Pinda na Makinda wampa changamoto Kikwete. Je watajiwajibisha au kuwajibishwa?

Ukweli ni kwamba Jk keshabariki posho za masaburi.Ila kwa vile unamjua raisi wako asivyo na msimamo anapima nguvu ya upepo na nadhani hakuna kiongozi kigeugeu kama yeye duniani.Je umeshau aliposema hawajui Dowans, na aliposema hakuna mwanafunzi wa chuo kikuu atafukuzwa kwa kukosa ada? Umesahau alivyomtuma Vuvuzela nape awatukane wakuvuliwa magamba kisha kamgeuka.Na ilani ya CCM na OIC je? si aliwageuka waisilamu wenzake.

Btw, wote hao yaani Jinga Kubwa, Bi kiroboto na huyo mtoto wa tajiri ambaye hajitambui wala hatambui madaraka yake ni yapi [mzee wa kumwaga chozi]; ni vipofu wanao-ongozana na mwisho wa siku wote watatumbukia katika shimo.

Kama kweli wewe naye unajiita great thinker, basi humu JF tumeishiwa. Kama baba yako aliyekuzaa akikutukana huwezi kujisikia vizuri ukimtukana wewe yeye atajisikiaje. Kama Initials za majina ya watu zingekuwa zinamaanisha Matusi sijui ingekuaje, hebu tupe initials za jina lako na wewe tukutafutie tusi lako. Kiongozi yeyote ambaye ni RIGID ndugu yangu siyo kiongozi huyo. Kiongozi anayejali Demokrasia na utawala bora lazima awe Flexible, ndiyo maana Viongozi wa CDM (SLAA na MBOWE ) wanapeleka chama wanavyojua simply because they are Rigid. Hakuna anayethubutu kuwakosoa na kuwashauri. Angalia mahusiano ya ZITTO na viongozi wakuu wa CDM na mahusiano na watu kama LEMA na SUGU na viongozi hao ni tofauti kabisa kwa sababu ZITTO hawanyeyekei na pale wanapokwenda kinume anatofautiana nao( mfano ni walipotoka nje ya ukumbi wa bunge wakati President anahutubia, ZITTO alibaki). Lema na Sugu wanakubalika kwa viongozi hao kwa sababu wanafuata nyao zao kama vile kuanzisha vurugu na n.k
kwa mtazamo wangu JK siyo kigeugeu bali ni Kiongozi anayekubali ushauri, madilko na hali halisi kulinagana na mazingira ya wakati huo.
 
Acha matusi mkuu. Kwa kauli zilizokwisha tolewa na viongozi hao, hakuna udangayifu wowote, bali wamekuwa wakitolea ufafanuzi upotoshwaji juu ya suala zima za posho za Wabunge. Hata kama wangekuwa wamepitisha nani mwenye kosa hapo wabunge waliopendekeza posho hizo au Rais, Waziri Mkuu au Spika. Tujaribu kutafakari sana kabla ya kulaumu. Nakumbuka wabunge wengi tu walikubaliana kupandishiwa posho wakiwemo wa upinzani. HAPA NANI ANAWADANGANYA WATANZANIA? Rais, Waziri Mkuu na Spika au WAbunge. Mimi naona ni Wabunge. Tujaribuni kwenda na facts badala ya hisia binafsi.

Kwa upande wangu wote wanawadanganya wananchi. 1. Kama wabunge wamependekeza kwani rais hana uwezo wakuangalia hali halisi ya serikali na kupanga kiasi kingine ambacho hakitamuumiza mlipa kodi? 2. Bi kiroboto jana anatuambia hayo malipo si ya mwaka mzima bali niwakati wa vikao tu kwani ikiwa ni wakati wa vikao tu ndo walijipandishie kiasi kikubwa hivyo? Awali ilivyopandishwa alidai ni ugumu wa maisha je huo ugumu wa maisha nikwa wabunge pekee? Walimu na madaktari wapo nje ya Tz? 3. PM yeye inaonyesha anapelekwapelekwa tu pasipokuwa na msimamo wake mfano anavyojifanya ni mtoto wa mkulima huku akiendelea kuwakandamiza hao hao tumwelewe je? Mtazamo wangu mafisadi ndo waliomweka kuwatimizia amalengo yao
 
Jk ukimwambia kwanini usikatae kusign atakuambia wenzangu hawatanielewa inamaana yupo hapo ikulu kuwatumikia wenzake na siyo wananchi na wapo kwakulindana
 
Thata sijui tata una utata. Naona kama hujui usemacho. Unaposema tatizo ni mfumo bila kufafanua una maanisha nini? Hivi Kikwete kusema nimeidhinisha au la ni suala la mfumo au common sense. Nadhani sihitaji kurejea vitabu vyangu vya ontology wala cosmology kujua kuwa unaongelea usichojua. Hebu fafanua zaidi maana ya ubovu wa mfumo kuhusiana na uongo wa hawa watatu tajwa. Tunajua mfumo wetu ni mbovu lakini katika hili tatizo si mfumo bali uadilifu binafsi wa wahusika.
 
Ukweli ni kwamba Jk keshabariki posho za masaburi.Ila kwa vile unamjua raisi wako asivyo na msimamo anapima nguvu ya upepo na nadhani hakuna kiongozi kigeugeu kama yeye duniani.Je umeshau aliposema hawajui Dowans, na aliposema hakuna mwanafunzi wa chuo kikuu atafukuzwa kwa kukosa ada? Umesahau alivyomtuma Vuvuzela nape awatukane wakuvuliwa magamba kisha kamgeuka.Na ilani ya CCM na OIC je? si aliwageuka waisilamu wenzake. Btw, wote hao yaani Jinga Kubwa, Bi kiroboto na huyo mtoto wa tajiri ambaye hajitambui wala hatambui madaraka yake ni yapi [mzee wa kumwaga chozi]; ni vipofu wanao-ongozana na mwisho wa siku wote watatumbukia katika shimo.
Jinga Kubwa=J.K
 
it's something which is irelevant kabisa hata ukiangalia kwa wabunge ambao wengine elimu zao ni ndogo na kazi yao nikupayuka majukwaani na kupitisha bajiti za kupewa hongo na kulala bungeni tu bado wanalipwa zaidi ya madaktari na walimu ambao wanafanyia kazi ktk mazingira magumu

Kiwango cha kufikiri kiwapo katika uzani wa kukubali meli iendelee kuzama badala ya kufanya jitihada za kuiokoa ndio zengwe la mabaharia waliokwisha kata tamaa na kubaki kula kwa fujo vilivyomo ndani ya meli kwa vile hawana hakika na mwendelezo wa maisha yao kutokana na meli kuzama wakati wo wote.
 
Thata sijui tata una utata. Naona kama hujui usemacho. Unaposema tatizo ni mfumo bila kufafanua una maanisha nini? Hivi Kikwete kusema nimeidhinisha au la ni suala la mfumo au common sense. Nadhani sihitaji kurejea vitabu vyangu vya ontology wala cosmology kujua kuwa unaongelea usichojua. Hebu fafanua zaidi maana ya ubovu wa mfumo kuhusiana na uongo wa hawa watatu tajwa. Tunajua mfumo wetu ni mbovu lakini katika hili tatizo si mfumo bali uadilifu binafsi wa wahusika.


Kikwete hajiamini katika nafasi yake pale Magogoni. Haiwezekani mswada uliopitishwa bungeni na kuwekewa mezani kwake akubali kusaini au aukatae aje aanze kuzunguka mbuyu kwa kumrudishia fail Waziri mkuu kwamba nendeni mkapime wenyewe kwa busara. Tunaye Rais asiyejiamini hii ndiyo hali halisi. Na kwa hali ilivyo ambayo Rais wetu anaonyesha ndio kiini cha mambo mengi kuyumba na hakuna atakayeona anakosea kwa vile hata ufanye nini hakuna kuwajibishwa kwa vile Rais mwenyewe hajui baadhi ya mambo anayowajibika.
 
Kama kweli wewe naye unajiita great thinker, basi humu JF tumeishiwa. Kama baba yako aliyekuzaa akikutukana huwezi kujisikia vizuri ukimtukana wewe yeye atajisikiaje. Kama Initials za majina ya watu zingekuwa zinamaanisha Matusi sijui ingekuaje, hebu tupe initials za jina lako na wewe tukutafutie tusi lako. Kiongozi yeyote ambaye ni RIGID ndugu yangu siyo kiongozi huyo. Kiongozi anayejali Demokrasia na utawala bora lazima awe Flexible, ndiyo maana Viongozi wa CDM (SLAA na MBOWE ) wanapeleka chama wanavyojua simply because they are Rigid. Hakuna anayethubutu kuwakosoa na kuwashauri. Angalia mahusiano ya ZITTO na viongozi wakuu wa CDM na mahusiano na watu kama LEMA na SUGU na viongozi hao ni tofauti kabisa kwa sababu ZITTO hawanyeyekei na pale wanapokwenda kinume anatofautiana nao( mfano ni walipotoka nje ya ukumbi wa bunge wakati President anahutubia, ZITTO alibaki). Lema na Sugu wanakubalika kwa viongozi hao kwa sababu wanafuata nyao zao kama vile kuanzisha vurugu na n.k
kwa mtazamo wangu JK siyo kigeugeu bali ni Kiongozi anayekubali ushauri, madilko na hali halisi kulinagana na mazingira ya wakati huo.


Nakubaliana na wewe. JK anafata ushauri wa wale waliomuweka madarakani na ambao unawajua. Pamoja na hayo, ukiwa kiongozi lazima uwe na falsafa ambazo unazisimamia na kuzitekeleza, siyo kufanya maamuzi kwa kuangalia hali ya hewa.
 
Kweli ni Bora kuogopa jeshi la kondoo linaloongozwa na SIMBA,kuliko jeshi la simba linaloongozwa na KONDOO.
 
Acha matusi mkuu. Kwa kauli zilizokwisha tolewa na viongozi hao, hakuna udangayifu wowote, bali wamekuwa wakitolea ufafanuzi upotoshwaji juu ya suala zima za posho za Wabunge. Hata kama wangekuwa wamepitisha nani mwenye kosa hapo wabunge waliopendekeza posho hizo au Rais, Waziri Mkuu au Spika. Tujaribu kutafakari sana kabla ya kulaumu. Nakumbuka wabunge wengi tu walikubaliana kupandishiwa posho wakiwemo wa upinzani. HAPA NANI ANAWADANGANYA WATANZANIA? Rais, Waziri Mkuu na Spika au WAbunge. Mimi naona ni Wabunge. Tujaribuni kwenda na facts badala ya hisia binafsi.

Ki utaratibu hizo posho haziwezi kulipwa mpaka rais azisaini. Wabunge wamependekeza kutokana na hali halisi ya maisha ilivyo kwa TUCTA na MAT walivyopendekeza. Rais na wataalamu wake walitakiwa kuangalia uwezo wa serikali na implication yake kwa wafanyakazi wengine kama walioangalia kwa madaktari. Huenda JK alisaini bila hata ya kusoma kilichomo kama kawaida yake. Na kama kawa siri ikavuja kwa wabunge kuwa JK kasaini. Unafikiri Spika ataacha kulipa wakati rais kaidhinisha hata kama aliidhinisha bila kujua kaidhinisha nini!!!!!!?????? Rais ndo anawadanganya wananchi.
 
Acha matusi mkuu. Kwa kauli zilizokwisha tolewa na viongozi hao, hakuna udangayifu wowote, bali wamekuwa wakitolea ufafanuzi upotoshwaji juu ya suala zima za posho za Wabunge. Hata kama wangekuwa wamepitisha nani mwenye kosa hapo wabunge waliopendekeza posho hizo au Rais, Waziri Mkuu au Spika. Tujaribu kutafakari sana kabla ya kulaumu. Nakumbuka wabunge wengi tu walikubaliana kupandishiwa posho wakiwemo wa upinzani. HAPA NANI ANAWADANGANYA WATANZANIA? Rais, Waziri Mkuu na Spika au WAbunge. Mimi naona ni Wabunge. Tujaribuni kwenda na facts badala ya hisia binafsi.

Pole kwa kazi. Sijui niseme umedANdia auumerukia na kuandika bila kutafakari. Unakumbuka Spika alisema posho ya330,000/- imeanza kulipwa kwa MPs kuanzia kikao kilichopita, Katibu wake akasemabado hazijaanza kulipwa.MAMA Makinda akapigia mstari kuwa she is right \mpswamelipwa. Katibu wake kakaa kimya. Ikulu ikasema JK hajabariki.
Leo PM anasema MKUU WA NCHI kaidhinisha naSPIKA na vivyo hivyo, leo wewe unasema sio kweli, la!!!!!!!! Sikuelewi unamaanishanini unaposema eti wabunge ndio wapotoshaji.
Ukweli ni kuwa wameamua kutufool WATZ, cozthey are sure we can do nothing to them. HIVI WEWE INAKUINGIA AKILINI KUWA PMPINDA ALISEMA asichokijua, kisha SPIKA MAKINDA naye anasema asichojua. No jamanikama ni hivyo basi serikali hii imesambaratika kama mihimili inakinzana kiasihicho.
THATHA ufahamu tu ndugu yangu kuwa TZ,wanasiasa ndiyo wanaothaminiwa sana hapa BONGO, wataalam hatawakilalamika snkama MADR, WALIMU NA WENGINE WENGI, KUMBUKA HAWA HAWA WALISEMA HAWANA 300,000/-KULIPA MSHAHARA ILA WANA 330,000/-KULIPA POSHO WABUNGE, hongera kama nawe nimmoja wao
POSHO ZIMEIDHINISHWA NA RAIS vinginevyowasingelipwa
 
Kama kweli wewe naye unajiita great thinker, basi humu JF tumeishiwa. Kama baba yako aliyekuzaa akikutukana huwezi kujisikia vizuri ukimtukana wewe yeye atajisikiaje. Kama Initials za majina ya watu zingekuwa zinamaanisha Matusi sijui ingekuaje, hebu tupe initials za jina lako na wewe tukutafutie tusi lako. Kiongozi yeyote ambaye ni RIGID ndugu yangu siyo kiongozi huyo. Kiongozi anayejali Demokrasia na utawala bora lazima awe Flexible, ndiyo maana Viongozi wa CDM (SLAA na MBOWE ) wanapeleka chama wanavyojua simply because they are Rigid. Hakuna anayethubutu kuwakosoa na kuwashauri. Angalia mahusiano ya ZITTO na viongozi wakuu wa CDM na mahusiano na watu kama LEMA na SUGU na viongozi hao ni tofauti kabisa kwa sababu ZITTO hawanyeyekei na pale wanapokwenda kinume anatofautiana nao( mfano ni walipotoka nje ya ukumbi wa bunge wakati President anahutubia, ZITTO alibaki). Lema na Sugu wanakubalika kwa viongozi hao kwa sababu wanafuata nyao zao kama vile kuanzisha vurugu na n.k
kwa mtazamo wangu JK siyo kigeugeu bali ni Kiongozi anayekubali ushauri, madilko na hali halisi kulinagana na mazingira ya wakati huo.

Wewe lazima utakuwa umeandika haya baada tu ya kuzinduka ICU.
 
Kama kweli wewe naye unajiita great thinker, basi humu JF tumeishiwa. Kama baba yako aliyekuzaa akikutukana huwezi kujisikia vizuri ukimtukana wewe yeye atajisikiaje. Kama Initials za majina ya watu zingekuwa zinamaanisha Matusi sijui ingekuaje, hebu tupe initials za jina lako na wewe tukutafutie tusi lako. Kiongozi yeyote ambaye ni RIGID ndugu yangu siyo kiongozi huyo. Kiongozi anayejali Demokrasia na utawala bora lazima awe Flexible, ndiyo maana Viongozi wa CDM (SLAA na MBOWE ) wanapeleka chama wanavyojua simply because they are Rigid. Hakuna anayethubutu kuwakosoa na kuwashauri. Angalia mahusiano ya ZITTO na viongozi wakuu wa CDM na mahusiano na watu kama LEMA na SUGU na viongozi hao ni tofauti kabisa kwa sababu ZITTO hawanyeyekei na pale wanapokwenda kinume anatofautiana nao( mfano ni walipotoka nje ya ukumbi wa bunge wakati President anahutubia, ZITTO alibaki). Lema na Sugu wanakubalika kwa viongozi hao kwa sababu wanafuata nyao zao kama vile kuanzisha vurugu na n.k
kwa mtazamo wangu JK siyo kigeugeu bali ni Kiongozi anayekubali ushauri, madilko na hali halisi kulinagana na mazingira ya wakati huo.

Mbona unakuwa na jazba kiasi hiki mkuu, hapa unatakiwa kujibu hoja tu, acha mambo zako za "adabrakadabra"

Hebu soma alichoandika huyu mkulu hapa chini ili uone mantiki ya hii hoja.

Kikwete hajiamini katika nafasi yake pale Magogoni. Haiwezekani mswada uliopitishwa bungeni na kuwekewa mezani kwake akubali kusaini au aukatae aje aanze kuzunguka mbuyu kwa kumrudishia fail Waziri mkuu kwamba nendeni mkapime wenyewe kwa busara. Tunaye Rais asiyejiamini hii ndiyo hali halisi. Na kwa hali ilivyo ambayo Rais wetu anaonyesha ndio kiini cha mambo mengi kuyumba na hakuna atakayeona anakosea kwa vile hata ufanye nini hakuna kuwajibishwa kwa vile Rais mwenyewe hajui baadhi ya mambo anayowajibika.
 
Kama kweli rais hajaidhinisha malipo ya marupurupu ya wabunge na posho za makalio, hawa akina Pinda na Makinda walipata wapi hayo waliyosema? Je hapa nani anawadanganya watanzania?

pengine labuda tuseme THE CITIZEN wamedanganya na MTN ambaye ndiye aliyenukuu gazeti la CITIZEN
 
Huu unawezekana ukawa ni muendelezo wa minyukano ndani ya CCM. Yaani wakati posho ya vikao inalalamikiwa kutoka kila quarter; Wananchi, wanaharakati, wapinzani, wahisani: ni jambo la ajabu kabisa kuwa wabunge tena wa CCM waje na hoja ya kuongeza posho hiyo hiyo tena kwa asilimia nyingi kiasi hicho halafu anapelekewa ili aidhinishe, halafu watu wanaanza kutamba wazi wazi kuwa ameshaidhinisha wakati hawajapata signed copy!!

Hapa kuna walakini na inaonekana kuna watu wanafanya kazi ambazo hawajui matokeo yake nini!! Suala hili linamuanika wazi kabisa rais na naona ameshtuka. Ila wasaidizi wake inaonekana hawaoni TEGO hilo!
 
Tunajadili hii mada kama vile hizi posho hazijalipwa, kiukweli hizi posho zilianza kulipwa tangu bunge lililopita. Cha maana tuangalie nani aliruhusu huo ulipaji kama rais alikuwa hajasaini? Mkaguzi mkuu wa serikali, takukuru na vyombo vya kinidhamu vinatakiwa vitupe taarifa ya huu mkanganyo. Ni wakati sasa na bunge liundiwe tume itakayoshughukia huu upimbavu na ikiwezekana hiyo ripoti isomwe kwa mbwembwe kama ambavyo ripoti nyingine zimesomwa. Na napendekeza mwenyekiti wa hiyo kamati awe Zitto au Januari.

Na sie watanzania ni wakati muafaka wa kuuliza huu uzembe umefanyikaje na ifike wakati tudai wazembe wawajibishwe.
 
Nashukuru Thatha kwa mchango wako na ukosoaji wako juu ya kumwita JK=Jinga Kubwa;nashukuru kwa kunikumbusha kuwa matusi si mazuri.Lakini nasikitika kwamba sina jina lolote zuri la kumuita huyo mtu zaidi ya hilo maana matendo yake yanasadifu jina lake.Mtu anayeona wezi wanaiba nyumbani kwake yeye anachekelea, watu wake wanakufa yeye anachekelea, yaani kila uchafu unaotendeka anauangalia tu.Ni sawa na mbwa asiye na meno hawezi kung'ata.Kama ni baba wa hivyo ni heri kuwa yatima na kupambana kivyangu maana huyo anauza hata urithi na mali za familia ambazo naye karithishwa wala hajazifatufa yeye.
 
Afadhali umeliona hilo kwa sababu wengi tunakimbilia kuwalaumu viongozi wetu wakati kumbe tatizo linaeleweka. Tatizo ni mfumo na mfumo haujawekwa na JK, MAKINDA au PINDA. Mfumo upo kisheria na ndicho tunachotakiwa kuongelea na hasa katika kipindi hiki cha mchakato wa kupata katiba mpya. Kafurila alikuwa sawa na ndiyo sababu kama mbunge makini hawezi kukimbilia kulaumu viongozi huku akijua tatizo ni mfumo. Kusema Rais, Waziri Mkuu au Spika anawadanganya wananchi ni kuonesha jinsi gani una upeo mdogo wa kuchambua mambo.

Wewe ndiyo j.in.g.a kabisa huo mfumo unaongelea umeshushwa kutoka mbinginu na shetani?!
Huyo mfumo mbovu wa posho na mishahara umewekwe na SERIKALI YA CCM deliberately.
Wenzao wa CDM waliwaeleza mavuvuzela wa CCM wa scrap POSHO za makalio (read sitting allowance).
Magamba kwa wingi wa ujinga wao wakapinga. It is no coincidence hiyo posho inayolalamikiwa ndiyo
imeongezwa kwa 200%

Wewe ndiye mwenye upeo mdogo usiyeweza to put 2 and 2 together to get 4!
 
Poleni wadanganyika!
Kupitishwa kwa muswada wa katiba kuna imply nini kwenye suala zima la posho kupelekwa kimzobemzobe namna hii? Kama tungekuwa na viongozi waadilifu, kungekuwa na baadhi ambao wangeshajiuzulu bila shinikizo. Aidha Pinda, Makinda au JK mwenyewe.

Pinda Muongo au JK muongo?
Pinda juzi tu hapa aliachiwa zigo na JK na JK huyoooo! mawinguni akamwambia alishighulikie suala la posho. Kwa nini asishughulikie mwenyewe? Uwoga! Anajua akikubali itakula kwake kwa wananchi na sekta zingine za serikali zitadai. Akikataa, sijui makubaliano yake na wabunge juu kupitishwa kwa muswada wa katiba. Hapa nahisi ndipo penye mtego. Mkuu wa nchi anawaogopa sana wabunge kiasi kwamba hawezi kufanya maamuzi kinyume chao na ndiyo maana anajaribu kusukumia zigo lake kwa wengine. Hajawahi kuogopa wapiga kura bali wabunge.

Makinda Muongo au Kashililla Muongo:
Makinda alizungumzia jambo hili kwa ujasiri mkubwa akipingana na yale aliyosema profession wake (Kashililla). Makinda anajua JK hawezi kumwangusha kwa lolote kwani kwanza alishaahidi mkipitisha tu mambo yenu yatakuwa sawa (dhana yangu). Kwa hiyo Kashililla alikuwa hajui nyuma ya pazia kuna nini.

Zitto Mkweli na Ikulu ni wakweli:
Ni ukweli wa muda mfupi tu na madaktari wameingilia dili. Posho ilikuwa zitolewe ili mambo yaende sawa. Zitto ana haki ya kutafuta taarifa kwa njia zozote azijuazo. Na amepata kuwa JK hajaidhinisha. Wanaopinga shauri yao. Ukweli unabaki palepale na Ikulu imethibitisha...mnataka nini tena?

Unafiki wa viongozi ni kwa manufaa ya nani?
Kwa manufaa yao na matumbo yao. JK si kuwa anashaurika kihivyo, bali anataka kufunika kombe mwanaharamu apite. Ukwelii wa ndani ya moyo wa mkulu huyu ni kuwa hana tatizo na ongezeko la posho ya wabunge. Ana tatizo na wengine nao kudai. Hana priorities, anafanya kazi kulingana na situation ya wakati huo. Hupenda sana kufurahisha watu ndiyo maana hawezi na hatakuja kuweza kufanya maamuzi magumu juu ya nchi hii...mmeshaona na mtaniambia baada ya kipindi chake.

Watanzania tumeliwa, hatuna rais!!!!
 
Back
Top Bottom