
 
Hv mtu mzima na akili zako utawzaje kuandika ushuzi kama huu
 
Sikusema SUMRY EXP imeanza baada Handsome Pinda kupewa u-PM, wala sikusema amejenga Uwanja wa Ndege Mpanda kwa pesa yake lakini swala linakuja hivi vyote vimekuja fasta mara baada ya yeye kuingia kuwa PM, hapo sijazungumzia kuhusu kuanzisha mkoa wa KATAVI maana hata bibi kiroboto alipewa wake wa NJOMBE so ni suala la kupeana hata Sumaye alijimegea MANYARA huenda NDESAMBURO akiwa PM nae akajipatia mkoa mpya wa KIBOROLONI. Mimi binafsi naamini kwenye usawa maana kwa nini iwe RUKWA?MPANDA tena baada ya yeye kuwa PM? na sio mikoa mingine? kwenye hayo mabasi ya SUMRY nakubaliana na nyie ushahidi nitatoa kesho saa 5 asubuhi pale Maelezo Dar es Salaam, samora Avenue. nimeshafanya Booking ya kupata nafasi muda huo. karibuni nyote. Watanzania tuzinduke tusianze kumlaumu mtoa mada kesho nikitoa ushahidi ninyi makada sijui mtaficha siri hiyo wapi. KWA STYLE HII YA MAJADILIANO HUMU NIMEGUNDUA ni kazi rahisi sana kuwaibia watanzania na wasishtuke.
 
i mean baada ya u-PM akaweka pesa za mule SUMRY na kutumia mamlaka yake SUMRY inakwepa kodi TRA
 
We need evidence... Otherwise this wastage of time!!
 
Wanajmvi huyu jamaa kwa nje anaonekana msafi kiundani ni mchafu kupitiliza toka aukwae u-PM amekomaa kuchota pesa zetu na kuzipeleka kwenye SUMRY EXPRESS na sasa wameona kama wanashtukiwa wamenunua kampuni ya MBEYA EXPRESS kupotezea. Hebu cheki ule Uwanja wa ndege MPANDA ulivyotengenezwa fasta. Pia, alitaka Yambesi awe Katibu mkuu kiongozi kwa sababu wanatoka wote RUKWA mzee Luhanjo akamzidi kete kwa kumpendekeza best yake mzee OMBENI. Kuweni makini na huyu mtu nje anajifanya anamwaga chozi kumbe fisadi kiaina. Zaidi anajidai anapigia debe kilimo kwanza kumbe ndo anapofisadi kuanzia Matreka,Mbolea etc.......MKUU TUMEKUSHTUKIA
Toa uthibitisho sio kupayuka payuka tu.
 
inawezekana vipi bila ushahidi kaka, mbona mpika majungu ivo wewe??? administrator unaachaje wapika majungu kutawala JF badala ya great thinkers??? Fanyia kazi hii.

Na wewe si ulete ushahidi kuwa siyo kweli? Wasaidie mods kwa kuwapa ushahidi kuwa haya ni majungu tu na bila shaka watachukua hatua stahili.
Mh! Mungu anisamehe lakini PINDA ni msafi jamani kwanini mnapenda kuzulia watu mambo? simjui hanijui lakini huyu baba MNAMUONEA !
Pinda ni msafi? Sasa anafanya nini kambini kwa wezi? Kikwete anazuliwa, Pinda anazuliwa, Lowassa anazuliwa, Nape anazuliwa, Chenge anazuliwa...! Sasa kama viongozi wa serikali, viongozi wa CCM pamoja na wabunge wote wa CCM wanazuliwa, hao "oil chafu" ndani ya CCM na serikalini, huo uzito wa kutokuelea wanaupata wapi?
 
Huyu ni mchokoza mada, kama una input unaweka huna unakaa kimya. Theme ya uzi huu ni Pinda katika darubini, sisi anaotuongoza tunahaki ya kuhoji credibility yake, mi nashangaa kama kweli hata leo nikawa waziri halafu nikashindwa kumiliki chini ya mil 100 tena za halali kabisa. Nikishindwa mi maanake sifai hata huo uongozi, kwani ni dhambi? siasa nyingine ni upuuzi
 
Ni kweli tunahitaji PM masikini? Kuna kosa gani akimiliki Sumry? Udaku mie huwa siupendi!
 
Inawezana ikwa kweli
ndani ya ccm
hamna msafi!
Ni bora nimwamini Luhanjo kuliko huyu jamaa yenu. Na huo mkoa wake aliouanzisha sijui but kwa mawazo yangu ufisadi siyo HEPA tu maamzi mabaya nayo ni ufisadi hatarishi zaid
 
Khaaa, sasa asifanye biashara? Au ndo siasa na biashara hazitakiwi?
 
Wanajmvi huyu jamaa kwa nje anaonekana msafi kiundani ni mchafu kupitiliza toka aukwae u-PM amekomaa kuchota pesa zetu na kuzipeleka kwenye SUMRY EXPRESS na sasa wameona kama wanashtukiwa wamenunua kampuni ya MBEYA EXPRESS kupotezea. Hebu cheki ule Uwanja wa ndege MPANDA ulivyotengenezwa fasta. Pia, alitaka Yambesi awe Katibu mkuu kiongozi kwa sababu wanatoka wote RUKWA mzee Luhanjo akamzidi kete kwa kumpendekeza best yake mzee OMBENI. Kuweni makini na huyu mtu nje anajifanya anamwaga chozi kumbe fisadi kiaina. Zaidi anajidai anapigia debe kilimo kwanza kumbe ndo anapofisadi kuanzia Matreka,Mbolea etc.......MKUU TUMEKUSHTUKIA

Jamani jitahidini kuwa na kumbukumbu! Habari hii iliwahi kuandikwa na Kubenea kwenye moja ya matoleo ya Mwanahalisi na Pinda mwenyewe wala hakujitokeza kukanusha, kwahiyo nadhani kuna ukweli wa kiwango fulani. Mimi simtetei hata kidogo maana waliojifanya wasafi ndio hao hao tunapata habari zao tunaishiwa kupigwa na butwaa.
 
Kwa wanaotaka evidence na kujifanya ni marealistics watupe evidence vile vile za EL na richmond sio kuwa mwanadamu anaetawaliwa na emotions and not helenic ability.
 
Inawezana ikwa kweli
ndani ya ccm
hamna msafi!
Labda kwa ule msemo usemao "samaki akioza mmoja basi wameoza wote" Watawala wetu walio madarakani wengi wao ni mafisadi na wenye kujineemesha wao wenyewe, lakini mimi binafsi naamini wapo wachache ambao ni waadilifu. Nisingependa kuwataja lakini ni muhimu tukubali hilo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom