Pinda afuta amri ya Waziri Magufuli

Pinda afuta amri ya Waziri Magufuli

Magufuli alidhani wamiliki halisi wa malori ni walalahoi wa kawaida, kumbe ni wale wale...
Sasa Magufuli ameingia 'choo cha kike, kichafu na kibovu' na huku anaumwa tumbo la kuharisha.
Chezea Riz moko wewe!!!
 
Magufuli na data za barabara zote, makandarasi, wafadhili na gharama za kila barabara....huyu jamaa alitaka Odinga Kenya ashinde halafu aje kumsaidia hapa ktk harakati za kusaka urais 2015, lkn sasa amechuja kinoma yaani baada ya jamaa kupigwa chini, Hotuba za Magufuli nyingi ni za kujipendekeza kwa rais aliyoko madarakani, alianza na Mkapa na sasa ni Kikwete. Huyo ndiyo Magufuli ninayemfahamu
 
Katika hili Magufuli asipojiuzuru nitamshangaa sana na kumdharau kupita maelezo.

Akiendelea kutaka kuwa waziri katika hali kama hii, Magufuli nitamfananisha na 'Mbwaa' muoga, kibogoyo, Kibutu anayebweka tu lakini haumi mtu!!
 
Azim Dewji bado ana machungu ya zile boti zake Magufuli alipompiga pini kupitisha kwenye lami kwenda Mwanza(boti zenyewe hata mwaka hazikumaliza tayari ni magofu pamoja na kelele nyingi) na hapa ndio alikuwa anataka kupoza machungu!!:A S-confused1:
 
GT wa JF majanga tu, badala ya kudai kila mtu afuate sheria wao wanashabikia watu waruhusiwe kuvunja sheria. Kuna baadhi ya maeneo hata hiyo rami wahaijui, lakn maeneo mengine barabara zinafumuliwa kila baada ya miaka mitatu badala ya miaka 13 normal life span ya barabara ya rami. Kwa mtu aliyewahi kuendesha barabara ya chalinze Ruvu atakubaliana na magufuli kuzuia magari yasibebe mzigo kupita viwango vilivyopendekezwa..
 
Kama ilivyotarajiwa, Serikali imesalimu amri! Sheria imepindwa, na sasa wenye malori ruksa kuendelea kuharibu barabara. Juzi niliyasema hapa Jukwaani kuwa nitashangaa kama Pinda ataunga mkono msimamo wa Magufuli. Huu ndiyo wakati mzuri kwa mtu kama Magufuli kujiuzulu maana kila anapojaribu kuafuata sheria, anapigwa nyundo ya utosi.

Magufuli has a metal block!! anafikiri uchumi wa nchi unajengwa na barabara nzuri tu zisizokuwa na vyombo vya usafiri!? Mara nyingi anakuwa na nia nzuri lakini top - down approach yake is very very detrimental to our national well being!
And he thinks he can develop Tanzania single handedly; Huyu JOHN POMBE"KALI" MAGUFULI has outlived his shelf life; its time for him to give way!
Barabara zenyewe anajenga sub standard kwa sababu ya 10%; the man can not listen to logic; too opinionated! hivi huyu Magufuli ni animist, a sadist, a chauvanist?! kwa nini hawezi kuzungumza na na binadamu wenzake akawasilikiza; wakamsikiliza tukapata muafaka?! kwa nini hajifunzi kutoka kwa Boss wake JK; mbona JK is more accomodating; more tolerant?! nani mkubwa baina ya JK na Magufuli!!????????????????; kwani yeye ndiye mwenye uchungu na nchi hii peke yake kuliko Rais?!
kwenye swala la barabara na bomoa bomoa zake aliaambiwa na JK na PM hadharani aache ubabe hakusikia!

what is wrong with this man!? this man needs psychiatric help probably!! msaidieni jamani!!

John Magufuli Tanzania sio yako peke yako; utaiacha. wisen up!

Adieu John Pombe Magufuli; God speed!
 
