Pinda, Muungano, na Hatima ya Zanzibar

Zanzibar will remain to be part of URT kwa sababu tangu mwaka 1964 sijasikia wazanzibari wakitaka kuvunja muungano kwa kutumia njia rasmi. Wazanzibari wanaihitaji bara kuliko bara inavyoihitaji Zanzibar.
Mwisho, historia ya Tanganyika na Zanzibar inadhihirisha wazi umuhimu wa muungano huo, kwani wengi waliopo sasa hivi visiwani humo ni jamii ya wabara waliohamishwa huko miaka mingi iliyopita.

Suwala linakuja hapa kuwa Uzanzibari si kuzaliwa Zanzibar bali ni ukaazi wa sehemu hiyo. Wazanzibari hawagombanii kuiondowa Zanzibar na kuiweka mbali na Bara hilo haliwezekani. SUALA hapa ni masilahi ya Zanzibar na wakazi wake . Hivyo tunategemea mkaazi wa Zanzibar akose huduma muhimu eti kwa sababu waliobara wanaamuwa maisha yao? Si mwenye damu ya Kiarabu, Kisukuma , Kizaramo au mkiristo au muislamu awepo pahala popote atakaeacha kutetea sehemu aliyopo iwe Mwanza, Kigoma, Pemba atakaeacha kuiteteyea sehemu anayoishi. Kwani hatuoni Wabunge wakigombana na mawaziri kutetea hadhi ya sehermu zao?
Ukiangalia kwa mtazamo huu ndio utaona wenye asili zote kule Zanzibar wanapigania Zanzibar na kwa bahati mbaya Serikali ya Muungano ni double Crosser. Inahubiri Utanzania kwa faida ya upande mmoja na kujivua madaraka ya upande wa pili katika masuala ya kuiendeleza Zanzibar. Wazanzibari wanahisi basi watumie kilicho chao (mfano mafuta) kujiendeleza. JEE WAUNGWANA HILO NI BAYA?
 
Mkira,
Jambo la kwanza wambie wajomba zako CCM waachilie uchaguzi wa haki na huru ili uone matokeo, hapo ndio utajua kua wa-zenj wanautaka muungano au la. Karume msimuonee jamani yeye hakuchaguliwa na wa-zenj amewekwa na kamati ya ccm Dodoma hili kila mtu anajua hata yeye mwenyewe, kwa hivyo usitegemee kua ana uwezo wa kuikataa amri ya ccm na waliomueka. Kwani Braza kweli haya ni mageni au hamyajui ? ZNZ haihitaji eti kwenda kwa Waarabu kwani waarabu wamo tayari ndani ya Znz infact ndani ya Ikulu, kwani huko bara hakuna waarabu kila mkoa. Mbona wewe wakuuma sana hawa waarabu? na pengine tukichunguza utaona lazima kapita / kaowa au kaolewa mwaraabu katika jadi zako. Wacha chuki na waarabu Marekani na nchi za ulaya ndio waliokua mbele kwenye ubaguzi wa rangi lakini haya huyaoni kwenye nchi za kiarabu. Tuulize sisi tunaokwenda Dubai kila wiki hal tunabaguliwa?
 
Kwa nini Visiwani wanakubali kuchaguliwa Raisi na CCM Dodoma?
Kwani huko Bara muna uhakika gani kama wananchi ndio waliomchagua kikwete? Au kwa sababu Kanisa ndio limesema kikwete ni chaguo la Mungu. at least visiwani wana uhakika na wanachokifanya isipokua uwezo wa kukataa kuchaguliwa rais ni mdogo. Hukumsikia Rais kikwete alipotembelea visiwani alivyosema ? Ati watu wa visiwani (ccm na cuf ) kazi yenu kwenye uchafuzi ni kutafuta wabunge na wakilishi , Raisi ni kazi yetu Dodoma. Braza yanayoendelea dodoma si mageni kwa wa-zenj.
 
Ukweli ni kuwa hata wao wanauhitaji huu muungano na umewasaidia mambo mengi tu ndo maana umeweza kuwepo toka 1964. Isije kuwa imeonekana kwasababu ya uwezekano wa neema ya mafuta, wajanja wachache wanataka kucapitalize kwa gharama za wazanzibar wote.
Mimi naona muhimu ni kuondoa kasoro za muungano na kusonga mbele.Ila kama wenzetu wanaona hilo haliwezekani, basi watangaze tarehe ya lini wanataka kujitoa maana hizi kelele zinachosha sasa. Tukumbuke jinsi watu tulivyokaa sehemu mbalimbali bila shida za hili Tatizo la wapi unakotoka.Naona Pinda hajakosea kwa hili!! Ukimya nao una kiasi.

Nini ushauri wako juu ya madini yanayotoka Bara na kuambiwa si ya Muungano?
 
Jamani wana JF,
Pinda naona amejibu vizuri. Viongozi wa Zenji wangekuwa na nia ya kuuimarisha Muungano wasingeenda public bila kuwa na makubaliano na wale wa SMT.

Wakati wa kuambizana ukweli umefika. Kama hawataki kuungana wajaribu kukaa pekeyao.Hayo mambo wanayalilia walishiriki kuyaongeza kwenye Katiba. Hakuna haja ya kuwabembeleza, watajiona tunawatetemekea

Mungu ibariki Tanzania na raia wake. Ameni

Hii unayozungumza wewe ni double standard. Mbona Wabunge wanazungumza mambo ya Serikali ndani ya Bunge. Wawakilishi wanamakosa gani kuyazungumza mambo ya Zanzibar kwenye BUNGE lao?
Serikali inaposhindwa kutekeleza matarajio ya wananchi wawakilishi wa wananchi wana haki ya kudadisi na kuonya. SMT na miungano kwa ujumla unawaangusha Wazanzibari na hivyo wawakilishi wao wana wajibu wa kuyazungumza. Na hili Public limetoka wapi kwa mambo ya Taifa?
 
kwa kweli viongozi wa zanzibar wamekuwa sio wastaarabu wana vikao rasmi wanavyoweza kuzungumzia kero za muungano lakini badala yake wamekuwa wakisema kwa kutumia lugha ambazo hazionyeshi dhamira safi ya muungano na sisi sasa tumeanza kuwajibu kwa jeuri ile ile wanyoitumia kama wanaona wananyanyasika wavunje ndoa hii maana vikao halali wanavipuuza lakini wajue wanzibari wengi ndio waliowekeza bara na wamenufaika katika shughuli zao ,sisi hatubababaiki au wakae kimya na mchele wa kyela watanunua kwa dola hongera Pinda

Haku8nana vikao halali vya kuzungumzia masuala ya Muungano zaidi ya Bunge na Baraza la Wawakilishi. Ustaarabu gani unaoutaka kutoka kwa viongozi wa Zanzibar huku unafurahia Wabunge wa Bara wakiiripua Serikali? Kwani kwa hili hakuna vikao rasmi? Sijui unaweza ukanieleza ni chombo gani chenye haki ya kuzungumzia Muungano zaidi ya Wananchi wenyewe na wawakilishi wao?
 
Tatizo la msingi wadau ni elimu finyu.Kama kuanzia asubuhi adi jioni watu wamekaa kwenye veranda wanajadili oooo tunaporwa mali zetu & mafuta na gesi na mengineyo yatabaki kuwa maneno matupu tu ujezi wa taifa si kwa kelele zisizokuwa na dira na jazba.Jijengeeni uwezo.Elimu bora kwa kizazi kijacho ndo msingi wa maendeleo mliyoikosa may be ilikuwa bahati mbaya lakini watoto wenu nao wasiikose ili nao wasibakie katika wimbi la kutoa lawama bali wawe chachu ya maendeleo.
Achana na udaku wa kutawaliwa kiroho kama wakati wa ukoloni. Hivyo hiyo elimu haitaki kugharamiwa? Gharama itatoka wapi iwapo kuna wengine wanahodhi kile ambacho kingesaidia kuleta mtaji wa kutowa elimu. Mawanzo hayo ya kusema kuwa watu wasidai haki zao na badala yake eti watafute elimu yatawasaidia nini wanaonyimwa haki hata hiyo ya kupata ekimu?
 
Pinda amesema vunjeni muungano muone.Ni kweli, jamani Zanzibar hakuna kitu; labda samaki ambao hata kuwavua taaabu kubwa. Hawa watu wamejazana bara. Kwao hakuna Ardhi yakutosha hakuna chochote. Chakula na hata kuni za kupikia vyote vinatoka bara ndiyo maana Pinda kasema Muungano ukivunjika watasaga meno. Ukweli unauma.

Pengine ungeacha kejeli zako na kwenda huko ili ukaoshe macho pengine ungeweza kujuwa ukweli. Fahamu tu kuwa machinga mliowafukuza Bara wote wamehamia huko.
 
Pinda kasema kile ambacho wengi tumekuwa tunakifikiria. Wazanzibari ambao wanataka muungano uvunjike ili wajiunge na FIFA, OIC, n.k. hawaoni mbali. Muungano ukivunjika ni rahisi watu wa bara labda kama laki moja wanaoishi na kufanya kazi Zanzibar kurudi nyumbani na yasitokee madhara yoyote. Je, tukisema Wazanzibar wote wanaoishi, kufanya kazi na biashara huku bara warudi kwao Zanzibar itatosha? Chakula chao kwa kiasi kikubwa kinatoka bara tena tunawaruhusu wenyewe waende Shinyanga, Kyela, Rukwa kununua na kupeleka visiwani bila ushuru wala bughudha. Je, wakija kama wanunuzi wa kutoka nje ya nchi wakatozwa VAT na ushuru mwingine Zanzibar patakalika? Kuna mtu aliwahi kusema kuwa wakazi wa visiwani popote pale duniani huwa wanaona maadui wanaokuja kuwavamia kutoka kila upande kila wakati. Kwa maneno mengine ni kwamba huwa wako insecure daima dumu. Na mimi nasema jaribuni muone. Mmetuchosha na vikelele vyenu.

Aisee mbona unajidanganya. Kwanza Zanzibar haijataka kuvunjika Muungano, wanachotaka mafuta yao watumie wenyewe. Kwani sasa Muungano si upo na mafuta hayapo tatizo ni nini tena?

Ama hili la Zanzibar kupata chakula Bara hilo si tatizo. Una umri gani Bwana Mdogio? Wakati wa Karume Mkubwa hakukuwa na biashara hii ya chakula baina ya pande mbili hizi na Zanzibar ilinawiri na kuendelea. Aidha kipindi kifupi kilichopita miaka ya mwanzo wa 1980 Bara kulikuwa na njaa na umasikini wa paka kula mkia wake na Zanzibar ikinawiri. Wakati huo Zanzibar ilikuwa ulaya kwa Bara. Mambo yalikuja kubadilika pale ASP ilipovunjwa kwa hila na kuanzia hapo kuididimiza Zanzibar kulianza.
Nakuhakikishia kuwa leo kama Bara wataamuwa kuuvunja Muungano Zanzibar itaanza kunyanyuka tena kwa haraka kwani SIRI KUBWA YA MAENDELEO YA NCHI NI KUWA NA UWEZO WA KUJIAMULIA MAMBO YAKE YENYEWE na hichi ndio inayoitwa SMT inajaribu kuinyima Zanzibar.
 
Mko tayari wapi mnatishia nyau tu. Maneno hayo ni ya wa unguja tu au pamoja na wapemba. Wapemba hawawezi kusema hivyo sababu nusu yao wako huku bara na ikiyokea hivyo wajue wanarudi kwao. Mnaonewa wapi? contribution yenu katika pato la taifa ni ngapi? chakula karibu chote kinatoka bara mnajua? HONGERA PINDA! Mbona hata sisi tumewachoka

Pili, mjue kabisa mkijitoa tu kwetu na pemba na uguja zinajitenga kila moja inakuwa nchi kivyake. Na mkipigana vita huko mmeshajitenga msikimbilie kwetu mkisema ni majirani zetu. Mnaitia doa nchi yetu kwa kupigana kwenu kila mara