Malori "yanajenga nchi" kwa "kubomoa barabara"

Picha+5.jpg
 
Magufuli alidhani wamiliki halisi wa malori ni walalahoi wa kawaida, kumbe ni wale wale...
Sasa Magufuli ameingia 'choo cha kike, kichafu na kibovu' na huku anaumwa tumbo la kuharisha.
Chezea Riz moko wewe!!!
Tanzania ni yetu sote, hatuna haja ya kuwaendekeza baadhi ya watu kiasi kwamba wajione wao ni bora zaidi. Mkiendelea kumpa kichwa mjue ni kama mnamkatia tiketi ya kwenda ICC, maana atafanya hata mengine akijua yuko juu ya sharia.
 
Masisiem ni sawa na ukoo wa panya tu magufuli anataka kujifanya mwema eti ana uchungu na kodi ya mwananchi kwa ujenzi wa barabara analeta sheria zake za vichochoroni,ki ukweli sekta anayosimamia barabara zinajengwa chini ya kiwango ndio maana anaogopa kuumbuka,ile ya kilwa road ni malori gani yalipita?
Rwanda unapakia mzigo mpaka tani 100 hakuna barabara hata iliyo crack!!Aseme tu ukweli hizi 10% wanazopiga kwenye kupeana tenda ndio maana wanatengeneza barabara za kichina(fake) halafu anataka kuwin simpath ya raia wanyonge wa nchi hii!!!
Pinda nae kilaza tu kuingilia amri za wenzake hivi yale mashangingi siku hizi yameacha kununuliwa ama?
Shame on them....
 
barabara za highways zilizojengwa kwa kiwango cha kimataifa haziwezi kuharibiwa kwa uzito uliozidi 5% ya mzigo halali.makufuli anaogopa kuaibika kwa anachokifahamu,iwe iweje tusubiri 2016 ndipo tutajua mbivu na mbichi,tutajutia kujenga barabara za kichina,kubomoa hatutaweza,kukarabati hatutaweza.ni afadhali tuimarishe reli, ya uhuru,ya kati ,ya mwanza, ya kaskazini na tujenge ya kusini
tujenge barabara nyingi za changarawe ni rahisi kuzikarabati na chache za standadi za lam
i
 
Kama ilivyotarajiwa, Serikali imesalimu amri! Sheria imepindwa, na sasa wenye malori ruksa kuendelea kuharibu barabara. Juzi niliyasema hapa Jukwaani kuwa nitashangaa kama Pinda ataunga mkono msimamo wa Magufuli. Huu ndiyo wakati mzuri kwa mtu kama Magufuli kujiuzulu maana kila anapojaribu kuafuata sheria, anapigwa nyundo ya utosi.

Mkuu umenivunja mbavu!!! Pamoja na misimamo ya Magufuli isiyotetereka huwa akifikishwa hapa hana ubavu wa kujiuzulu na kujiwekea historia.
 
Magufuli alidhani wamiliki halisi wa malori ni walalahoi wa kawaida, kumbe ni wale wale...
Sasa Magufuli ameingia 'choo cha kike, kichafu na kibovu' na huku anaumwa tumbo la kuharisha.
Chezea Riz moko wewe!!!

Aisee hii kitu nimemsikia mmoja wa viongozi wa umoja wa wenye malori akisema redioni jana alipokuwa anahojiwa uko sahihi mkuu.
 
Kama ilivyotarajiwa, Serikali imesalimu amri! Sheria imepindwa, na sasa wenye malori ruksa kuendelea kuharibu barabara. Juzi niliyasema hapa Jukwaani kuwa nitashangaa kama Pinda ataunga mkono msimamo wa Magufuli. Huu ndiyo wakati mzuri kwa mtu kama Magufuli kujiuzulu maana kila anapojaribu kuafuata sheria, anapigwa nyundo ya utosi.

Sheria gani mtu mbabe sana huyu tena aliyejaa kejeli. Ajiuzulu mapema. Tumechoka na maneno yake yasiyo na busara. Wakati fulani rais alimshauri aache ubabe hakusikia na badala yake akasema wasio na nauli wapige mbizi. Kiongozi gani huyu? Anaongoza wizara kama nyumba yake. Ebo! Amelewa sifa. Hivi mlevi wa sifa mwenzake Mwakyembe amerudi India au? Mbona hasikiki tena baada ya kujipachika waziri wa madawa ya kulevya pamoja na sbughuli za TRA as though alikuwa waziri wa fedha?
 
Back
Top Bottom