Hivyo kabla ya kuja huu Muungano Wazanzibari waliishi vip? Hao wachache mnaowaonea choyo huko Bara hawawezi kuwafanya waliowengi wasidai haki yao. Hivyo mnawatumia hao kama kinga? Elewa kuwa hicho walichonacho kinawafaidia wao wakiwa huko kama nyinyi mlivyoenea nchi za watu kutafuta riziki.Wao wataamuwa kuishi huko au kurudi kwao kwani si watu kama Machupa wako tayari kuukana utaifa wao kwa kuangalia masilahi. Tunapozungumzia mambo ya Zanzibar tunakusudia masilahi ya wakaazi wa Visiwa vya Pemba na Unguja wakiwamo Wazaramo, Wanyamwezi, Wachaga na wengine wote waliotoka Bara ambao wanaishi Zanzibar
Hili la chakula kutoka Bara ni la kupangwa tu kwani chakula hicho hakiji bure bali kinanunuliwa hivyo kinaweza kununuliwa pengine popote ulimwenguni. Wazanzibari hawakuwa watumiaji wa vyakula vitokavyo bara wamejizoesha baada ya kukaa pamoja na ndugu zao wa Bara. Si kitu kigumu kuachana na magharage.
 
weeeeeeee acha kabisa zenj waachiwe nchi ile wamekwisha nawaambieni, hawataweza bora wajifiche tu ktk muungano, japo bara pia hatuupendi lakini kwa uvivu naoujua wa kule? duh ni balaa, sasa wazenj wao maduka sasa nani atazalisha nani atanunua? wabara kibao ndo wamechangamsha huko visiwani wala hakuna lolote, Pinda yupo right, sasa wananusa mafuta wanajidaii ooh hatuwataki, hata huo uongozi hapo tabu tupu! mbunge ana wakilisha watu 2500? hilo jimbo kijiji? na bado maendeleo anashindwa kuleta, ebu tulieni tumechoka hata kuwabeba na kodi zetu.

Wacha utoto wako. Hivyo mnashindiwa nini kuendeleza mikowa yenu na kukimbilia Zenj? Unataka kunambia kuwa mnakimbilia kufanywa manamba kule? Wazanzibari ni wavivu , maduka mnaendesha nyinyi sasa la kujiuliza pesa za matumizi mnatowa nyinyi na hayo maduka mnayoyaendesha mnayaendesha kwa mpango wa Cherity? Wallahi hujui unavyojitukana, eti unaacha kukaa kijijini kwenu wewe usie mvivu ukagombana na jembe badala yake unakimbilia Zanzibar kufanya umanamba. Unajitukana nafsi yako na wote wanaomtazamo kama wako na wala huwatukani hao wavivu wa Zanzibar.
 
bana eeeh!! mambo mengine kuosha vinywa tuu!! waache wajiungee yakhee! kwani shida iko wapi? wakifika FIFA wataambiwa nyie si mkoa wa Tanzania? sasa mnataka nini? labda kwa wakina OIC watawakubalia kwa sababu wavivu kufikiri!

Werevu husema thamani ya mtu inaonekana kwa mtazamo wake kwa ndugu yake.
 
Hawa wagunya hawa hawezi kufikiri sana maana wengi wao ni michicha tu .Eti wamesoma hahaha wapuuzi hawa wavaa kandambili .Akivaa suti na kikofia juu ? Waache wajaribu hawa .Tuwa waswaga wote na kujaza magereza bara wakiendelea na ujinga huu .Pinda acha tuwavumilie kidogo Mzee lakini umesha waonyesha kwamba wa wapuuzi .

Kutawaliwa bado kuko. Hata mtu akisahau rubega na kuifanya Suti ndio bwana ipo kazi.
 
Mkuu huyu mheshimiwa anafurahisha sana. Kila mwenye akili timamu anajua kuwa Zanzibar haiwezi kujiunga na OIC, hata watu wa Zanzibar wenyewe wanajua ni kuvunja sheria. Sera ya CCM na sheria ya nchi iko wazi, kama mtu anaongea najifurahisha tu, it will take kubadilisha sera ya chama na sheria za nchi kwa Zanzibar kujiunga na OIC. Sasa hapa mheshimiwa sijui kwanini anajaribu kuongelea kitu ambacho hana haja ya kukiongelea, anaacha kutwambia Kagoda vipi, mapendekezo ya tume ya Mwakyembe vipi......... Ni mtu ambaye tulikuwa na matumaini naye kuwa ataleta discipline serikali lakini naona naye anavutwa kwenye siasa za mipasho, na kuplay silent approach ya kushughulikia mambo. Huyu anasema hivi yule anasema hivi, inaonekana kuwa serikali siku hizi kila mtu muongeaji, leo waziri mkuu kesho mwakilishi zanzibar and so on and so on. Kweli tunaonesha utoto.

Kwani huu mnauita Muungano si wa nchi mbili? Akili ya mtu asiepotoshwa na choyo ni kuwa atamsikiliza mwenzake na pasipo muwafaka mtatafuta wenye busara na hata hilo likishindikana basi lengo la umoja halipo tena na ni bora mtafute njia nyengine ya ushirikiano. Unapoona mmoja anatunisha misuli kumtisha mwengine basi pana mushkeli hapo. Nafikirikuna upande una hoja ya ubabe na kuna upande kuna hojua ya kuonewa kwani ubabe mwenzake ni kuonea alie dhaifu.
 
Poleni Ngekewa na Mwiba kwa uchungu wa kutawaliwa; lakini bado sijaona jawabu la kujinasua, ndiyo maana tunasema hiyo ni porojo tupu.
 
Tatizo kubwa ambalo huwa naliona kwa watu wa kipande ile, ni kwamba katika kila argument wanayoleta wanasema wanapigania haki yao. HIVI HAKI YENU NININI? haki yenu ninini hata mnasema hivyo? hivi tz tunafaidika nini na hawa watu wasiofika hata milion moja? mbona mimi huwa nawaona ni kero tupu? kama muungano hawautaki, piga chini tuendelee na maisha kila mtu ya kwake. KITU CHA AJABU wazanzibar huwa wanafikiri watanzania wanaoishi bara wanawategemea kuwa bila wao hawawezi, kwa kifupu NI VIONGOZI WETU TU WANATUBURUTA, hata sisi hatuwataki kama nyinyi hamtaki kuwa pamoja na sisi. duniani kama mtu hataki kuambatana na wewe ni kuachana naye, na kama kuna kiongozi mwingine akiingia hapo nakwambia anaweza akawapiga chini ili muwe watu wa huko shelisheli labda. kama ni mafuta, hivi SIKU MKICHIMBA MAFUTA YAKAWA HAMNA, SISI HUKU BARA TUKACHIME HALAFU TUKAWAAMBIA TUNAVUNJA MUUNGANO mtajisikiaje? mbona akili zenu hazijakombolewa jamani?
 
Hivi wazanzibari mnasubiri nini kujitoa kwenye Muungano,kwasababu ninavyoona mimi wazanzibari wote hamuutaki muungano sasa kwanini msiseme jamani eenh sasa siye basi tunawaachia Tanganyika yenu na sisi tunabaki kama sisi.

Siku mkijiondoa kwenye Muungano huu,nafikiri mimi nitakuwa wa kwanza kufanya sherehe! Naona kero tu na huu muungano choko choko nyingi zisizo na faida wala nini kwa Taifa letu.

Kwa maneno ya Pinda nahisi hata Kikwete ameshachoka na hizi vurugu sema anasubiri tu Karume aje amwambie siye tunataka tubaki peke yetu amwambie SAWA. au kama Karume anaogopa kusema mwambieni hata amtume msema hovyo Ali Juma Shamhuna aje aseme kama hawataki muungano.

Zanzibar tunawambembeleza kama sijui kitu gani,mimi nafikiri ni muda muafaka to call it quit.

AMA KWELI! Kwani lengo lenu kwa Muungano lilikuwa lipi? Umoja au kuhodhi cha wenzenu? Wazanzibari wanataka kutumia kilicho chao ndani ya Muungano. Huu uungwana wa kutishia kuvunja Muungano hautajenga bali kubomoa tru. Zanzibar ilikuwepo kabla ya Muungano na haikuwahiu ku7tegemea Bara kwa lolote sasa hali ikirudia kama awali haitokuwa tabu kwao. Kwani hamuoni mifano ya nchi zilizokuwa katika Muungano wa Urussi mbali ya kubanwa bado wanaendelea.
 
Back
Top Bottom